Serikali Tatu: Mapalala Anashindwa Kuchagua, Anatutisha Kwa Tulichokichagua...!

Serikali Tatu: Mapalala Anashindwa Kuchagua, Anatutisha Kwa Tulichokichagua...!

maggid

JF-Expert Member
Joined
Dec 3, 2006
Posts
1,084
Reaction score
1,246
Ndugu zangu,

Kwenye The Citizen la leo kuna makala ndefu ya Bernard Mapalala. Huyu ni Kaka na mwafamilia mwenzangu kwenye tasnia ya habari.

Mapalala ameanza kujenga hoja yake kwa kuiwekea nguzo za mwandishi Martin Meredith ( The State Of Africa). Bahati nzuri nami ninacho kitabu cha mwandishi huyo na nimekisoma.

Ufananisho wa Nigeria na hoja iliyo mezani kwetu juu ya Katiba na Muundo wa Serikali haungiliani. Ni vitu viwili tofauti. Sisi hatuna Igbo wala Biafra.

Lakini, ukiacha hilo. Ndugu yangu Bernard anahangaika pia na utambulisho wetu. Naamini anajua, lakini anashindwa kuweka wazi sisi ni nani na tumetoka wapi. Anataka hata tuukane Utanganyila wetu.

Bernard anaongea lugha ile ya Waziri Mkuu Pinda Bungeni aliposema kuwa ' Zanzibar Si Nchi'. Baadae ikaonekana kuwa ' Zanzibar Ni Nchi'.

Mapalala nae anataka tuamini kuwa hakujawahi kuwepo Tanganyika kwa kuwa anaandika;
" There was a Tanganyikan State, but there was no Tanganyikan Nation".

Ni yale yale ya ' Zanzibar si nchi ni dola!'. Unawezaje kuwa na dola bila kuwa na nchi?

Na Mapalala huyu katika andiko lake hili refu amejikita katika kutuonyesha hatari ya kuwa na Serikali Tatu na hata kuwepo Tanganyika bila yeye mwenyewe, mahali popote pale, kutueleza wazi anasimamia katika muundo gani wa Serikali.

Nadhani Mapalala angefanya hivyo, na kutueleza ni kwanini tufuate mfumo anaodhani yeye unatufaa, iwe Serikali Moja au Mbili, Ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Jumapili Njema.
http://mjengwablog.com
 
Katumwa huyo! Hana jipya kaka! Cha kujiuliza ni je Dr Salim, Jaji Warioba, Mzee Butiku, Prof Baregu ni VICHAA KUPENDEKEZA SERIKALI 3? JE 2naoshadadia serikali 2 mnaelimu na ufahamu wa nchi yetu kuliko TUME YA KATIBA?
 
Katumwa huyo! Hana jipya kaka! Cha kujiuliza ni je Dr Salim, Jaji Warioba, Mzee Butiku, Prof Baregu na WENGINE ni VICHAA KUPENDEKEZA SERIKALI 3? JE 2naoshadadia serikali 2 mnaelimu na ufahamu wa nchi yetu kuliko TUME YA KATIBA?
 
...katika mambo yoote,hili la serikali tatu lazima litaigharimu ccm na washirika wake na lazima wagonge pua chini watake wasitake,tumeamua na haturudi nyuma mpaka kieleweke...
 
Siku nyingi huwa nasoma habari zako kwa leo angalau umenikuna.
Asante sana.
 
Inawezekana kweli haijawahi kuwapo Tanganyika Nation, lakini zanzibar inapojitutumua na kujiita Nation, na sisi tunalazimika kubaki kama Taifa, tunaanza kujitambua kutokea hapo.
 
Miaka mingi nchii imelilia serikali 03, ni hivyo hakuna zaidi.

Tume imefanya vizuri sana maana imezingatia maoni ya watu wote na kuyapima kwa makini.

Anayeongelea serikali 02 na huku anapinga serikali 03 si mwezetu. Tujiepushe naye - ana lake jembo. Ni mnyonyaji, fisadi na asiyependa watu wawe huru. Nadhani anasimama katika hoja ileile - Huwezi kutawala matajiri- Kwa hiyo wafukarishe watu wote ili uwatawale. Watakubali uwatawale mpaka lini?
 
