Serikali Mbili Kamwe Haziwezi Kutatua Kero za Muungano!. Ni Ama Serikali 3! Ama Serikali 1

Serikali Mbili Kamwe Haziwezi Kutatua Kero za Muungano!. Ni Ama Serikali 3! Ama Serikali 1

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Wanabodi,

Huku mivutano kuhusu muundo wa muungano ukiendelea, nimefazifanyia tathmini ndogo kero za muungano kwa pande zote, nikajiridhisha pasi shaka, kuwa Jaji Warioba yuko very right!, muundo wa serikali mbili, licha ya kushindwa kumaliza kero za muungano kwa kipindi cha miaka 50 iliyopita!, hivyo nimejiridhisha kuwa muundo wa serikali mbili, kamwe, hauwezi kutatua kero hizo, hata zikipewa kipindi cha miaka 100 mingine!. Dawa ya kudumu ya kupunguza kero hizo, japo sio kuzimaliza kabisa ni serikali 3, ila suluhisho la kudumu, na dawa ya kutibu kwa kuzimaliza kabisa, kero za muungano, ni serikali moja! ambayo inaunda nchi moja chini ya rais mmoja!.

Naomba niwapitishe very briefly kwenye baadhi ya kero hizi.


  1. Kutokuwa na Uwazi wa Mapato na Matumizi wa Fedha za Jamhuri ya Muungano, kwa sababu serikali ya Muungano pia ndio serikali ya Tanganyika!, hakuna any dividing line zipi ni gharama za Tanganyika na zipi ni gharama za muungano!, serikali mbili haziwezi kutatua hili milele!. Dawa ni ama serikali tatu hivyo gharama za Tanganyika zitajulikana, and the same applies to mapato, kwa sasa Tanganyika pekee ndio tunagharimia muungano!, Its about time sasa kila mtu aubebe mzigo wake mwenyewe!.
  2. Kutokuwa na Akaunti ya Pamoja. Hili lilishindikana kwa sababu fedha za Tanganyika pia ndizo pekee zimekuwa zikigharimia muungano!, uwe na account ya pamoja ya nini wakati Zanzibar haitoi single cent?. Serikali tatu ndio suluhisho la tatizo hili account itafunguliwa Serikali ya Tanganyika itatiamo fedha na Zanzibar italazimika, huu ndio utakuwa mwisho wa dezo dezo!.
  3. Uwepo wa Mkanganyiko wa Mapato jinsi ya kuchangia gharama uendeshaji wa Serikali zote mbili utamalizwa kwa kuinyofoa serikali ya Tanganyika ndani ya serikali ya muungano!.
  4. Kuwepo kwa Tume mbili zinazoshindana katika Nchi moja pia kutaondolewa kama kila mtu atakuwa kivyake vyake!.
  5. Zanzibar kutoshirikishwa kikamilifu na Serikali ya Jamhuri ya Muungano katika mchakato wa kupata misaada kutoka kwa Nchi za nje nako pia kutamalizikia kwa sababu misaada sio jambo la muungano, kwa sasa tunawapa Zanzibar asilimia 4.5 ya misaada yote ya Tanzania!. Kila mtu atajitafutia, na huu ndio utakuwa mwisho wa watu kujivunia wasichokipanda, kujipakulia wasichokipika, na kujilia vya watu!.
  6. Malalamiko kuwa Viongozi Wakuu wa Zanzibar wanachaguliwa Dodoma na sio Zanzibar nako pia kutaisha, mambo yote ya Zanzibar sasa yatakuwa yao wenyewe!.
  7. Zanzibar kulalamika kuwa kuna baadi ya mambo yamefanywa kuwa ya Muungano kupitia kutungwa kwa Sheria ya Bunge la Jamhuri ya Muungano na baada ya hapo mambo hayo huwa katika utatanishi, hili nalo litakwisha.
