Serikali: Wanafunzi wasizuiwe kwenda likizo

Serikali: Wanafunzi wasizuiwe kwenda likizo

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amesema wamepokea malalamiko kwamba kuna Shule zinazuia Wanafunzi kwenda likizo bila kushauriana na Wazazi huku Wazazi wengine wakitakiwa kulipa ili kuwaweka Wanafunzi Shuleni ambapo amewataka Viongozi wa Shule kutambua kuwa ni haki ya Mwanafunzi kwenda likizo.

Akiongea Jijini Dodoma Mkenda amesema “Kwa Shule za Serikali kuna mwongozo umetolewa na Kamishna wa Elimu wa siku za kufunga na kufungua Shule, ni muhimu sana tukajifunza kuzingatia huo mwongozo ili Wanafunzi wapate muda pia wa kupumzika, nahimiza Wakuu wa Shule wote na Wakurugenzi wazingatie utaratibu huo"

"Kwa Shule binafsi Kamishna alisema waangalie kalenda lakini wanaweza kufanya adjustment kulingana na mahitaji yao lakini ukweli unabaki palepale kwamba Wanafunzi wetu wanahitaji kupumzika"

"Wito wetu ni kwamba tusipelekee Kamishna atoe waraka wenye masharti makali kwa Shule binafsi, Wanafunzi wana haki ya kupumzika, likizo zimewekwa ili Watoto wapate muda wa kupumzika, wakae na Wazazi wao, wapate kucheza vilevile na kubadilisha mazingira na hii huwa inawasadia"




Soma mijadala ya kulalamikia wanafunzi kubaki shuleni:
 
Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amesema wamepokea malalamiko kwamba kuna Shule zinazuia Wanafunzi kwenda likizo bila kushauriana na Wazazi huku Wazazi wengine wakitakiwa kulipa ili kuwaweka Wanafunzi Shuleni ambapo amewataka Viongozi wa Shule kutambua kuwa ni haki ya Mwanafunzi kwenda likizo.

Akiongea Jijini Dodoma Mkenda amesema “Kwa Shule za Serikali kuna mwongozo umetolewa na Kamishna wa Elimu wa siku za kufunga na kufungua Shule, ni muhimu sana tukajifunza kuzingatia huo mwongozo ili Wanafunzi wapate muda pia wa kupumzika, nahimiza Wakuu wa Shule wote na Wakurugenzi wazingatie utaratibu huo"

"Kwa Shule binafsi Kamishna alisema waangalie kalenda lakini wanaweza kufanya adjustment kulingana na mahitaji yao lakini ukweli unabaki palepale kwamba Wanafunzi wetu wanahitaji kupumzika"

"Wito wetu ni kwamba tusipelekee Kamishna atoe waraka wenye masharti makali kwa Shule binafsi, Wanafunzi wana haki ya kupumzika, likizo zimewekwa ili Watoto wapate muda wa kupumzika, wakae na Wazazi wao, wapate kucheza vilevile na kubadilisha mazingira na hii huwa inawasadia"
#MillardAyoUPDATES


NB: Hongera Jamii Forums, malalamiko yamesikilizwa
 
Sasa wabunge washadakia huko, wanaenda kuliongelea, nawakati wabunge wengi Wana shule binafsi Sasa kama siyo kutaka kujipendelea ni Nini? Tena wanaongelea darasa la Saba eti wanafanya mtihani mwezi wa Tisa na mitaala inaisha wa kumi na Moja wakati hakuna kitu kama hicho, Sasa hawa watoto wadogo wa darasa la nne?

Na Cha ajabu wao wanapumzika hawakai bungeni mwaka mzima, Sasa kwanini watoto wa shule wasipate mapumziko?

Inamaana walimu wanauchungu wa kuwasaidia wazazi kulea kuliko hao wazazi wanaopenda watoto wao wasiwaone nyumbani ila wakawe shule tu, wengine mpaka makambi wanatengeza watoto wadogo wakajihudumie huko shule, kama tumefika huku itabidi na Kambi za watu wazima zitengenezwe ili watoto wakiwa wakubwa waishi kwa kutafuta pesa pekee hakuna kwenda kusalimia hata wazazi maana watahitaji kutafuta pesa mwaka mzima, alafu imagine mtoto anasoma boarding eti kisa ni darasa la mtihani basi harudi nyumbani ni kukaa tu shule maisha yake yote hiyo ni haki kweli?
 
