Serikali kuu 3: Serikali ya Tanganyika, Serikali ya Zanzibar na Serikali ya Muungano Tanzania?

Serikali kuu 3: Serikali ya Tanganyika, Serikali ya Zanzibar na Serikali ya Muungano Tanzania?

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
42,872
Reaction score
34,363
TAFADHALI USININUKUU




JJ_af456.jpg





Ndugu zangu,

Haiyumkini Majaji wetu hawa wazaliwa na wazalendo wa nchi hii wakawa wote wana matatizo katika kufikiri kwao;

Jaji Francis Nyalali, Jaji Robert Kissanga, Jaji Joseph Warioba na Jaji Augustine Ramadhan . Wote hawa

wamependekeza mfumo wa Serikali Tatu ili kuunusuru na kuuimarisha Muungano wetu.

Nahofia, kuwa baadhi ya wanasiasa wetu ndio wenye matatizo katika kufikiri kwao. Kwamba wanaangalia kwanza

ni mfumo gani wa Serikali utakaowanufaisha wao binafsi, makundi yao na vyama vyao kwa kuangalia namna

watavyoshinda chaguzi za kisiasa na kushika madaraka. Wanaangalia zaidi leo na kesho. Kwao kesho kutwa na

mtondogoo ni mbali sana." - Tafadhali Usininukuu.

Maggid Mjengwa,
Dar es Salaam
0754 678 252.(P.T)
Chanzo.
http://mjengwablog.com/habari-za-kijamii/item/8406-tafadhali-usininukuu.html#.UtQ7F2RPIa5
 
Sijakunukuu lakini nimekuelewa Mjengwa. Ifike mahali,tasnia ziheshimiwe.Huu mtindo wa wanasiasa kujifanya wanajua kila kitu si mzuri hata kidogo.Katiba ni suala hasa la kisheria. Ingawa kuna chembechembe za tasnia nyingine mbalimbali. Lakini,kama magwiji wa Sheria hao wote wameona hivyo,nani mbobezi zaidi wa kushindana nao?

Tena kuna hata Wahadhiri Waandamizi na Wasomi hasa wa Katiba mfano wa Prof.Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi na Hayati Dr.Sengondo Adrian Mwarabu Mvungi. Hawa wapinzani wa wazo hili pevu la Serikali tatu wanataka nini tena? Wanasiasa ndio wanaotuharibia baadhi ya vitu hapa nchini.Siasa iwe na mipaka yake.Si kila mahali.

Kwa hili la Katiba, wanasiasa watusaidie tu kuipata.Si kuvuruga. Wakituvurugia,tutawavurugia na kutavurugika
 
kweli mmesema yote. Wanasiasa wanadhani wao ndio vijogoo katika kila kitu. Angalia CCM wanavyopingana hata na mwenyekigoda wao, ufinyu wa kufikiri na utapiamlo wa mawazo tu ndio tatizo hapa.
 
Ikiwa Zanzibar wana serikali yao kwa nini Tanganyika tusiwe nasi na serikali yetu halafu tukawa na serikali inayotuunganisha, Mimi naona ni sawa na ni halali, kwani tukiachia kuwa na serikali mbili watakao kula hasara ni sisi wa Tanganyika. Mungu atusaidia.
 
serikali tatu inachanganua mipaka ya muungano. Tubadilike watanganyika, kwan raisi wa tanganyika atakuwa simba? Kwa kweli ikija tanganyika zile chokochoko za wamdebwedo zitapungua
"TRUST ME MAN"
 
Unaweza fahamu hii place?????
 

Attachments

  • ImageUploadedByJamiiForums1390289660.586929.jpg
    ImageUploadedByJamiiForums1390289660.586929.jpg
    105 KB · Views: 84
Muungano ni wa nchi zaidi ya moja, sasa kama mmoja wa hao wanaotaka kuungana akighaili basi haiwezekani kuwepo muungano!!! Wazanzibari wao wameishasema kuwa hawautaki muungano wa serikali mbili sasa hawa wanachama wa magamba wahafidhina kwanini hawataki kuelewa kuwa hawawezi kuwashurutisha wazenj kuwa na serikali mbili!!! Kama wanataka kuheshimu sera yao ya kuimalisha na kuenzi wanayoiita TUNU ya muungano basi hawana budi kufuata ushauri wa mwenyekiti wao kuwa wajiandae kisaikolojia kuwa na serikali TATU!!!.
 
