Serikali, tuzike watakaopeteza Maisha kutokana na COVID19 kwa heshima. Utaratibu uwekwe wazi

Serikali, tuzike watakaopeteza Maisha kutokana na COVID19 kwa heshima. Utaratibu uwekwe wazi

introvert

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2010
Posts
1,372
Reaction score
2,420
WanaJF,

Bila kuandika mengi, ombi kwa Serikali ni kupumzisha ndugu zetu kwa heshima na kwa utaratibu unaoeleweka na kwa uwazi.

Kwa sasa Serikali imeamua kutumia "HERD IMMUNITY" kama njia ya kupambana na huu ugonjwa. Hii ni kutokana na kauli ya Rais alipozungumza na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama, matendo ya Serikali kusisitiza kazi ziendelee kama maBar, Ibada, usafiri wa umma, n.k. na sasa kauli ya Waziri Kigwangala.

Njia hii inayotumiwa inatabiriwa kuwa na vifo vingi na kwa utaratibu wa sasa ni Serikali inayozika miili ya wanaopeteza maisha. Iwapo vifo vitakua vingi kama inavyotabiriwa, maombi kwa Serikali ni kuandaa utaratibu wa wazi na unaoeleweka wa kuzika wale wote watakaopeteza maisha.

Hakuna sababu yoyote ya kuficha vifo au kuzika kwa usiri usiku.

Kila mkoa, hata wilaya, itenge maeneo kuhakikisha kuna nafasi ya kutosha ya kuzika na utaratibu uwekwe wazi wa jinsi ya kuzika.

Serikali imechagua njia hatari ya HERD IMMUNITY basi wale watakaopeteza maisha wazikwe kwa heshima.

Mwisho, kwa namna yoyote ile, lazima wale waliofanya maamuzi wawe RESPONSIBLE and ACCOUNTABLE.
 
Kama hadithi Fulani za kutisha mtu anakusimulia naomba hivyo hivyo iendelee kuwa kama hadithi tu ila kama kweli utakua ndio uhalisia itakuwa balaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Toka lini virus wakawa na herd immunity? Kwa system hii watu wengi watapoteza maisha.
Hata mafua ukipona unaweza kuumwa tena, pia hata corona ukipona unaweza kuumwa tena.

Kuwaza herd immunity kwenye corona ni upuuzi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni upuuzi wa hali ya juu. Hawajui hata wao hawapo immunised. Hii njia nchi itajikuta inapoteza watumishi wa afya. Na hivi hakuna PPE. Yaani naona giza tu. Tangagiza.
Na tukipoteza watumishi wa afya nani atatoa huduma ?Hii itasababisha watu wengi sana kupoteza maisha.
 
Kuna mtu alitamka hatuwezi kuzuia ndege za kimataifa ili tusikose watalii, sasa hao watalii sijui kwa sasa wako wapi.

Hakuna mtalii atakayekuja hata wakianza kusafiri. Mtalii hawezi kuja nchi ambayo haionyeshi kupambana na tatizo hili. Watakuja pale itakapopatikana chanjo.
 
Toka lini virus wakawa na herd immunity? Kwa system hii watu wengi watapoteza maisha.
Hata mafua ukipona unaweza kuumwa tena, pia hata corona ukipona unaweza kuumwa tena.

Kuwaza herd immunity kwenye corona ni upuuzi.

Sent using Jamii Forums mobile app

Ni hatari sana kuchukua njia hii kwani inaweza kupelekea idadi kubwa ya vifo na kuua sekta ya afya. Maajabu zaidi ni kuona waziri Kigwangala mwenye medical degree akitetea hii njia.
 
Wanazika usiku kama wachawi

♡♤Life belongs to all who struggle for it♤♡♧
 
Ni upuuzi wa hali ya juu. Hawajui hata wao hawapo immunised. Hii njia nchi itajikuta inapoteza watumishi wa afya. Na hivi hakuna PPE. Yaani naona giza tu. Tangagiza.
Na tukipoteza watumishi wa afya nani atatoa huduma ?Hii itasababisha watu wengi sana kupoteza maisha.

Umeongea ukweli. Sekta ya Afya haiwezi kuhudumia wagonjwa wengi kwa wakati mmoja. Ratio ya daktari kwa mgonjwa tayari ni tatizo sasa kujaribu hii njia ni kuipeleka sekta nzima ya afya kaburini.
 
Back
Top Bottom