Waziri Bashungwa ataka wafungwa kuanza kupewa mafunzo ya VETA pamoja na vyeti pindi wawapo gerezani

Waziri Bashungwa ataka wafungwa kuanza kupewa mafunzo ya VETA pamoja na vyeti pindi wawapo gerezani

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Wakuu,

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innnocent Bashungwa amelitaka Jeshi la Magereza kusimamia kikamilifu mpango wa kuwapa ujuzi na mafunzo ya ufundi stadi Wafungwa wanapokuwa Gerezani na watakaohitimu mafunzo kutunukiwa vyeti vinavyotambuliwa na VETA wakati wanapomaliza vifungo vyao ili kuwajengea uwezo kujitegemea wanaporudi katika jamii.

Bashungwa ameeleza hayo tarehe 14 Februari 2025 wakati alipofanya ziara ya kikazi Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, Dodoma ambapo amebainisha kuwa Jeshi hilo kwa kushirikiana na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi stadi (VETA) litaanza utekelezaji wa mpango wa kuwapa mafunzo Wafungwa wanapokuwa Gerezani.

Bashungwa ameeleza kuwa mpango huo ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa Jeshi la Magereza wa kuwapo ujuzi wa ufundi stadi Wafungwa wanapokuwa wanatumikia vifungo yao pamoja kurasimisha ujuzi wanakuwa nao na kuwapatia vyeti.

“Mheshimiwa Rais alitoa maelekezo kwa Kamishna Jenerali wa Magereza, kuwapa ujuzi (ufundi stadi) kwa kuwaendeleza wanaoingia gerezani na ujuzi, lakini wale wanaoingia hawana ujuzi kabisa, kuangalia namna ya kuwapa ujuzi ili wanapotokaa waweze kujikimu kimaisha,” ameeleza Bashungwa.

bash.png
 
Wakuu,

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innnocent Bashungwa amelitaka Jeshi la Magereza kusimamia kikamilifu mpango wa kuwapa ujuzi na mafunzo ya ufundi stadi Wafungwa wanapokuwa Gerezani na watakaohitimu mafunzo kutunukiwa vyeti vinavyotambuliwa na VETA wakati wanapomaliza vifungo vyao ili kuwajengea uwezo kujitegemea wanaporudi katika jamii.

Bashungwa ameeleza hayo tarehe 14 Februari 2025 wakati alipofanya ziara ya kikazi Makao Makuu ya Jeshi la Magereza, Dodoma ambapo amebainisha kuwa Jeshi hilo kwa kushirikiana na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi stadi (VETA) litaanza utekelezaji wa mpango wa kuwapa mafunzo Wafungwa wanapokuwa Gerezani.

Bashungwa ameeleza kuwa mpango huo ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa Jeshi la Magereza wa kuwapo ujuzi wa ufundi stadi Wafungwa wanapokuwa wanatumikia vifungo yao pamoja kurasimisha ujuzi wanakuwa nao na kuwapatia vyeti.

“Mheshimiwa Rais alitoa maelekezo kwa Kamishna Jenerali wa Magereza, kuwapa ujuzi (ufundi stadi) kwa kuwaendeleza wanaoingia gerezani na ujuzi, lakini wale wanaoingia hawana ujuzi kabisa, kuangalia namna ya kuwapa ujuzi ili wanapotokaa waweze kujikimu kimaisha,” ameeleza Bashungwa.

Hii nimeona sweden wako vizuri sana katika hili. Sema kule ni zaidi ya kuwa huru bongo. mfungwa anaenda shule mwenyewe kala suti anajifunza anarudi domitory ana kila kitu. Wale jamaa yani wanaweza kukufanya utamani ukawe mfungwa kule.
 
Kabla ya yote hayo wafungwa wapewe haki za kukutana na wake / wapenzi wao, angalau mara moja kwa wiki 2

Mtu yupo jela mwaka mzima hajawahi kukutana na mwenzake, akili haiwezi kukaa sawa kuwaza mtu anayempenda sio wa kwake tena, hawawezi kupata mtoto, n.k.
 
