MwanaHaki
R I P
- Oct 17, 2006
- 2,401
- 707
KWA TAKRIBAN miongo miwili sasa, serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kupitia kitengo cha Tanzania Investment Centre (TIC) pamoja na asasi nyingine, imekuwa ikiweka mkazo na jitihada kubwa za kuweka mazingira rafiki kwa wawekezaji, wawekezaji ambao ni raia wa nje, hususan watu weupe - wazungu!
TIC ilipoanzishwa ilijikosha kwa kusema kwamba inamkaribisha mwekezaji yeyote, awe wa ndani au nje. Lakini kadri siku zilivyosonga mbele dhamira yake halisi ilizidi kujitokeza; Wazungu tu!
Hivyo basi, kutokana na sera hii, Rais amekuwa akisafiri mara kwa mara nje ya nchi kwenye nchi mbalimbali zilizoendelea barani Ulaya na Marekani akifanya kazi ya Ubalozi wa Kiuchumi, kazi ambayo aliibuni akiwa Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, kiasi cha kuwashangaza wadau wa uchumi na diplomasia hapa nchini na kuhoji: Rais amesahau kwamba yeye ni Kiongozi wa Nchi?
Wadau wengine wamekwenda mbele zaidi na kusema kwamba Rais ameidhalilisha Taasisi ya Urais, kwani Rais ni Taasisi, si mtu binafsi.
"Rais anapashwa kukumbushwa kwamba alipaswa kuikabidhi sera ya Economic Diplomacy au kuunda taasisi ambayo ingefanya kazi hiyo chini ya ofisi yake, jambo ambalo lingemwezesha kujiepusha na tuhuma nzito wa matumizi mabaya ya ofisi yake, ikiwa ni pamoja na matumizi yasiyo ya msingi ya fedha nyingi ambazo mara nyingi huwa hazina maelezo na wala matumizi yake hayakaguliwi.
"Yote hayo ni tisa. Kumi ni pale rais anapoandamana na maswahiba wenzake akitumia chombo cha serikali, Ndege ya Rais, watu ambao hawajahakikiwa, hawajachunguzwa wala kuidhinishwa na Idara ya Usalama wa Taifa, Kitengo cha Usalama wa Rais.
"Unajua, ndege hii ilinunuliwa kwa mabilioni ya fedha na kilichomo ndani yake ni siri ya taifa. Sasa iwapo mmoja wa watu hao angekuwa gaidi au jasusi, angeweza kuuza siri za ndege hiyo, jambo ambalo lingeweza kuhatarisha usalama wa ndege hiyo na hata Rais mwenyewe. Sisi tunajiuliza anawaamini kiasi gani watu hao kiasi cha kuwapa nafasi kubwa namna hiyo?
"Kama mjuavyo, ndege hiyo ni ndogo, kwa hiyo unakuta watu wachache, 5 hadi 7 wanapanda ndege hiyo, waliobaki, 70 na ushee wanapanda ndege za mashirika ya nje, Business au First Class!
"Sisi hatuna chuki na Rais wetu. Tunampenda. Lakini tunajiuliza iwapo kasi hii ya kutafuta wawekezaji hawa wa nje imezaa au itazaa matunda," kilisema chanzo chetu.
----------------
Hii ni sehemu ya kwanza ya makala haya. Usikose kusoma sehemu ya pili na ya mwisho ya sehemu hii muda si mrefu ujao.
TIC ilipoanzishwa ilijikosha kwa kusema kwamba inamkaribisha mwekezaji yeyote, awe wa ndani au nje. Lakini kadri siku zilivyosonga mbele dhamira yake halisi ilizidi kujitokeza; Wazungu tu!
Hivyo basi, kutokana na sera hii, Rais amekuwa akisafiri mara kwa mara nje ya nchi kwenye nchi mbalimbali zilizoendelea barani Ulaya na Marekani akifanya kazi ya Ubalozi wa Kiuchumi, kazi ambayo aliibuni akiwa Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, kiasi cha kuwashangaza wadau wa uchumi na diplomasia hapa nchini na kuhoji: Rais amesahau kwamba yeye ni Kiongozi wa Nchi?
Wadau wengine wamekwenda mbele zaidi na kusema kwamba Rais ameidhalilisha Taasisi ya Urais, kwani Rais ni Taasisi, si mtu binafsi.
"Rais anapashwa kukumbushwa kwamba alipaswa kuikabidhi sera ya Economic Diplomacy au kuunda taasisi ambayo ingefanya kazi hiyo chini ya ofisi yake, jambo ambalo lingemwezesha kujiepusha na tuhuma nzito wa matumizi mabaya ya ofisi yake, ikiwa ni pamoja na matumizi yasiyo ya msingi ya fedha nyingi ambazo mara nyingi huwa hazina maelezo na wala matumizi yake hayakaguliwi.
"Yote hayo ni tisa. Kumi ni pale rais anapoandamana na maswahiba wenzake akitumia chombo cha serikali, Ndege ya Rais, watu ambao hawajahakikiwa, hawajachunguzwa wala kuidhinishwa na Idara ya Usalama wa Taifa, Kitengo cha Usalama wa Rais.
"Unajua, ndege hii ilinunuliwa kwa mabilioni ya fedha na kilichomo ndani yake ni siri ya taifa. Sasa iwapo mmoja wa watu hao angekuwa gaidi au jasusi, angeweza kuuza siri za ndege hiyo, jambo ambalo lingeweza kuhatarisha usalama wa ndege hiyo na hata Rais mwenyewe. Sisi tunajiuliza anawaamini kiasi gani watu hao kiasi cha kuwapa nafasi kubwa namna hiyo?
"Kama mjuavyo, ndege hiyo ni ndogo, kwa hiyo unakuta watu wachache, 5 hadi 7 wanapanda ndege hiyo, waliobaki, 70 na ushee wanapanda ndege za mashirika ya nje, Business au First Class!
"Sisi hatuna chuki na Rais wetu. Tunampenda. Lakini tunajiuliza iwapo kasi hii ya kutafuta wawekezaji hawa wa nje imezaa au itazaa matunda," kilisema chanzo chetu.
----------------
Hii ni sehemu ya kwanza ya makala haya. Usikose kusoma sehemu ya pili na ya mwisho ya sehemu hii muda si mrefu ujao.