Asa angetoa tamko jamani hata kama ndo tunataka watoto wasome ndo mtoto anafunga jumatano hiyohiyo anaendelea na kitabu tena full time?

Haitoshi kuna mkoa umeweka mock tarehe 4/7 maana yake wanalazimisha watoto wasifunge kwa ratiba kama hiyo
 
Mie mwanangu nilimwambia kabisa huendi,hata jumamosi nimekataa haendi. Full stop.
Kwa uzoefu hizi tuition watoto wanagongana sana na kugongwa pia. Huwa hazina uagalizi maalumu. Hivyo walimu na jemba zisizo na adabu huwagonga.
 
Hakuna kitu nlikuwa spendi kama tuition aise maisha yangu yote ya shule..mama angu alikuwa mwalimu pale Musoma kulikuwa anaitwa TEMU alikuwa anafundisha sana tuition mjini kule..mama angu alikuwa akiskia walimu wa tuition popote lazima akupeleke ukasome'binafsi skuwa shabiki wa hizo mambo kabisa nlichokuwa nafanya ni kuanguka ule uwanja wandege pale Musoma narudi home..badae mama kagundua mchezo nkamwambia spendi tuition kabisa akaniacha..sekondari tote kusoma tuition likizo nilikuwa naitumia kusaidia kazi za nyumbani na kuleta wadogo zangu..Advance pia skusoma tuition nlikuwa stationery kwa baba angu mdogo effectively kabisa likizo zote nlijihusisha na mambo ya kijani nkirudi shule nlikuwa nakomaa na discussion na yale waliyosoma tuition na nlikuwa the best student nkapata zawadi ..nliperfom vizuri kwenda chuo pia so mzazi kama unaona mwanao haelekei usimlazimishe inachosha san kusoma through out non stop 24 7 360 hakuna kupumzika...hizo mambo za kijani ndo zinaniweka mjini kwa sasa ninaofisi yangu inaniweka mjini(stastionery)na nimeajiriwa pia.hii kitu pia ni kama nimewarithisha wanangu naona nao wanapita mulemule
 
Prof mkenda tuachie watoo wetu wasome we wako wako st kayumba?
 
Kwa aina ya kizazi kilichopo sasa, ukikiacha kirahisi tu kurudi nyumbani "kupumzika" wakati wa likizo, basi kuna kila dalili kwa shule nyingi za sekondari kuja kuvuna mabua wakati kutoka kwa matokeo ya NECTA.

Naunga mkono hoja ya kuyabakiza shuleni yale madarasa ya mitihani (form 2 na 4) kwa makubaliano kati ya wazazi na uongozi wa shule.
 
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amesema wamepokea malalamiko kwamba kuna Shule zinazuia Wanafunzi kwenda likizo bila kushauriana na Wazazi huku Wazazi wengine wakitakiwa kulipa ili kuwaweka Wanafunzi Shuleni ambapo amewataka Viongozi wa Shule kutambua kuwa ni haki ya Mwanafunzi kwenda likizo.

Akiongea Jijini Dodoma Mkenda amesema “Kwa Shule za Serikali kuna mwongozo umetolewa na Kamishna wa Elimu wa siku za kufunga na kufungua Shule, ni muhimu sana tukajifunza kuzingatia huo mwongozo ili Wanafunzi wapate muda pia wa kupumzika, nahimiza Wakuu wa Shule wote na Wakurugenzi wazingatie utaratibu huo"

"Kwa Shule binafsi Kamishna alisema waangalie kalenda lakini wanaweza kufanya adjustment kulingana na mahitaji yao lakini ukweli unabaki palepale kwamba Wanafunzi wetu wanahitaji kupumzika"

"Wito wetu ni kwamba tusipelekee Kamishna atoe waraka wenye masharti makali kwa Shule binafsi, Wanafunzi wana haki ya kupumzika, likizo zimewekwa ili Watoto wapate muda wa kupumzika, wakae na Wazazi wao, wapate kucheza vilevile na kubadilisha mazingira na hii huwa inawasadia"




Soma mijadala ya kulalamikia wanafunzi kubaki shuleni:

Amejibu kisiasa.. hajatoa order.

Mjanja Sana huyu.
 
Back
Top Bottom