Kwanza nianze kuomba radhi kama sijaielewa sana hoja ya Mh Nchemba ya mfuko wa Elimu ya juu. Nasema naomba radhi kwa sababu kama serikali muda wote imekuwa ikijisifia kwa kuongeza fedha ktk kufanikisha wote walio na sifa ya kupata mkopo wa Elimu ya juu wanapata, iweje leo hii tuanzishe tena kitu ambacho naweza kukiona kama ni parallel to HESLB?Pili, Nadhani serikali na wabunge mnatuchezea tu. Nasema mnatuchezea kwa mambo yafuatayo; a) Pale Bodi ya Elimu ya juu maafsa mikopo wale sidhani kama wanafahamu wajibu wao na hata sijui kama nyie wabunge na serikali mnatambua majibu na aina ya huduma watoazo wale maafsa pale bodi ya mikopo.Nimesema maafsa hawatambui kazi ni ipi kwa sababu ukifika kwa huduma hizo utasikia mwingine anakwambia kwanza kwa nini unafuatilia mkopo wakati tayari muhula unakaribia kwisha kwani si ujilipie tu? Kibaya nikiwa hapo ndani alikuja bwana mmoja nadhani anasoma shahada ya uzamili ama uzamivu.
Alipoeleza kuwa nae hajapata mkopo tena hafahamu sababu zilizomsababisha asipate mkopo alijibiwa na nyie si mjisomeshe tu yaani wewe unasoma shahada ya Uzamivu unafuatilia mkopo? Kajisomesheni kwa mishahara yenu. Baya zaidi pia ni kuwa pale ndani kila mtu nadhani ni kama kachanganyikiwa vile. Nasema hivyo kwa sababu yule dada alimjibu hivyo yule bwana aliekuwa anafuatilia mkopo na akamsisitizia kuwa wale wa Uzamivu wote wameshapewa mkopo. Lakini mie nina ndugu yangu anasoma UZAMIVU hajapata mkopo huo. Nasema serikali na wabunge tatizo la mikopo hamlifahamu ya nini kuanzisha Mfuko wa elimu wakati wahudumu ndo wanatoa majibu kama haya?
Alipoeleza kuwa nae hajapata mkopo tena hafahamu sababu zilizomsababisha asipate mkopo alijibiwa na nyie si mjisomeshe tu yaani wewe unasoma shahada ya Uzamivu unafuatilia mkopo? Kajisomesheni kwa mishahara yenu. Baya zaidi pia ni kuwa pale ndani kila mtu nadhani ni kama kachanganyikiwa vile. Nasema hivyo kwa sababu yule dada alimjibu hivyo yule bwana aliekuwa anafuatilia mkopo na akamsisitizia kuwa wale wa Uzamivu wote wameshapewa mkopo. Lakini mie nina ndugu yangu anasoma UZAMIVU hajapata mkopo huo. Nasema serikali na wabunge tatizo la mikopo hamlifahamu ya nini kuanzisha Mfuko wa elimu wakati wahudumu ndo wanatoa majibu kama haya?