TAFADHALI USININUKUU




JJ_af456.jpg





Ndugu zangu,

Haiyumkini Majaji wetu hawa wazaliwa na wazalendo wa nchi hii wakawa wote wana matatizo katika kufikiri kwao;

Jaji Francis Nyalali, Jaji Robert Kissanga, Jaji Joseph Warioba na Jaji Augustine Ramadhan . Wote hawa

wamependekeza mfumo wa Serikali Tatu ili kuunusuru na kuuimarisha Muungano wetu.

Nahofia, kuwa baadhi ya wanasiasa wetu ndio wenye matatizo katika kufikiri kwao. Kwamba wanaangalia kwanza

ni mfumo gani wa Serikali utakaowanufaisha wao binafsi, makundi yao na vyama vyao kwa kuangalia namna

watavyoshinda chaguzi za kisiasa na kushika madaraka. Wanaangalia zaidi leo na kesho. Kwao kesho kutwa na

mtondogoo ni mbali sana." - Tafadhali Usininukuu.

Maggid Mjengwa,
Dar es Salaam
0754 678 252.(P.T)
Chanzo.
http://mjengwablog.com/habari-za-kijamii/item/8406-tafadhali-usininukuu.html#.UtQ7F2RPIa5



Zanzibar ndio wanaoongoza mwelekeo wa hii katiba mpya. Zanzibar hawataki Serikali moja. Kule Zanzibar kuna mgawanyiko mkubwa kuhusu Serikali mbili. CCM ingependa status Quo--yaani mambo yaende kama zamani; tuendelee na serikali mbili. CUF na wengine hawataki status Quo. Dawa ni kuleta serikali tatu kunusuru muungano.

Ishu ambayo tungekuwa tunajadii ni hii: Tuwe na serikali tatu za aina gani? Kama CCM wanadhani wataburuza Watanzania kukubali serikali mbili hii ni ndoto ya ndaria kabisa.

Tanzania kubakisha jina hili tujadili ni aina gani ya serikali tatu tunataka. Mimi napendekeza Federal states tatu kuunda Tanzania: Pemba State, Unguja State, na Tanganyika State. Hizi state tatu ndo ziunde United Republic of Tanzania. Hii ndo itakuwa njia sahihi ya kuuokoa muungano wetu katika katiba mpya.

Nimeitenga Pemba kutoka Zanzibar kwa sababu najua hawa watu hawaelewani kwa sababu za kidini. Pemba ni siasa kali wakati ambapo Unguja ni moderates kidini. Hivi visiwa viwili hawapikikipi chungu kimoja hata kidogo. Kuna wakati hata nimekuwa na mashaka vitendo vya kigaidi vyote tumesikia vikitokea Zanzibar vina mizizi yake kutoka Pemba. Kwa hiyo pengine ni vizuri tukawatenga tu kungali mapema kila mtu awe na State yake kikatiba waendelee tu kutegemeana kiuchumi kama ambavyo wamelazimishwa na mazingira miaka yote.


Mwisho wa Mada: CCM isahau kabisaaaa, wazo la serikali mbili. Its gone with the wind.... Njoeni tujadili ni serikali tatu za aina gani tunataka, badala ya kudhani serikali mbili zitarudi. Hizo ndo zishapitwa na wakati hivyo.......
 
Muungano ni wa nchi zaidi ya moja, sasa kama mmoja wa hao wanaotaka kuungana akighaili basi haiwezekani kuwepo muungano!!! Wazanzibari wao wameishasema kuwa hawautaki muungano wa serikali mbili sasa hawa wanachama wa magamba wahafidhina kwanini hawataki kuelewa kuwa hawawezi kuwashurutisha wazenj kuwa na serikali mbili!!! Kama wanataka kuheshimu sera yao ya kuimalisha na kuenzi wanayoiita TUNU ya muungano basi hawana budi kufuata ushauri wa mwenyekiti wao kuwa wajiandae kisaikolojia kuwa na serikali TATU!!!.