  8. Kitendo cha Zanzibar kuwa nchi huru, inabendera yake, ina wimbo wa Taifa, Serikali yake na imebadili Katiba yake kutambuliwa kama Nchi kutamalizwa kwa serikali moja!, serikali mbili au tatu, haziwezi kutatua hili, huwezi kuwa na muungano wa nchi mbili halafu bado zikabaki nchi mbili!.
  9. Kitendo cha Zanzibar kubadili masharti ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano ambayo inasema Sheria za Muungano zinazotungwa na Bunge hilo,zitumike sehemu zote, badala yake Katiba ya Zanzibar inaelekeza kuwa ili Sheria
  10. itumike Zanzibar Sharti ipelekwe kwenye Baraza la Muungano ni lazima kikemewe na kuadabishwa!. Katiba ya JMT ndio supreme!. Hili pia haliwezi kumalizwa na serikali mbili wala tatu, bali dawa ya hili ni serikali moja!.
  11. Hili la Zanzibar kutunga Sheria kuhusu Fedha, ambalo ni suala lililopo kwenye Katiba ya Muungano pia litamalizwa na serikali moja!.
  12. Hili la Zanzibar kutunga Katiba ambayo imechukua Madaraka ya Rais yaliyopo kwenye Jamhuri ya Muungano,inaeleza kwamba Rais wa Jamhuri ya Muungano anamadaraka ya kugawa Nchi katika maeneo ya Kiutawala, mabadiliko ya kumi ya Katiba ya Zanzibar ya 1984 yametambua kuwa Zanzibar ni Nchi na yamempatia Rais wa Zanzibar mamlaka ya Kuigawa Nchi katika meneo ya Muungano litamalizwa kwa serikali tatu!.
  13. Hili la Katiba ya Zanzibar inaeleza Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Nchi mbili lakini Katiba ya Jamhuri inaeleza kuwa Tanzania ni Nchi moja haliwezi kumalizwa kwa serikali mbili, bali serikali moja, nchi moja!.
  14. Masharti ya Katiba yaliyowekwa kwenye Katiba ya Zanzibar kuhusu Mchango wa Zanzibar katika mambo ya Muungano yamepingana na masharti ya Muungano, hili linaweza kumalizwa kwa serikali 3, kila nchi kuchangia serikali ya muungano, na kiwekwe kipengele expressly kuwa kuchangia muungano ni lazima!, sio favour na hakuna options wala kugomea!.
  15. Muundo wa Muungano uliopo umepoteza kutambulisho Kihistoria Tanganyika kuhusu watu wa Tanganyika kupitia maslahi yao, hili dawa yake ni serikali tatu.
  16. Hili la Wananchi wa Tanzania Bara, kutokuwa na haki ya kumiliki Ardhi,wakati wenzano wa upande wa Zanzibar wanahaki ya kumiliki Ardhi Tanzania Bara linaweza kumalizwa kwa serikali moja ila its very unfortunately, mbia mmoja ni landless, wakati mwingine ana ample land!.
  17. Hili la Wabunge wa Zanzibar huchangia mijadala ya Muungano na ambayo kwa uhakika wake ni mambo ya Tanganyika na kwamba Wabunge wa Tanganyika hawana nafasi ya kuchangia katika Baraza la Wawakilishi.
  18. Kwa mujibu wa Sheria ya Mzanzibari ya mwaka 1985 Watanzania ambao ni Watanzania wa Bara kutakiwa kutimiza masharti Maalum ili kupata haki ya kiraia wakati Mzanzibari hutakiwi kupata haki hiyo bila masharti yeyote,haki hiyo ni pamoja na kugombea Uongozi, litamalizwa kwa serikali 3!.
  19. Kitendo cha selfishness Zanzibar kuendelea kuushikilia utaifa wake, wakati Tanganyika tuliupoteza, kutamalizwa kwa serikali moja, hivyo kuwakata kabisa vilimilimi, ghubu na makelele kibao kuhusu muungano.
  20. Sambamba na hizi kero kubwa kubwa, kuna vikero vingine vidogo vidogo, vyote vitamalizika kwa nchi moja, serikali mmoja, rais mmoja!.
​Pasco

