Serikali Kutoa Muongozo wa Kuajiri Wanaojitolea

Serikali Kutoa Muongozo wa Kuajiri Wanaojitolea

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

SERIKALI KUTOA MUONGOZO WA KUAJIRI WANAOJITOLEA

Serikali imeeleza kuwa iko hatua za mwisho kukamilisha mwongozo utakaoangazia jinsi ya kuwaingiza katika mfumo watumishi wanaojitolea nchini.

Hayo yameelezwa, Jumatano, Januari 29, 2025, na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Deus Sangu, wakati akijibu swali la nyongeza la mbunge wa Lulindi (CCM), Issa Mchungahela.

Mchungahela amehoji Serikali inazungumziaje watumishi wanaojitolea katika kada mbalimbali, hususan ya elimu, ambako kuna watu waliojitolea kwa zaidi ya miaka 10.

Akijibu swali hilo, Sangu amesema jambo hilo limekuwa likizungumzwa mara kwa mara bungeni na kwamba Serikali iliahidi kulifanyia mchakato, ambao hivi sasa umefika katika hatua za mwisho.
 

Attachments

  • WhatsApp Video 2025-02-02 at 16.56.13.mp4
    4.1 MB
Wamejitolea kwa miaka 10, aisee

Sasa kama wanaajiri hao wanaojitolea bc wasije kutangaza nafasi za kazi afu vijana waanze kuomba wakati wana mpango wa kuajiri wanaojitolea.
 
Wamejitolea kwa miaka 10, aisee

Sasa kama wanaajiri hao wanaojitolea bc wasije kutangaza nafasi za kazi afu vijana waanze kuomba wakati wana mpango wa kuajiri wanaojitolea.
Nakuunga Mkono, kwa sababu itakuwa haina maana kuanzisha Ajiraportal,
Halafu hizo nafasi za kujitolea sio rahisi
 
Interviews zinaendelea nchi nzima za walimu...
Hao wanaojitolea waendelee tu.

Siasa..
 
Ni uamuzi mzuri japo unahitaji busara ya hali ya juu
Mfano: Unaweza kuta 95% ya waalimu wanaojitolea ni wa Kiswahili na Historia wakati somo lisilo na waalimu ni HESABU....
 

SERIKALI KUTOA MUONGOZO WA KUAJIRI WANAOJITOLEA

Serikali imeeleza kuwa iko hatua za mwisho kukamilisha mwongozo utakaoangazia jinsi ya kuwaingiza katika mfumo watumishi wanaojitolea nchini.

Hayo yameelezwa, Jumatano, Januari 29, 2025, na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Deus Sangu, wakati akijibu swali la nyongeza la mbunge wa Lulindi (CCM), Issa Mchungahela.

Mchungahela amehoji Serikali inazungumziaje watumishi wanaojitolea katika kada mbalimbali, hususan ya elimu, ambako kuna watu waliojitolea kwa zaidi ya miaka 10.

Akijibu swali hilo, Sangu amesema jambo hilo limekuwa likizungumzwa mara kwa mara bungeni na kwamba Serikali iliahidi kulifanyia mchakato, ambao hivi sasa umefika katika hatua za mwisho.
Cha ajabu wataletwa ambao hawajawahi kujitolea kabisa kisa WHO KNOW YOU.
 
Back
Top Bottom