Hata wa Serikali tatu hawana utashi nao: "wao" wanataka madaraka kamili ya Zanzibar na "muungano wa mkataba".
 
Wakuu, hao wanaovuma kama Wazanzibari wakiongozwa na CUF, hawaitaki Tanzania. Ni sisi huku Tanganyika pamoja na CCM ndio tunaohangaika kui"save" Tanzania (JMT). Wao wanachohitaji hasa ni madaraka kamili ya serikali yao ya Zanzibar. Hii habari ya serikali tatu ni tapatapa ya CCM na baadhi ya Watanganyika ambao bado tunashindwa kukubali kuipoteza JMT. Wazanzibari hao hawahangaiki na hoja hii; wanachoangalia ni kama huo mfumo (wa serikali 3) utawakwamisha kwenye lengo lao la kushika hatamu kikamilifu. Hapo ndipo watakapoupinga kwa nguvu zote. Hawa watu wamepania madaraka ya kiserikali kwa nia moja.
 
Wakuu, hao wanaovuma kama Wazanzibari wakiongozwa na CUF, hawaitaki Tanzania. Ni sisi huku Tanganyika pamoja na CCM ndio tunaohangaika kui"save" Tanzania (JMT). Wao wanachohitaji hasa ni madaraka kamili ya serikali yao ya Zanzibar. Hii habari ya serikali tatu ni tapatapa ya CCM na baadhi ya Watanganyika ambao bado tunashindwa kukubali kuipoteza JMT. Wazanzibari hao hawahangaiki na hoja hii; wanachoangalia ni kama huo mfumo (wa serikali 3) utawakwamisha kwenye lengo lao la kushika hatamu kikamilifu. Hapo ndipo watakapoupinga kwa nguvu zote. Hawa watu wamepania madaraka ya kiserikali kwa nia moja.

Mkuu, wewe umepiga mulemule penyewe; Wazanzibari hao uliowasema ndio ambao hawautaki muungano, na sababu kubwa ni za kidini tu, ingawa wengi hawasemi wazi lakini huo ndio ukweli.

Nchi hii bado haijampata mtu jasiri kama Nyerere wa kulisema hili kwa uwazi, wengi wanalizungumza ku-"save" tu face zao, na hili ndilo tatizo kubwa kuliko yote!

Watanzania (bara na visiwani) tunashindwa sasa kujiona kama Taifa moja na badala yake tunaanza sasa kujitambulisha kwa udini kwa kisingizio cha usehemu, upuuzi mtupu!

Hata hizi serikali tatu ni panadol tu kwenye kutibu malaria, dawa ni kuondokana kabisa na Zanzibar na Tanganyika ili tubaki na Tanzania pekee. Hizi nyinginezo hatuna budi kuzitunza vizuri kwenye vitabu vya historia!

Nyerere na Karume walifanya jambo moja zuri linalotuhitaji sisi wa kizazi hiki kufanya ziada iliyobaki, badala yake sisi (kwa usomi na utaalam wetu) tumeamua kuharibu jambo jema lililoanzishwa na waasisi hawa.

Muungano ulio imara ni suala la utashi wa kisiasa na kamwe sio jambo la kisheria kama wengi wanavyojaribu kutuaminisha hapa. Sheria hufuata katika kuyaweka sawa makubaliano hayo ya kisiasa.

Nyerere na Karume kama wanasiasa wa wakati ule walifanya maamuzi yale vema; lililotakiwa kwa sasa ni wanasiasa wetu kupambanua nini dhamira yao ya kutuunganisha watanzania wote chini ya mwavuli mmoja badala ya utitiri huu wa serikali ambao nina hakika kuwa huko tuendako patachimbika tu, maana hapa tulipofika ndo tumelikoroga kabisaaa!!!!
 