 
Hata mie nakuunga mkono. Kama kweli tunataka muungano uimarike basi tuwe na serikali moja. La sivyo muungano wetu ni mchezo wa kuigiza na unafiki, ubinafsi na uroho wa madaraka unaotusumbua hapa.

Uliona wapi vitu viwili vinaungana na kutokeza vitu viwili au vitatu? Toka vitu viwili kuwa vitatu sio muungano, ni mpasuko.

Kwanza serikali moja maana yake ni compromise; wale wanaotaka serikali tatu na wale wanaotaka serikali mbili wote wamekosa ili kuzuia kutoelewana na makundi.
 
jk alichokifanya jana ni kuwatisha wanzanzibar kwa kuwatishia nyau kuwa ikija serikali ya Tanganyika basi wategemee mabadiliko kuhusu wao na maisha yao huku Tanganyika hivi kama Rais huwezi kutumia busara kushawishi hadi uwatishe wanzibar wana ardhi na majumba marekani inakuwaje Tanganyika hilo tatizo?

swali kwako PASCO kwanini JK anaonekana kutokujali mabadiliko ya katiba ya zanzibar ya mwaka 2010 hasa ukizingatia yalivunja katiba ya Tanzania ??
 
jk alichokifanya jana ni kuwatisha wanzanzibar kwa kuwatishia nyau kuwa ikija serikali ya Tanganyika basi wategemee mabadiliko kuhusu wao na maisha yao huku Tanganyika hivi kama Rais huwezi kutumia busara kushawishi hadi uwatishe wanzibar wana ardhi na majumba marekani inakuwaje Tanganyika hilo tatizo?

swali kwako PASCO kwanini JK anaonekana kutokujali mabadiliko ya katiba ya zanzibar ya mwaka 2010 hasa ukizingatia yalivunja katiba ya Tanzania ??
Politiki, sio tuu JK hata Warioba, wote wanaiogopa Zanzibar kama ukoma!.Warioba alipaswa atoe hizi options 2, au serikali moja au serikali tatu!, kwa vile wanaigopa Zanzibar, sijawahi sikia hoja ya serikali moja ikizungumzwa!.

Yale mabadiliko ya katiba ya Zanzibar ya 2010, ule ni uhaini wa wazi kabisa!, ingebidi Karume akaozee jela!, ila kwa vile ule ni uamuzi wa Wazanzibari kwa ujumla wao, huku bara wote wanawagwaya!. Haku kuigwaya gwaya Zanzibar, ndiko kunakozidi kuwavimbisha mabichwa na kuendelea kujiona wao ndio wao, huku wakitubeza kutwa kucha!.

Wazanzibari wote wanataka serikali 3!, Watanganyika wengi we don't give a dam kuhusu Zanzibar, after all liabilities tupu!, hivyo sass Watanganyika tumechoka kuibeba Zanzibar, lijitu linabebwa halibebeki!, mikelele njia nzima!, tumefikia point, sasa kila aubebe mzigo wake mwenyewe!, hili linawezekana kwa serikali tatu!, kama hawawezi kujibeba, then tuwabebe jumla tujue moja!, serikali moja!.
Pasco
 
Hivi huwa ni sababu ipi inayowafanya viongozi wetu kutuburuza kila mara zinapoibuka hoja zinazohusu kero za muungano? Nimewahi kuuliza hili swali lakini acha niulize tena, hivi huu muungano ni kwa faida ya nani? Na kama viongozi wakiendelea kutuburuza katika suala hili ni nini hatima ya mungano kwa siku zijazo? Kwa sababu muungano wa serikali 2 ni sera ya CCM je ikitokea chama kingine kimeshinda uchaguzi katika upande wowote wa Tanzania (mfano CUF ikishinda Zanzibar) itakuwaje wakati kila chama kina mtazamo tofauti kuhusu muungano?
 
Mkuu Pasco naunga hoja mkono, lakini hawa jamaa zetu wazenj ni walalamishi sana, kwa tabia yao hii ya ulalamishi hata ukiunda serikali 1 au 2 au 3 au 4 au 10 au hata 20 hakika hawataacha kulalamika tu, we unaonaje kama tukigawana mbao ili kila mmoja akajenga kibanda chake anachoona kinamfaa, mi naona hili ndilo suruhisho la muungano.
 
Last edited by a moderator:
Serikali moja ndio muundo sahihi wa Muungano, serikali mbili au tatu ni kufumbia macho matatizo ya msingi ya Muungano
Kama Zanzibar wanataka utaifa wao basi wapewe na muungano ufe maana hakuna mataifa mawili yote yapo sovereign na bado mnasema mna muungano. Labda waseme ujirani mwema nitawaelewa.
Zaidi ya yote Zanzibar walishavunja Katiba ya Jamhuri ya Muungano, nashangaa hakuna kiongozi yoyote "mtanga na nyika' anaegusia hili.
Ila na sisi wapuuzi sana kwenye mambo ya msingi, kanchi kale hata kiganjani hakajai eti kana uwakilishi sawa kwenye Tume na Bunge la katiba, hivi sisi tumelogwa au tunaumwa.
 
ndugu yangu umeandika pointi za msingi sana,suluhisho la malalamish yote ni serikali moja.hii itatupa nafasi ya kuungana katika kila jambo na kutokuweka mwanya wa kuibuka kwa maswali,nahisi muungano huu ni wa kiusalama zaidi kuliko tunavofikiri kuwa eti tunapendana ndio tumeungana.dhana ya kuungana ipo wazi ni kuwa kitu kimoja katika kila jambo,tunaposema tumeungana kwa baadhi ya mambo huo si muungano udumuo.
 
