Serikali kuzuia mazao kuuzwa nje kutadumaza kilimo na kuvuruga uchumi

Serikali kuzuia mazao kuuzwa nje kutadumaza kilimo na kuvuruga uchumi

chinchilla coat

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2016
Posts
5,107
Reaction score
10,969
Wadau kwema? Kumekuwa na miito ya baadhi ya watu wakitaka serikali izuie watu kuuza chakula nje ya nchi ili kukabiliana na tatizo la bei ya chakula kupanda.

Sina uhakika sana kama hilo litachangia kushusha bei ya vyakula likifanyika sasa hivi, ila nina uhakika litarudisha nyuma sekta ya kilimo kwa kiasi kikubwa.

Kwa nini? Sekta ya kilimo kwa Tanzania ipo chini sababu ya bei ya mazao mara nyingi kuwa chini na haimlipi mkulima na hata kuna kipindi hairudishi hata gharama za kilimo, sababu ni ukosefu wa masoko yanayoeleweka.

Na hii hufanya watu wengi wasite kuwekeza kwenye kilimo kwa sababu faida yake ni ndogo ukilinganisha na risk na effort anyotumia na kupelekea kilimo cha Tanzania kuwa duni ama kufanywa tu na wakulima wadogo wadogo kwa ajili ya kupata chakula na sio biashara.

Mtu akiwa na milioni zake 200 anaona ni afadhali awe anaingiza bidhaa za kichina nchini kuliko kufanya kilimo sababu kilimo hakilipi.

So matokeo yake nchi inakua ya wachuuzi zaidi kuliko wazalishaji, na ndio maana tunaona nchi imetapakaa machinga kila kona na kwa sababu hii.

Sasa mbinu pekee ya kweli kupunguza bei ya vyakula ama bei ya kitu chochote ni kuongeza supply tu na sio kudhibiti soko.

Na bei za mwaka huu kuwa juu ni mauamivu kwa baadhi ya watu lakini ni neema pia kwa sababu itawapa wakulima mapato na mtaji na nguvu zaidi kuwekeza zaidi kwenye kilimo kipindi kijacho itakayopelekea supply kuongezeka.

Pia inaweza kuwashawishi watu ambao wana mitaji ila hawataki kuwekeza kwenye kilimo kuanza kufikiria kuhusu kuingia kwenye kilimo.

Serikali inaweza kuzuia baa la njaa kwa kuwahimiza wakulima kuweka akiba na kununua kutoka kwa wakulima kwa ajili ya akiba ila sio kuzuia soko la nje.

Kilimo ndio sekta ambayo itatuingizia fedha za kigeni, itaajiri watu wengi na kouondoa umasikini kama tukitumia vizuri.
 
Serikali ya watu wenye akili na inayokngizwa na Rais Samia haiwezi kufanya huo ujinga..

Awamu ya 6 inatambua kilimo kama Biashara na Sio kujikomu at expense of wakulima maskini..

Kwa muktadha huo kamwe haitafunga mipaka,watu walime na wauze Kisha wanufaike na jasho lao..Hili itapunguzia mzigo hata serikali wa kununua Mazao Kutoka Kwa wakulima Nje ya mahitaji halisi..

Leo tunavyoongea Mchele umekuwa zao kuu la exports na kushinda korosho naazao mengine yaliyozoeleka 👇
 

Attachments

  • Screenshot_20220713-184512.png
    Screenshot_20220713-184512.png
    130.7 KB · Views: 9
  • Screenshot_20220713-184653.png
    Screenshot_20220713-184653.png
    34.3 KB · Views: 10
Serikali ya watu wenye akili na inayokngizwa na Rais Samia haiwezi kufanya huo ujinga..

Awamu ya 6 inatambua kilimo kama Biashara na Sio kujikomu at expense of wakulima maskini..

Kwa muktadha huo kamwe haitafunga mipaka,watu walime na wauze Kisha wanufaike na jasho lao..Hili itapunguzia mzigo hata serikali wa kununua Mazao Kutoka Kwa wakulima Nje ya mahitaji halisi..

