Serikali oneni aibu sana kwa hili la wanafunzi wa vyuo!!!!!!!!

Serikali oneni aibu sana kwa hili la wanafunzi wa vyuo!!!!!!!!

BIG X

JF-Expert Member
Joined
Nov 4, 2011
Posts
777
Reaction score
212
Sidhani hawa viongozi wetu wana watoto kwenye hivi vyuo, Yani wapo tayari kununua maelfu ya mabomu kuliko kuwapatia mahitaji hawa wanafunzi wa vyuo. Labda viongozi wetu hawana watoto, sababu hawajui uchungu wa watoto. Kuna maana gani ya kuwa na viongozi wazee kwenye serikali yetu halafu serikali inakosa busara kama uzee ni busara.

Ukiangalia hizo picha hapo hao wanafunzi wamekaa wakijadili matatizo yao ambayo yanawaumiza na wayapeleke panapohusika. Mnapowawekea Askari na vifaa vya hatari nyuma manake ni nini, ni kuwatisha!!. Kama ni kuwatisha basi serikali ijue inakosea sana badala yake mnawajenga ujasiri hawa wanafunzi bila nyie kujua. Baada ya miaka mingi 20-30 taifa litakuwa na watu wenye hasira ambao hawataliheshimu Jeshi la polisi hata kidogo, mnajenga nchi ya watu wenye visasi wakati huo nyinyi viongozi hamtakuwepo, mtakua mmetuachia balaa watanzania. Ndio mnataka tuwakumbuke kwa hayo!!!.

Ni wazazi gani nyie mnaoshindwa kuongea na vijana wenu, mkawasaidia na kuwatatulia shida zao. Mnafikiri mtaiweza nchi kwa kufanya vitisho!!!.

Kama mnawatisha sana wanafunzi miaka nenda rudi na hakuna anayetishika, mambo yanajirudia vilevile. mmeshindwa kuelewa mnatengeneza nchi ya namna gani.

Ni watoto wa masikini ndio wanateseka hivi!!!!.

Mjue tu kila jambo huwa lina mwisho wake.


DSC06409.JPGimages23.jpgimages24.jpgimages25.jpg
 
Hao watoto wakasome wanachochewa na wanasiasa uchwara kwa vichipsi kuku. Wanasiasa hao wanajulikana, lakini wahindi wanasema "deka jaega".
 
Hao watoto wakasome wanachochewa na wanasiasa uchwara kwa vichipsi kuku. Wanasiasa hao wanajulikana, lakini wahindi wanasema "deka jaega".

Inawezekana hujazaa wewe. Ndio mana hujui uchungu wa mwana. Ungekuwa na mtoto au ndugu kwenye hivyo vyuo usingeongea uo upuuzi. Nenda kashinde kule Cheat-Chat ndio kunakufaa.
 
Kweli waone aibu!! wazee wazima kujali matumbo yao tu!! Loh!
 
Serikali ina mkakati wa dhati wa kufanya hili taifa kuwa taifa la mambumbumbu, kwa nini watoto wanaodai elimu wanapigwa mabomu?

Serikali inafikiria nini ???????

Kweli serikali imeshindwa kuwasikia hawa watoto na kuwapa mikopo, hawaombi hela za bia, hawaombi hela za club wanataka elimu.

Serikali yetu hii hivyo ina watu wenye akili kweli?????
 
Hao watoto wakasome wanachochewa na wanasiasa uchwara kwa vichipsi kuku. Wanasiasa hao wanajulikana, lakini wahindi wanasema "deka jaega".

punguza kuvuta bange............. ndo madhara yake hayo!
 
Sidhani hawa viongozi wetu wana watoto kwenye hivi vyuo, Yani wapo tayari kununua maelfu ya mabomu kuliko kuwapatia mahitaji hawa wanafunzi wa vyuo. Labda viongozi wetu hawana watoto, sababu hawajui uchungu wa watoto. Kuna maana gani ya kuwa na viongozi wazee kwenye serikali yetu halafu serikali inakosa busara kama uzee ni busara.

Ukiangalia hizo picha hapo hao wanafunzi wamekaa wakijadili matatizo yao ambayo yanawaumiza na wayapeleke panapohusika. Mnapowawekea Askari na vifaa vya hatari nyuma manake ni nini, ni kuwatisha!!. Kama ni kuwatisha basi serikali ijue inakosea sana badala yake mnawajenga ujasiri hawa wanafunzi bila nyie kujua. Baada ya miaka mingi 20-30 taifa litakuwa na watu wenye hasira ambao hawataliheshimu Jeshi la polisi hata kidogo, mnajenga nchi ya watu wenye visasi wakati huo nyinyi viongozi hamtakuwepo, mtakua mmetuachia balaa watanzania. Ndio mnataka tuwakumbuke kwa hayo!!!.

Ni wazazi gani nyie mnaoshindwa kuongea na vijana wenu, mkawasaidia na kuwatatulia shida zao. Mnafikiri mtaiweza nchi kwa kufanya vitisho!!!.

Kama mnawatisha sana wanafunzi miaka nenda rudi na hakuna anayetishika, mambo yanajirudia vilevile. mmeshindwa kuelewa mnatengeneza nchi ya namna gani.

Ni watoto wa masikini ndio wanateseka hivi!!!!.

Mjue tu kila jambo huwa lina mwisho wake.


View attachment 41032View attachment 41033View attachment 41034View attachment 41035
Kenge huwa hasikii mpaka umtandike hadi damu imtoke maskioni ndo ataskia.
 
Juzi tu wanafunzi wa karatu sec. mliwafanyia hivihivi, hamna aibu nyie, leo UDSM hivyohivyo, na kesho mtaendelea hivyo hivyo. Hamuwezi soma alama za nyakati. Huyo JK ana raha gani kutalii kila siku huku wanafunzi nchini wanapata shida!!!.
 
Polen sana wana udsm,inahuzunisha sana vijana tunavyoteseka,huku tukiona mabilion yanaibiwa mchana kweupe
 
Back
Top Bottom