Mi naunga mkono hoja ya wahed, serikal moja ilikuwa inafaa zaidi lakini kwa upepo ulivyo kwa wazanzibari ni ngumu sana kuchangama na tanganyika completely kutengeneza nchi moja, watataka tu kujitenga na kutaka kanchi kao katambulike, kwa mfumo uliopo sasa hvi wa serikal mbili ambao zanzibar wamevunja katba na kujitangaza nchi tumepata nchi mbili na serikal mbili badala ya nchi moja na serikal mbil kama ilivyokuwa awali, na ukitaka kujua hii hoja ni chungu sana kwa wanaoshabikia serikal mbili, hakuna hata mmoja aliyetolea ufafanuzi hili suala hadi humu katika mitandao, kila mtu analikwepa, hawawezi kueleza iweje zanzbar ilijitangaza kuwa nchi ndani ya muungano? Kwa nini katiba ilivunjwa na watawala walioapa kuilinda hawajawajibika? OKay tukiwa na serikali mbili wakati zanzibar ikiwa ni nchi inamaanisha itafika wakati nao wataomba kuwa wanachama UN, na je Zanzibar itakuwa mwanachama mara mbili maana Tanzania tayari mwanachama wa UN, ambayo ndan yake Zanzibar ipo. Muungano hauna faida tusome alama za nyakati, kila mmoja abaki na chake kwani hilo la nchi moja serikal moja ndio wazo zuri lakini halitekelezeki kwani zanzibar wanaitaka zanzibari yao kama nchi.
 
ndugu yangu umeandika pointi za msingi sana,suluhisho la malalamish yote ni serikali moja.hii itatupa nafasi ya kuungana katika kila jambo na kutokuweka mwanya wa kuibuka kwa maswali,nahisi muungano huu ni wa kiusalama zaidi kuliko tunavofikiri kuwa eti tunapendana ndio tumeungana.dhana ya kuungana ipo wazi ni kuwa kitu kimoja katika kila jambo,tunaposema tumeungana kwa baadhi ya mambo huo si muungano udumuo.

Hili wazo ni zuli lakini kwa hali iliyopo sasa ni ngumu sana kutekelezeka kwan wazanzibar wanaitaka nchi yao itambulike kama nchi, na ndio maana hii opition ya serikali moja haipati nguvu ingawa wachache walijaribu kuitaja, tatzo la watawala wa tanganyika wanawaogopa wazanzbari, eti mafuta na gesi sio vya muungano vip kuhusu gesi ya mtwara na wao haiwahusu? Au ndio changu changu, chako cha wote.
 
Muungano ufe; nitapoteza historia tu lakini sitapoteza usingizi wowote kwa vile nafasi zinashikiliwa na wazenj hapa Tanganyika nitajipatia moja.

Kikwete siyo referee mzuri katika mechi hii ya Katiba mpya kwa sababu anaogopa wazenji, kwa hiyo njia pekee iliyobaki ni kumaliza muungano huo ili kila sehemu iangalie nafasi yake. Wilaya mbili tu za Sikonge na Urambo katika mkoa wangu zinaizidi sana Zanzibar na Pemba kwa pamoja, iweje watuyumbishe namna hiyo?

Mikopo na misaada ya nje hutolewa kwa miradi fulani, mkopo ulitolewa kwa mradi wa kusaidia kilimo cha tumbaku Tabora hauwezi kulalamikiwa na watu wa Kagera kwa vile wao hawalimi tumbaku; vile vile mradi wa kujenga bandari huko Bagamoyo kuunganisha nchi zisizokuwana na mpaka na bahari hauwezi kulalamikiwa na watu Mwanza kwa vile wao hawako katika bahari ya kuungansihwa na nchi hizo, Ni vivyo hivyo iwapo Zanzibar inataka mkopo unaohusu Zanzibar lakini mkopo huo ukaombwa na serikali ya jamhuri ya muungano kwa ajili ya mradi huo kusingekuwa na tatizo, lakini Zanzibar kuidharau serikali ya jamhuri yakmuungano na kutaka kila kitu wafanye wenyewe inatosha kabisa kuonyesha kuwa hawana haja na muungano huo; hivyo ni vizuri ufe kwa vile unakuwa ni mzigo zaidi kwa watanaganyika ku-accommodate matakwa ya wazanzibari wakati waoi hawatakui kuaccommodate yale ya watanganyika.
 
Wanabodi,

Huku mivutano kuhusu muundo wa muungano ukiendelea, nimefazifanyia tathmini ndogo kero za muungano kwa pande zote, nikajiridhisha pasi shaka, kuwa Jaji Warioba yuko very right!, muundo wa serikali mbili, licha ya kushindwa kumaliza kero za muungano kwa kipindi cha miaka 50 iliyopita!, hivyo nimejiridhisha kuwa muundo wa serikali mbili, kamwe, hauwezi kutatua kero hizo, hata zikipewa kipindi cha miaka 100 mingine!. Dawa ya kudumu ya kupunguza kero hizo, japo sio kuzimaliza kabisa ni serikali 3, ila suluhisho la kudumu, na dawa ya kutibu kwa kuzimaliza kabisa, kero za muungano, ni serikali moja! ambayo inaunda nchi moja chini ya rais mmoja!.