Tujiulize kwanza maana ya nation na state na ni jinsi gani hizo mantiki zinahusiana na suala la idadi za serikali.
 
Sitta alisema serikali tatu ni ulafi tu kama mbili zimetushinda tuwe na moja tu mengine majanga.
 
Ndugu zangu,

Kwenye The Citizen la leo kuna makala ndefu ya Bernard Mapalala. Huyu ni Kaka na mwafamilia mwenzangu kwenye tasnia ya habari.

Mapalala ameanza kujenga hoja yake kwa kuiwekea nguzo za mwandishi Martin Meredith ( The State Of Africa). Bahati nzuri nami ninacho kitabu cha mwandishi huyo na nimekisoma.

Ufananisho wa Nigeria na hoja iliyo mezani kwetu juu ya Katiba na Muundo wa Serikali haungiliani. Ni vitu viwili tofauti. Sisi hatuna Igbo wala Biafra.

Lakini, ukiacha hilo. Ndugu yangu Bernard anahangaika pia na utambulisho wetu. Naamini anajua, lakini anashindwa kuweka wazi sisi ni nani na tumetoka wapi. Anataka hata tuukane Utanganyila wetu.

Bernard anaongea lugha ile ya Waziri Mkuu Pinda Bungeni aliposema kuwa ' Zanzibar Si Nchi'. Baadae ikaonekana kuwa ' Zanzibar Ni Nchi'.

Mapalala nae anataka tuamini kuwa hakujawahi kuwepo Tanganyika kwa kuwa anaandika;
" There was a Tanganyikan State, but there was no Tanganyikan Nation".

Ni yale yale ya ' Zanzibar si nchi ni dola!'. Unawezaje kuwa na dola bila kuwa na nchi?

Na Mapalala huyu katika andiko lake hili refu amejikita katika kutuonyesha hatari ya kuwa na Serikali Tatu na hata kuwepo Tanganyika bila yeye mwenyewe, mahali popote pale, kutueleza wazi anasimamia katika muundo gani wa Serikali.

Nadhani Mapalala angefanya hivyo, na kutueleza ni kwanini tufuate mfumo anaodhani yeye unatufaa, iwe Serikali Moja au Mbili, Ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Jumapili Njema.
MjengwaBlog :: Habari, Picha, Matangazo na Matukio

kwa kweli hata mie sipendelei serikali mbili, maana zanzibarb wa:shock😱 wana katiba yao inojitosheleza kwa nini sisi bara ndo tuwe wa kuburutwa tu kila siku? mie naona serikali tatu ni jawabu, la muungano ufe kwani hauna faida kwa watu wa bara, ukizingatia hatuna uhuru wa kumiliki ardhi visiwani ila raia wenye asili ya visiwani wana uhuru wa kumiliki ardhi bara! serikali tatu na katiba ya tanganyika (tz bara) ambayo itakuwa inatulinda watanganyika muhimu. sasa hivi watanganyika tuko kama yatima tunaoburuzwa na walezi wetu!
 
Mimi ni muhumini wa serikali tatu lakin siyo sahihi kusema kuwa muungano hauna tija kwa watanzania wote wa tanganyika na wa zanzibar. Mimi ndungu zangu wanafanya biashara mji mkongwe pamoja na watu wengine wengi kutoka Ar chuga. Karibu 90% ya maduka ya utalii mji mkongwe wanamili hawa jamaa wa Ar. Hamuni kuwa muungano ukivunjika watapata tabu ya kufanya business zao. Wapemba nao wanamili biashara nying kariakoo na magorofa kibao sasa hamuoni kuwa muungano ukivunjika kutakuwa na matatizo kwa watu wetu hawa. Tuongelee kuimarisha muungano siyo kuuvunja.
 
Katumwa huyo! Hana jipya kaka! Cha kujiuliza ni je Dr Salim, Jaji Warioba, Mzee Butiku, Prof Baregu ni VICHAA KUPENDEKEZA SERIKALI 3? JE 2naoshadadia serikali 2 mnaelimu na ufahamu wa nchi yetu kuliko TUME YA KATIBA?

Hao ni vichaa haswaa, tena ni wazee ambao Wako fasturated, wakati Nyerere akiwepo walikuwa wanamlamba miguu na kujifanya wanafunzi wake wenye nidham sasa amekufa wamemsaliti.
 
Back
Top Bottom