Na support hili,,, states watu wana graduate kabisa hata medicine bora wa some waje kujenga nchi kuliko mtu kukaa bure tu akitoka anataman arud tena kwakukosa mishe za kufanya
 
Hili nimeliona El Salvador kwa bwana Nayib Bukele .Wale wahalifu wa magenge lazima ujue kushona kwa kutumia charahani ,sasa ulete ukorofi wako uvunje sindano hata kwa bahati mbaya ,hiyo mikwaju utakayokula mpaka utasema ni nini hiki.Wewe ni nani mpaka ushindwe kukata kitambaa na kuandaa mashono?!
 
Serikali ya CCM ktk hili mechelewa Sanaa ,,ila km mmeamua awamu hii bac lisiishie mdomo mwa waziri Bali likaanze kazi mara Moja ...
 
Wafungwa wanaotumikia adhabu kwenye magereza mbalimbali nchini wanatarajiwa kuanza kupewa mafunzo ya umahiri kwenye ufundi stadi na kutunukiwa vyetu vya uhitimu kutoka Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi stadi (VETA).

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innnocent Bashungwa aliyeliagiza jeshi la magereza kuanza utekelezaji wa mpango huo kwa kushirikiana na VETA kama ilivyotolewa maagizo na Rais Samia Suluhu Hassan.

“Rais Samia alitoa maelekezo kwa Magereza kuwapa ujuzi zaidi wafungwa wanaoingia gerezani na ngazi fulani ya ujuzi na kuwapa mafunzo wasio na ujuzi wowotw kwa lengo la kuwa msingi wa kuanzia pindi wanapomaliza kutumikia adhabu zao.” ameeleza Bashungwa

Mbali ya maagizo hayo Bashungwa pia amekabidhi mabasi saba kwa Kamishna Jenerali wa Magereza (CGP), Jeremiah Katungu yatakayotumika kuwasafirisha mahabusu kuhudhuria mashauri mahakamani na kutekeleza shughuli nyingine za kimagereza.

Cc Azam tv
 
Wazo zuri na wote walazimishwe kusoma fani mbalimbali unatoka jela una PhD pia serikali itoe ruzuku wafungwa wasome bure au wapewe mikopo ya kusoma kozi mbalimbali
 
Wafungwa wanaotumikia adhabu kwenye magereza mbalimbali nchini wanatarajiwa kuanza kupewa mafunzo ya umahiri kwenye ufundi stadi na kutunukiwa vyetu vya uhitimu kutoka Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi stadi (VETA).

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innnocent Bashungwa aliyeliagiza jeshi la magereza kuanza utekelezaji wa mpango huo kwa kushirikiana na VETA kama ilivyotolewa maagizo na Rais Samia Suluhu Hassan.

“Rais Samia alitoa maelekezo kwa Magereza kuwapa ujuzi zaidi wafungwa wanaoingia gerezani na ngazi fulani ya ujuzi na kuwapa mafunzo wasio na ujuzi wowotw kwa lengo la kuwa msingi wa kuanzia pindi wanapomaliza kutumikia adhabu zao.” ameeleza Bashungwa

Mbali ya maagizo hayo Bashungwa pia amekabidhi mabasi saba kwa Kamishna Jenerali wa Magereza (CGP), Jeremiah Katungu yatakayotumika kuwasafirisha mahabusu kuhudhuria mashauri mahakamani na kutekeleza shughuli nyingine za kimagereza.

Cc Azam tv
Wafundishwe na udereva wa magari makubwa
 
Kwa ugumu huu wa maisha....
Bora niende jela tukapate ujuzi...😶
 
Kabla ya yote hayo wafungwa wapewe haki za kukutana na wake / wapenzi wao, angalau mara moja kwa wiki 2

Mtu yupo jela mwaka mzima hajawahi kukutana na mwenzake, akili haiwezi kukaa sawa kuwaza mtu anayempenda sio wa kwake tena, hawawezi kupata mtoto, n.k.
Hili jambo nimuhimu kilngozi. Sababu hata litaweza kupunguza kulawitiana huko.
 
Back
Top Bottom