Naomba niwapitishe very briefly kwenye baadhi ya kero hizi.



  1. Kutokuwa na Uwazi wa Mapato na Matumizi wa Fedha za Jamhuri ya Muungano, kwa sababu serikali ya Muungano pia ndio serikali ya Tanganyika!, hakuna any dividing line zipi ni gharama za Tanganyika na zipi ni gharama za muungano!, serikali mbili haziwezi kutatua hili milele!. Dawa ni ama serikali tatu hivyo gharama za Tanganyika zitajulikana, and the same applies to mapato, kwa sasa Tanganyika pekee ndio tunagharimia muungano!, Its about time sasa kila mtu aubebe mzigo wake mwenyewe!.
  2. Kutokuwa na Akaunti ya Pamoja. Hili lilishindikana kwa sababu fedha za Tanganyika pia ndizo pekee zimekuwa zikigharimia muungano!, uwe na account ya pamoja ya nini wakati Zanzibar haitoi single cent?. Serikali tatu ndio suluhisho la tatizo hili account itafunguliwa Serikali ya Tanganyika itatiamo fedha na Zanzibar italazimika, huu ndio utakuwa mwisho wa dezo dezo!.
  3. Uwepo wa Mkanganyiko wa Mapato jinsi ya kuchangia gharama uendeshaji wa Serikali zote mbili utamalizwa kwa kuinyofoa serikali ya Tanganyika ndani ya serikali ya muungano!.
  4. Kuwepo kwa Tume mbili zinazoshindana katika Nchi moja pia kutaondolewa kama kila mtu atakuwa kivyake vyake!.
  5. Zanzibar kutoshirikishwa kikamilifu na Serikali ya Jamhuri ya Muungano katika mchakato wa kupata misaada kutoka kwa Nchi za nje nako pia kutamalizikia kwa sababu misaada sio jambo la muungano, kwa sasa tunawapa Zanzibar asilimia 4.5 ya misaada yote ya Tanzania!. Kila mtu atajitafutia, na huu ndio utakuwa mwisho wa watu kujivunia wasichokipanda, kujipakulia wasichokipika, na kujilia vya watu!.
  6. Malalamiko kuwa Viongozi Wakuu wa Zanzibar wanachaguliwa Dodoma na sio Zanzibar nako pia kutaisha, mambo yote ya Zanzibar sasa yatakuwa yao wenyewe!.
  7. Zanzibar kulalamika kuwa kuna baadi ya mambo yamefanywa kuwa ya Muungano kupitia kutungwa kwa Sheria ya Bunge la Jamhuri ya Muungano na baada ya hapo mambo hayo huwa katika utatanishi, hili nalo litakwisha.
  8. Kitendo cha Zanzibar kuwa nchi huru, inabendera yake, ina wimbo wa Taifa, Serikali yake na imebadili Katiba yake kutambuliwa kama Nchi kutamalizwa kwa serikali moja!, serikali mbili au tatu, haziwezi kutatua hili, huwezi kuwa na muungano wa nchi mbili halafu bado zikabaki nchi mbili!.
  9. Kitendo cha Zanzibar kubadili masharti ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano ambayo inasema Sheria za Muungano zinazotungwa na Bunge hilo,zitumike sehemu zote, badala yake Katiba ya Zanzibar inaelekeza kuwa ili Sheria
  10. itumike Zanzibar Sharti ipelekwe kwenye Baraza la Muungano ni lazima kikemewe na kuadabishwa!. Katiba ya JMT ndio supreme!. Hili pia haliwezi kumalizwa na serikali mbili wala tatu, bali dawa ya hili ni serikali moja!.
  11. Hili la Zanzibar kutunga Sheria kuhusu Fedha, ambalo ni suala lililopo kwenye Katiba ya Muungano pia litamalizwa na serikali moja!.
  12. Hili la Zanzibar kutunga Katiba ambayo imechukua Madaraka ya Rais yaliyopo kwenye Jamhuri ya Muungano,inaeleza kwamba Rais wa Jamhuri ya Muungano anamadaraka ya kugawa Nchi katika maeneo ya Kiutawala, mabadiliko ya kumi ya Katiba ya Zanzibar ya 1984 yametambua kuwa Zanzibar ni Nchi na yamempatia Rais wa Zanzibar mamlaka ya Kuigawa Nchi katika meneo ya Muungano litamalizwa kwa serikali tatu!.
  13. Hili la Katiba ya Zanzibar inaeleza Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Nchi mbili lakini Katiba ya Jamhuri inaeleza kuwa Tanzania ni Nchi moja haliwezi kumalizwa kwa serikali mbili, bali serikali moja, nchi moja!.
  14. Masharti ya Katiba yaliyowekwa kwenye Katiba ya Zanzibar kuhusu Mchango wa Zanzibar katika mambo ya Muungano yamepingana na masharti ya Muungano, hili linaweza kumalizwa kwa serikali 3, kila nchi kuchangia serikali ya muungano, na kiwekwe kipengele expressly kuwa kuchangia muungano ni lazima!, sio favour na hakuna options wala kugomea!.
  15. Muundo wa Muungano uliopo umepoteza kutambulisho Kihistoria Tanganyika kuhusu watu wa Tanganyika kupitia maslahi yao, hili dawa yake ni serikali tatu.
  16. Hili la Wananchi wa Tanzania Bara, kutokuwa na haki ya kumiliki Ardhi,wakati wenzano wa upande wa Zanzibar wanahaki ya kumiliki Ardhi Tanzania Bara linaweza kumalizwa kwa serikali moja ila its very unfortunately, mbia mmoja ni landless, wakati mwingine ana ample land!.
  17. Hili la Wabunge wa Zanzibar huchangia mijadala ya Muungano na ambayo kwa uhakika wake ni mambo ya Tanganyika na kwamba Wabunge wa Tanganyika hawana nafasi ya kuchangia katika Baraza la Wawakilishi.
  18. Kwa mujibu wa Sheria ya Mzanzibari ya mwaka 1985 Watanzania ambao ni Watanzania wa Bara kutakiwa kutimiza masharti Maalum ili kupata haki ya kiraia wakati Mzanzibari hutakiwi kupata haki hiyo bila masharti yeyote,haki hiyo ni pamoja na kugombea Uongozi, litamalizwa kwa serikali 3!.
  19. Kitendo cha selfishness Zanzibar kuendelea kuushikilia utaifa wake, wakati Tanganyika tuliupoteza, kutamalizwa kwa serikali moja, hivyo kuwakata kabisa vilimilimi, ghubu na makelele kibao kuhusu muungano.
  20. Sambamba na hizi kero kubwa kubwa, kuna vikero vingine vidogo vidogo, vyote vitamalizika kwa nchi moja, serikali mmoja, rais mmoja!.
Pasco
Wanabodi,
Leo sikukuu ya Muungano, nafanya mapitio ya baadhi ya mabandiko ya muungano.

