Serikali ondoeni mamlaka ya Wakuu wa Mikoa na Wilaya juu ya Polisi, hayafai kabisa wakati huu

Serikali ondoeni mamlaka ya Wakuu wa Mikoa na Wilaya juu ya Polisi, hayafai kabisa wakati huu

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Mamlaka waliyo nayo wakuu wa mikoa, wilaya na Mawaziri kuamuru polisi kukamata watu au kuanzisha kesi hayapaswi kuwepo kabisa katika nchi inayoitwa ya kidemokrasia.

Huenda utaratibu huu ulifahaa wakati wa Nyerere kutokana na hali ya kisiasa na idadi ndogo ya watu wakati huo ila utaratibu huu haukapaswa kuendelea kuanzia utawala wa Mwinyi, wakati huu ndio haufai kabisa kwa sababu ya mabadiliko makubwa zaidi ya kisiasa na ongezeko la idadi ya watu.

Leo katika mfumo wa vyama vingi unapompa mkuu wa mkoa, wa wilaya au Waziri ambao ni makada wa chama tawala mamlaka ya kukamata watu utahakikisha vipi hawayatumii mamlaka hayo vibaya kisiasa?

Leo hii unapompa mkuu wa wilaya mamlaka hayo juu ya wilaya yenye watu zaidi ya milioni moja atayatumia vipi mamlaka hayo wakati hata watu wa mtaa wake tu walio wengi hawafahamiani?
 
Sio rahisi hayo kwa nchi hii ya CCM.

Unafahamu kiongozi wa CCM ana nguvu sana hapa taifani hata hao wakuu wa wilaya na mikoa wana subiri.

Nchi hii siasa ina nguvu kubwa kuliko elimu wala taaluma. Vyeo vya kisiasa vinatukuzwa sana hapa taifani kuliko chochote.

Mfano Samia hatukuzwi kwa sababu yeye ni Samia bali kiti anachokalia chamani na serikalini.

CCM wanapenda sana madaraka mamlaka hayo hawawezi yaondoa kwa sababu yana wasaidia katika harakati zao za siasa chafu.
 
Naunga mkono hoja. Ni kichekesho kuruhusu raia kuamuru Jeshi kutekeleza matakwa ya raia.
Odcourse duniani kuko hivyo, tofauti ya nchi zilizo endelea na za kwetu huwezi kuamka tu na kuamrisha vyombo vya usalama. Kuna sheria kali na procedure. Mfano US , mkuu wa deprtment ya DOJ, huyu anawajibika kwa rais only , wabunge sijui mawaziri hawawez kuamrisha vyombo hivyo bila yeye kufahmu. So inakuwa ni ngumu

Kwetu hapa hamna separation of power, na huu ndio mwanya wanao utumia
 
Mamlaka waliyo nayo wakuu wa mikoa, wilaya na Mawaziri kuamuru polisi kukamata watu au kuanzisha kesi hayapaswi kuwepo kabisa katika nchi inayoitwa ya kidemokrasia.

Huenda utaratibu huu ulifahaa wakati wa Nyerere kutokana na hali ya kisiasa na idadi ndogo ya watu wakati huo ila utaratibu huu haukapaswa kuendelea kuanzia utawala wa Mwinyi, wakati huu ndio haufai kabisa kwa sababu ya mabadiliko makubwa zaidi ya kisiasa na ongezeko la idadi ya watu.

Leo katika mfumo wa vyama vingi unapompa mkuu wa mkoa, wa wilaya au Waziri ambao ni makada wa chama tawala mamlaka ya kukamata watu utahakikisha vipi hawayatumii mamlaka hayo vibaya kisiasa?

Leo hii unapompa mkuu wa wilaya mamlaka hayo juu ya wilaya yenye watu zaidi ya milioni moja atayatumia vipi mamlaka hayo wakati hata watu wa mtaa wake tu walio wengi hawafahamiani?
Kwa vile watu nao wameanza Kufungua kesi pale wanapoona wamedhalilishwa au wameonewa, na kudai fidia nadhani itasaidia kwa wale ambao hawataki kujifunza kwa njia rahisi watakuwa wakijifunza kwa njia ngumu.
 
Katiba mpya ndio suluhisho! Sio tu mamlaka yao, hata uwepo wa cheo cha mkuu wa mkoa na mkuu wa wilaya hauna tija
 
Kama CCM wanaona mfumo huu ni Mali kwao,basi DC awe amri jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama kwenye wilaya yake, na Mkuu wa mkoa awe amri jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama kwenye mkoa wake.
 
Sio rahisi hayo kwa nchi hii ya CCM.

Unafahamu kiongozi wa CCM ana nguvu sana hapa taifani hata hao wakuu wa wilaya na mikoa wana subiri.

Nchi hii siasa ina nguvu kubwa kuliko elimu wala taaluma. Vyeo vya kisiasa vinatukuzwa sana hapa taifani kuliko chochote.

