Serikali kutoa ruzuku ya mbolea shilingi Bilioni 150

Serikali kutoa ruzuku ya mbolea shilingi Bilioni 150

benzemah

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2014
Posts
1,533
Reaction score
3,187
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa leo amelihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati akitoa hoja ya kuahirisha mkutano wa saba wa Bunge la 12 la jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Katika mengi aliyoyazungumzia mimi nimefurashishwa na kitendo cha Serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu kulenga kutumia kutumia Shilingi Bilioni 150 kama ruzuku ya mbolea kwa mazao yote.

Ameeleza kuwa mfumo wa utoaji wa ruzuku utawalenga wazalishaji wa ndani lakini amepigilia msumari kuwa makampuni ambayo hayataungana na Serikali katika mfumo huu Serikali hatutosita kuwafutia leseni ya kuendesha biashara ya mboloea nchini.

Hatua hii ni mkombozi mkubwa kwa wananchi zaidi ya asilimia 70 ambao wanategemea kilimo hapa nchini. Hatua hii pamoja na ongezeko kubwa katika bajeti ya Kilimo 2022/23 itakwenda kupunguza mfumuko wa bei ya chakula nchini, kuongeza eneo la umwagiliaji, kuongeza upatikanaji wa ajira kwa vijana na wanawake katika kilimo zitakazofikia milioni 1 ifikapo mwaka 2025.

Untitled design (13).jpg
 
Waziri wa Fedha ni Mwigulu Nchemba, halafu kwa Ruzuku hiyo ya billion 150, kwa vyovyote vile kila mfuko wa Mbolea punguzo lake itakuwa Tzs 100. Mwingulu ana Akili ya U- CCM halisi. Acha Ruzuku ya Serikali iliwe na CCM na COVID-19 tu.
 
Hapa zitapigwa na wajanja maana nadhani 2008-2014 walikuwa na kitu kinaitwa DADPs, watu walikuwa wanalipana posho pekee
 
Waziri wa Fedha ni Mwigulu Nchemba, halafu kwa Ruzuku hiyo ya billion 150, kwa vyovyote vile kila mfuko wa Mbolea punguzo lake itakuwa Tzs 100. Mwingulu ana Akili ya U- CCM halisi. Acha Ruzuku ya Serikali iliwe na CCM na COVID-19 tu.
Hata hiyo itapigwa kwenye posho na ufisadi, kilimo kwanza na DADPs zilifia wapi?
 
Hizo ni kanjanja serikali ya ccm iko vizuri kwenye kutaja figa subiri utekelezaji. Tutaambiwa pesa zilizoenda ni robo ya makisio huku, ndani ya iyo robo kutakuwa na wizi wa hizo pesa
 
Jambo la heri kwa wakulima

Tunasubiri kuona utekelezaji sasa

Ova
 
Back
Top Bottom