Japo waasisi wa muungano wetu huu adhimu ni Nyerere na Karume, muungano ni kama ndoa, kuna mtu ana proposes, mwingine anakubali, ndoa inafungwa. Kwenye muungano wetu huu adhimu, aliye proposes ni Nyerere, Karume akakubali. Nia ya Nyerere ni kwenda kwenye serikali moja. Wito kwa viongozi wetu, kama nia ya kweli ni kudumisha muungano, twende kwenye serikali moja. Tumuenzi Mwalimu Nyerere kwa kuyaishi maono yake!. Nawatakia Muungano Mwema.

Paskali
 
Wanabodi,

Huku mivutano kuhusu muundo wa muungano ukiendelea, nimefazifanyia tathmini ndogo kero za muungano kwa pande zote, nikajiridhisha pasi shaka, kuwa Jaji Warioba yuko very right!, muundo wa serikali mbili, licha ya kushindwa kumaliza kero za muungano kwa kipindi cha miaka 50 iliyopita!, hivyo nimejiridhisha kuwa muundo wa serikali mbili, kamwe, hauwezi kutatua kero hizo, hata zikipewa kipindi cha miaka 100 mingine!. Dawa ya kudumu ya kupunguza kero hizo, japo sio kuzimaliza kabisa ni serikali 3, ila suluhisho la kudumu, na dawa ya kutibu kwa kuzimaliza kabisa, kero za muungano, ni serikali moja! ambayo inaunda nchi moja chini ya rais mmoja!.

Naomba niwapitishe very briefly kwenye baadhi ya kero hizi.