Mfano Samia hatukuzwi kwa sababu yeye ni Samia bali kiti anachokalia chamani na serikalini.

CCM wanapenda sana madaraka mamlaka hayo hawawezi yaondoa kwa sababu yana wasaidia katika harakati zao za siasa chafu.
Very well said mkuu.🙌🏾
 
Odcourse duniani kuko hivyo, tofauti ya nchi zilizo endelea na za kwetu huwezi kuamka tu na kuamrisha vyombo vya usalama. Kuna sheria kali na procedure. Mfano US , mkuu wa deprtment ya DOJ, huyu anawajibika kwa rais only , wabunge sijui mawaziri hawawez kuamrisha vyombo hivyo bila yeye kufahmu. So inakuwa ni ngumu

Kwetu hapa hamna separation of power, na huu ndio mwanya wanao utumia
Ni kweli, Attorney General wa Marekani ambaye ndiye mkuu Department of Justice hawezi kumuamuru mkuu wa FBI au afisa mwingine yeyote wa FBI kumkamata mtu fulani. FBI wako huru kuamua wamchunguze na wamkamate nani na kwa wakati gani.
 
Mamlaka waliyo nayo wakuu wa mikoa, wilaya na Mawaziri kuamuru polisi kukamata watu au kuanzisha kesi hayapaswi kuwepo kabisa katika nchi inayoitwa ya kidemokrasia.

Huenda utaratibu huu ulifahaa wakati wa Nyerere kutokana na hali ya kisiasa na idadi ndogo ya watu wakati huo ila utaratibu huu haukapaswa kuendelea kuanzia utawala wa Mwinyi, wakati huu ndio haufai kabisa kwa sababu ya mabadiliko makubwa zaidi ya kisiasa na ongezeko la idadi ya watu.

Leo katika mfumo wa vyama vingi unapompa mkuu wa mkoa, wa wilaya au Waziri ambao ni makada wa chama tawala mamlaka ya kukamata watu utahakikisha vipi hawayatumii mamlaka hayo vibaya kisiasa?

Leo hii unapompa mkuu wa wilaya mamlaka hayo juu ya wilaya yenye watu zaidi ya milioni moja atayatumia vipi mamlaka hayo wakati hata watu wa mtaa wake tu walio wengi hawafahamiani?
Unataka kui suffocate CCM? Au unataka iishi vipi? CCM ilishajifia kitambo sana, vyombo vya ulinzi na usakama ndiyo oxygen machine inayoifanya muine kuwa ipo hai hapo kitandani.
Hata kama Tume ya uchaguzu ingekuwa inaundwa ndani ya vikao vya CCM, lakini isingekuwa backup ya vyombo vya ulinzi na usalama CCM ingekuwa imeshaootea kitambo.
Tuna mijitu mishamba na mipumbavu sana kwenye vyombo vya ulinzi na usakama (ondoa JWTZ, ingawa kuna baadhi siku hizi ni kama hawajitambui hasa huko mawilayani) mijitu hiyo haijui kabisa wajubu wai, na yenyewe imekaririshwa na CCM kwamba bila CCM imara nchi itasambaratika na yenyewe inaongea hivyo, yaani haijui kwamba hilo ni jukumu lao siyo CCM.
Vyombo vya ulinzi na Usalama mbele ya CCM vinajiona nafasi zao ni sawa na wale walinzi comedians wa getini kwenye bongo movies mbele ya bosi wao, hawana say
 
Kwa vile watu nao wameanza Kufungua kesi pale wanapoona wamedhalilishwa au wameonewa, na kudai fidia nadhani itasaidia kwa wale ambao hawataki kujifunza kwa njia rahisi watakuwa wakijifunza kwa njia ngumu.
Bado mkuu wa mkoa anaye jiona anaweza kuajiri wakati wowote na anaweza kufuta kazi mtu yeyote wakati wowote ili mradi kajisikia tu kwa mihemko yake
 
Ni kweli, Attorney General wa Marekani ambaye ndiye mkuu Department of Justice hawezi kumuamuru mkuu wa FBI au afisa mwingine yeyote wa FBI kumkamata mtu fulani. FBI wako huru kuamua wamchunguze na wamkamate nani na kwa wakati gani.
Unaona mifumo ya wenzetu ilivyo jipanga. Separation of power si rahis kutumika na viongozi chini ya rais.
hapa kwetu we need that, else misconducts na abuse of power haitoisha
 
Bado mkuu wa mkoa anaye jiona anaweza kuajiri wakati wowote na anaweza kufuta kazi mtu yeyote wakati wowote ili mradi kajisikia tu kwa mihemko yake
Naye aendelee kufanya tu ubabe atapatikana akiingia kwenye 50 za watu wanaojua haki zao na wanaweza kuzidai.
 
Back
Top Bottom