Leo tunavyoongea Mchele umekuwa zao kuu la exports na kushinda korosho naazao mengine yaliyozoeleka 👇
Naam, jambo jema hili
 
Wadau kwema? Kumekuwa na miito ya baadhi ya watu wakitaka serikali izuie watu kuuza chakula nje ya nchi ili kukabiliana na tatizo la bei ya chakula kupanda.

Sina uhakika sana kama hilo litachangia kushusha bei ya vyakula likifanyika sasa hivi, ila nina uhakika litarudisha nyuma sekta ya kilimo kwa kiasi kikubwa.

Kwa nini? Sekta ya kilimo kwa Tanzania ipo chini sababu ya bei ya mazao mara nyingi kuwa chini na haimlipi mkulima na hata kuna kipindi hairudishi hata gharama za kilimo, sababu ni ukosefu wa masoko yanayoeleweka.

Na hii hufanya watu wengi wasite kuwekeza kwenye kilimo kwa sababu faida yake ni ndogo ukilinganisha na risk na effort anyotumia na kupelekea kilimo cha Tanzania kuwa duni ama kufanywa tu na wakulima wadogo wadogo kwa ajili ya kupata chakula na sio biashara.

Mtu akiwa na milioni zake 200 anaona ni afadhali awe anaingiza bidhaa za kichina nchini kuliko kufanya kilimo sababu kilimo hakilipi.

So matokeo yake nchi inakua ya wachuuzi zaidi kuliko wazalishaji, na ndio maana tunaona nchi imetapakaa machinga kila kona na kwa sababu hii.

Sasa mbinu pekee ya kweli kupunguza bei ya vyakula ama bei ya kitu chochote ni kuongeza supply tu na sio kudhibiti soko.

Na bei za mwaka huu kuwa juu ni mauamivu kwa baadhi ya watu lakini ni neema pia kwa sababu itawapa wakulima mapato na mtaji na nguvu zaidi kuwekeza zaidi kwenye kilimo kipindi kijacho itakayopelekea supply kuongezeka.

Pia inaweza kuwashawishi watu ambao wana mitaji ila hawataki kuwekeza kwenye kilimo kuanza kufikiria kuhusu kuingia kwenye kilimo.

Serikali inaweza kuzuia baa la njaa kwa kuwahimiza wakulima kuweka akiba na kununua kutoka kwa wakulima kwa ajili ya akiba ila sio kuzuia soko la nje.

Kilimo ndio sekta ambayo itatuingizia fedha za kigeni, itaajiri watu wengi na kouondoa umasikini kama tukitumia vizuri.
Mkuu umeongea point sana. Maana kulikuwa na thread iliyokuwa ikimwomba Mheshimiwa Rais Samia Suluhu azuie chakula kisiuzwe nje. Binafsi kama Mkulima Mdogo anayepambana ili kuzalisha kwa wingi nilikerwa sana na maudhui yaliyokuwemo kwenye thread ile. Ili uweze kufanya shughuli za kiuchumi kwa uhakika ziachie Demand and Supply zifanye kazi, kuliko kuanza kutumia nguvu itakayowakatisha tamaa wananchi wengi kuwekeza kwenye kilimo. Binafsi nimefurahi kuona kwamba Wakulima Wadogo tunaanza kutumia mbinu za umwagiliaji ili kupambana na ukame na kuongeza uzalishaji. Zaidi, Kazi iendeleee!
 
Hii hali ya mavuno, chakula na bei zake ziendelee vivihivi kwa maslahi mapana ya wakulima wa Tanzania. Anayechukia au anayeona bei ziko juu akalime mwenyewe. Sio suala la kufurahisha wavivu "wengi" waliopo mtaani bila shughuli ya kuwaingizia kipato.

Wenye vipato waendelee kununua na kula kwa fahari!!!!
 
Hii hali ya mavuno, chakula na bei zake ziendelee vivihivi kwa maslahi mapana ya wakulima wa Tanzania. Anayechukia au anayeona bei ziko juu akalime mwenyewe. Sio suala la kufurahisha wavivu "wengi" waliopo mtaani bila shughuli ya kuwaingizia kipato.

Wenye vipato waendelee kununua na kula kwa fahari!!!!
Njia ya kushusha bei ya vyakula ni kuongeza uzalishaji basi, na hii inamaanisha watu wengi zaidi walime
 
Back
Top Bottom