  1. Kutokuwa na Uwazi wa Mapato na Matumizi wa Fedha za Jamhuri ya Muungano, kwa sababu serikali ya Muungano pia ndio serikali ya Tanganyika!, hakuna any dividing line zipi ni gharama za Tanganyika na zipi ni gharama za muungano!, serikali mbili haziwezi kutatua hili milele!. Dawa ni ama serikali tatu hivyo gharama za Tanganyika zitajulikana, and the same applies to mapato, kwa sasa Tanganyika pekee ndio tunagharimia muungano!, Its about time sasa kila mtu aubebe mzigo wake mwenyewe!.
  2. Kutokuwa na Akaunti ya Pamoja. Hili lilishindikana kwa sababu fedha za Tanganyika pia ndizo pekee zimekuwa zikigharimia muungano!, uwe na account ya pamoja ya nini wakati Zanzibar haitoi single cent?. Serikali tatu ndio suluhisho la tatizo hili account itafunguliwa Serikali ya Tanganyika itatiamo fedha na Zanzibar italazimika, huu ndio utakuwa mwisho wa dezo dezo!.
  3. Uwepo wa Mkanganyiko wa Mapato jinsi ya kuchangia gharama uendeshaji wa Serikali zote mbili utamalizwa kwa kuinyofoa serikali ya Tanganyika ndani ya serikali ya muungano!.
  4. Kuwepo kwa Tume mbili zinazoshindana katika Nchi moja pia kutaondolewa kama kila mtu atakuwa kivyake vyake!.
  5. Zanzibar kutoshirikishwa kikamilifu na Serikali ya Jamhuri ya Muungano katika mchakato wa kupata misaada kutoka kwa Nchi za nje nako pia kutamalizikia kwa sababu misaada sio jambo la muungano, kwa sasa tunawapa Zanzibar asilimia 4.5 ya misaada yote ya Tanzania!. Kila mtu atajitafutia, na huu ndio utakuwa mwisho wa watu kujivunia wasichokipanda, kujipakulia wasichokipika, na kujilia vya watu!.
  6. Malalamiko kuwa Viongozi Wakuu wa Zanzibar wanachaguliwa Dodoma na sio Zanzibar nako pia kutaisha, mambo yote ya Zanzibar sasa yatakuwa yao wenyewe!.
  7. Zanzibar kulalamika kuwa kuna baadi ya mambo yamefanywa kuwa ya Muungano kupitia kutungwa kwa Sheria ya Bunge la Jamhuri ya Muungano na baada ya hapo mambo hayo huwa katika utatanishi, hili nalo litakwisha.
  8. Kitendo cha Zanzibar kuwa nchi huru, inabendera yake, ina wimbo wa Taifa, Serikali yake na imebadili Katiba yake kutambuliwa kama Nchi kutamalizwa kwa serikali moja!, serikali mbili au tatu, haziwezi kutatua hili, huwezi kuwa na muungano wa nchi mbili halafu bado zikabaki nchi mbili!.
  9. Kitendo cha Zanzibar kubadili masharti ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano ambayo inasema Sheria za Muungano zinazotungwa na Bunge hilo,zitumike sehemu zote, badala yake Katiba ya Zanzibar inaelekeza kuwa ili Sheria
  10. itumike Zanzibar Sharti ipelekwe kwenye Baraza la Muungano ni lazima kikemewe na kuadabishwa!. Katiba ya JMT ndio supreme!. Hili pia haliwezi kumalizwa na serikali mbili wala tatu, bali dawa ya hili ni serikali moja!.
  11. Hili la Zanzibar kutunga Sheria kuhusu Fedha, ambalo ni suala lililopo kwenye Katiba ya Muungano pia litamalizwa na serikali moja!.
  12. Hili la Zanzibar kutunga Katiba ambayo imechukua Madaraka ya Rais yaliyopo kwenye Jamhuri ya Muungano,inaeleza kwamba Rais wa Jamhuri ya Muungano anamadaraka ya kugawa Nchi katika maeneo ya Kiutawala, mabadiliko ya kumi ya Katiba ya Zanzibar ya 1984 yametambua kuwa Zanzibar ni Nchi na yamempatia Rais wa Zanzibar mamlaka ya Kuigawa Nchi katika meneo ya Muungano litamalizwa kwa serikali tatu!.
  13. Hili la Katiba ya Zanzibar inaeleza Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Nchi mbili lakini Katiba ya Jamhuri inaeleza kuwa Tanzania ni Nchi moja haliwezi kumalizwa kwa serikali mbili, bali serikali moja, nchi moja!.
  14. Masharti ya Katiba yaliyowekwa kwenye Katiba ya Zanzibar kuhusu Mchango wa Zanzibar katika mambo ya Muungano yamepingana na masharti ya Muungano, hili linaweza kumalizwa kwa serikali 3, kila nchi kuchangia serikali ya muungano, na kiwekwe kipengele expressly kuwa kuchangia muungano ni lazima!, sio favour na hakuna options wala kugomea!.
  15. Muundo wa Muungano uliopo umepoteza kutambulisho Kihistoria Tanganyika kuhusu watu wa Tanganyika kupitia maslahi yao, hili dawa yake ni serikali tatu.
  16. Hili la Wananchi wa Tanzania Bara, kutokuwa na haki ya kumiliki Ardhi,wakati wenzano wa upande wa Zanzibar wanahaki ya kumiliki Ardhi Tanzania Bara linaweza kumalizwa kwa serikali moja ila its very unfortunately, mbia mmoja ni landless, wakati mwingine ana ample land!.
  17. Hili la Wabunge wa Zanzibar huchangia mijadala ya Muungano na ambayo kwa uhakika wake ni mambo ya Tanganyika na kwamba Wabunge wa Tanganyika hawana nafasi ya kuchangia katika Baraza la Wawakilishi.
  18. Kwa mujibu wa Sheria ya Mzanzibari ya mwaka 1985 Watanzania ambao ni Watanzania wa Bara kutakiwa kutimiza masharti Maalum ili kupata haki ya kiraia wakati Mzanzibari hutakiwi kupata haki hiyo bila masharti yeyote,haki hiyo ni pamoja na kugombea Uongozi, litamalizwa kwa serikali 3!.
  19. Kitendo cha selfishness Zanzibar kuendelea kuushikilia utaifa wake, wakati Tanganyika tuliupoteza, kutamalizwa kwa serikali moja, hivyo kuwakata kabisa vilimilimi, ghubu na makelele kibao kuhusu muungano.
  20. Sambamba na hizi kero kubwa kubwa, kuna vikero vingine vidogo vidogo, vyote vitamalizika kwa nchi moja, serikali mmoja, rais mmoja!.
​Pasco
Kwanza nakiri kuwa sikusoma bango lote ILA nimekwenda straight kwenye kichwa cha mada, nami nasema hivi, uzoefu umeonyesha kuwa Serikali mbili zinaweza kutatua kero za Muungano. Utauliza uzoefu UPI? Ni kuwa kwa kipindi hiki kifupi cha Rais Samia Suluhu Hassani, Seriklai yake (ya SMT) na ile ya Rais Dr.Hussein Mwinyi (ya SMZ) zimetatua kero nyingi za Muungano; huo ndio uzoefu ninao sema na kuzungumzia. Utaona zimeundwa au hata kuimarishwa na wakati mwingine kutolewa maagizo maalum na mahsusi kwa viongozi wa juu - kama VP wa SMT au Waziri wa Fedha na wengine washughulikie kero za Muungano. Kwa mantiki hiyo na kwa ushahidi huo, binafsi naamini Serikali Mbili (na hasa hasa kama zote zinaongozwa na Wazanzibari) zinaweza kutatua kero za Muungano. Nawasilisha.
 
