Wataalamu wa sheria, mtusaidie, mtuelimishe hapa, hili jambo limekaaje?
Ajali, mpaka hapo ilipofikia, ni kweli ndio utaratibu na sheria...kesi ya namna hiyo huwa inakuaje?
Taarifa za awali za polisi hazina mchango hapo?
Insurance, kama ilikuwepo, ina mchango gani hapo?
Waliogongwa, walikuwa kwenye chombo kingine au la, sijasikia, lakini wajuvi mnaweza kutujuza kwa mazingira yote mawili, muelekeo sahihi wa kesi kwa mujibu wa sheria, unapaswa kuwa vipi?
Kweli, nyumba inapaswa kuuzwa?