Muungano ni wa nchi zaidi ya moja, sasa kama mmoja wa hao wanaotaka kuungana akighaili basi haiwezekani kuwepo muungano!!! Wazanzibari wao wameishasema kuwa hawautaki muungano wa serikali mbili sasa hawa wanachama wa magamba wahafidhina kwanini hawataki kuelewa kuwa hawawezi kuwashurutisha wazenj kuwa na serikali mbili!!! Kama wanataka kuheshimu sera yao ya kuimalisha na kuenzi wanayoiita TUNU ya muungano basi hawana budi kufuata ushauri wa mwenyekiti wao kuwa wajiandae kisaikolojia kuwa na serikali TATU!!!.

Wazanzibari muungano wanautaka. Lakini si kwa mfumo huu uliopo ambao wanauona unapendelea kikundi kimoja cha watu kule Zanzibar na kuwaacha wengine wakiwa hawana manufaa na huo muungano. Serikali tatu ndo njia sahihi ya kuachana na mfumo unaoleta shida. Vyama vyote vianze kujadili ni aina gani ya serikali tatu tuwe nayo. Wazo la Serikali mbili ni mfu kabisa. Kama kuna mtu anafikiri itawezekana anajidanganya. Tujadili tuunde serikali tatu za namna gani. hilo ndilo la kulijadili hapa.
 
Mwl. Nyerere na Mh. Karume, walikaa pamoja na mabaraza yaliokuwa yanaongoza nchi zao. Wakawaza kuunganisha vyama viwili vilivyoongoza nchi zao. Wakavifanya kuwa chama kimoja.
Wangeweza kuviimarisha vyema kabisa, ASP na TANU, tangu Zanzibar hadi Kigoma, Pemba hadi Ukerewe. Lakini wakasema, kama huu wetu ni muungano, tuwe na chama kimoja. Tukaupata muungano wa vyama viwili ASP na TANU vikafa milele na kufufuka kama CCM. Kikakubalika kila pahali Tanzania nzima. HUO NDO MUUNGANO.
Ajabu ni pale Tanganyika inasema imeungana na Zanzibar halafu zikafa kifa urongo zikafufuka vichwa viwili. Kimoja kikafa kabisa (Tanganyika) hakikufufuka, lakini kile cha Zanzibar kimefufuka pamoja na cha muungano. Sasa hapa tuna vichwa viwili. Muungano na Zanzibar.
Wanasiasa wanatuona siye mabwe.ge hatujui kuona mambo. Wamesharuhusu Zanzibar kusimama yenyewe ila Tanganyika isiamshwe kabisaaa. Zanzibar, tayari wana kila kitu chao cha dola kasoro kuambiwa tunaomba mtuambie bado mpo na sisi? Wao hawana haja ya muungano wenu.
To cut things short; let me say this, kwa sasa, na kwa hali ya Zanzibar ilivyo, Serekali ya ccm imeuvunja muungano kwa kuruhusu Zanzibar kurudi kufukua yaliokuwa yamezikwa. Laiti wangeyaacha kama walivyo acha yale ya ASP na TANU. Kwani walijua wakisema (1992) tuvirudishe vyama vyetu vya kale Nyerere angewastukia.
Dawa; Ni Serekali moja tuu ya Muungano wa Tanzania. Huu ndo muungano. Serekali 3 au 4 (Tanganyika +Unguja+Pemba) ni uongo. Huo sio muungano ni shirikisho. Tutangaze kuwa tumetoka kwenye muungano tukaenda shirikisho. Full Stop. Ni mawazo yangu tu
 
wwe kweli mburula hata historia huijui, wapi karume na nyerere waliunganisha vyama kwa taarifa yako karume aligoma kuunganisha vyama alijua nyerere ni laghai na anataka kuimeza znz kwa mgongo wa siasa na ilitokea mwaka mzima karume hakusema na nyerere na muungano ulikua hatarini kuvunjika uliza upewe data ucikurupuke na hili ndo tatizo la wadanganyika wengi mnangalia maneno ya nyerere kuliko fact halisi katika dunia hii nani anakana utaifa wake kama sio nyinyi na mwalimu wenu uzaledo na nchi yake hana na huo ndio urithi wenu kutoka kwa baba yenu. cc tutabakia wazanzibari na nyinyi watanganyika hata kma mnamkana mama yenu alie wazaa. Zanzibar Kwanza Tz shengesha baadae
 
Back
Top Bottom