Wanabodi,

Huku mivutano kuhusu muundo wa muungano ukiendelea, nimefazifanyia tathmini ndogo kero za muungano kwa pande zote, nikajiridhisha pasi shaka, kuwa Jaji Warioba yuko very right!, muundo wa serikali mbili, licha ya kushindwa kumaliza kero za muungano kwa kipindi cha miaka 50 iliyopita!, hivyo nimejiridhisha kuwa muundo wa serikali mbili, kamwe, hauwezi kutatua kero hizo, hata zikipewa kipindi cha miaka 100 mingine!. Dawa ya kudumu ya kupunguza kero hizo, japo sio kuzimaliza kabisa ni serikali 3, ila suluhisho la kudumu, na dawa ya kutibu kwa kuzimaliza kabisa, kero za muungano, ni serikali moja! ambayo inaunda nchi moja chini ya rais mmoja!.

Pasco
paschal changamoto ni kwamba hata weye ni mmoja wa wengi ambao hamjishughulishi kudai katiba mpya.Unawategea CDM tu wakupambanie.Upo na CCM yako isiyotaka katiba mpya na unawatetea kila siku.Halafu unashangaa!
Mkuu Moisemusajiografii, kwa vile humu jf, kila uchao, wanaingia members wapya, hivyo kuna members hatufahamia tumeanzia wapi kupigania katiba mpya and what we stand for, sio vibaya tukasalimiana kwa kukumbushana na kukutakia mwaka mpya mwema!.
P
 
Mkuu Moisemusajiografii, kwa vile humu jf, kila uchao, wanaingia members wapya, hivyo kuna members hatufahamia tumeanzia wapi kupigania katiba mpya and what we stand for, sio vibaya tukasalimiana kwa kukumbushana na kukutakia mwaka mpya mwema!.
P
Sawa.Zamani ukikuwa unajidhihirisha wazi.Siku hizi yawezekana mimi(nasisitiza mimi)sijakuona wala kusikia unaidai katiba mpya wapi!Yawezekana ni kwenye vikao,makongamano,mikutano na warsha za wanasheria na wanahabari.Mimi sijakusikia wala kukuona.Onesha njia kwa kuwa mstari wa mbele mkuu.
 
Back
Top Bottom