Serikali watuambie ukweli wa hizi tozo

Serikali watuambie ukweli wa hizi tozo

pakaywatek

JF-Expert Member
Joined
Dec 28, 2014
Posts
4,660
Reaction score
6,282
Walisema wameongeza shilingi 100 kwenye mafuta kwa ajili ya barabara, wakaanzisha makato kwenye miamala wakadai ni kwa ajili ya barabara, wakakopa trilioni 2.7 kwa ajili ya barabara. Kwa nini wasituambie ukweli wasingizie barabara?

Hii ni mbali na 1200 kwa kila lita moja ya mafuta ya kula, shilingi 3100 kwenye mtungi wa gesi.
 
Ajabu ni kuwa vijana wa UVCCM wako busy kutengeneza/kufake habari za kuonyesha kuwa mbowe ni gaidi. Hakuna ugaidi mbaya kama huu ambao serikali inawafanyia wananchi wanyonge.
 
Wameona kwenye tozo ya miamala watu wengi wamesusa. Na kwenye mafuta idadi ya Wamiliki wa magari Tanzania haifiki hata milion. Sasa nikuwabana tu jambanani kina Etwege Idugunde MZALAMO kwenye luku
 
Kuna tatizo mahala, nadhani kuna wajanja wanamdanganya Samia waendelee kutupiga watanzania, haiwezekani tozo mpya kila kukicha mpaka wanasahau kama walishatudanganya sababu ya tozo hizo, barabara tozo, huku kuna mkopo toka bank ya dunia kwa ajili ya barabara.

Huyu Rais wetu aamke, aiangalie serikali yake anayoiongoza inaendaje, ni kama vile amekaimu majukumu yake kwa wasaidizi wake kwa kujua, au bila kujua, ni vurugu.

Nimeona kwenye gazeti tozo kwenye vituo vya mafuta, reli, saloon, nk hizi pesa zote zinaenda wapi? mwananchi mmoja mwenye saluni yake akatwe tozo kwenye saluni, bei ya mafuta, miamala ya simu, na kodi ya majengo kwa luku, huu ni ujinga, sio ubunifu.

Tuliambiwa Magufuli alikuwa anawaibia watu pesa zao akajenge miundombinu, sasa iweje pesa alizoiba Magufuli zitoshe kuendeleza hiyo SGR na Nyerere Dam wakati hii serikali ya Samia inahangaika kubuni kila aina ya tozo? hapa tatizo ni vichwa vya hawa viongozi, sioni sababu nyingine.

Pamoja na yote haya bado utasikia uhaba wa vyumba vya madarasa, na ukosefu wa maji safi na salama.

Samia aamke toka usingizini, haya mambo amewaachia wengine wayafanye badala yake yataendelea kumsababishia achukiwe na wananchi, na kudharauliwa, aanze kuwa mfuatiliaji yeye binafsi, asikae tu ofisini na kupanda ndege kila siku.
 
Walisema wameongeza shilingi 100 kwenye mafuta kwa ajili ya barabara, wakaanzisha makato kwenye miamala wakadai ni kwa ajili ya barabara, wakakopa trilioni 2.7 kwa ajili ya barabara. Kwa nini wasituambie ukweli wasingizie barabara?

Hii ni mbali na 1200 kwa kila lita moja ya mafuta ya kula, shilingi 3100 kwenye mtungi wa gesi.
Barabara zipi, hii barabara ya makongo haifiki km. 2 lakini ina zaidi ya miaka kumi inajengewa mdomoni tu.........kifupi haiendi popote na watu wanakula vumbi daily, wakadanganye wajinga wajinga......
 
Walisema wameongeza shilingi 100 kwenye mafuta kwa ajili ya barabara, wakaanzisha makato kwenye miamala wakadai ni kwa ajili ya barabara, wakakopa trilioni 2.7 kwa ajili ya barabara. Kwa nini wasituambie ukweli wasingizie barabara?

Hii ni mbali na 1200 kwa kila lita moja ya mafuta ya kula, shilingi 3100 kwenye mtungi wa gesi.
Johnson & Johnson anatoka Amerika kote kule mpaka Bongo hapa bure bure tu........! Lengo kuu la hizo tozo ndo Hili Sasa na hautakuja kuambiwa na mtu mwingine Hadi kiama.
 
Walisema wameongeza shilingi 100 kwenye mafuta kwa ajili ya barabara, wakaanzisha makato kwenye miamala wakadai ni kwa ajili ya barabara, wakakopa trilioni 2.7 kwa ajili ya barabara. Kwa nini wasituambie ukweli wasingizie barabara?

Hii ni mbali na 1200 kwa kila lita moja ya mafuta ya kula, shilingi 3100 kwenye mtungi wa gesi.
Ukweli Maza alikuta kasiki liko tupu kabisa. Kwa ule utaratibu wa kulindana na kukilinda chama imebidi sisi walalahoi tuzugwe huku tukikamuliwa hadi tone la mwisho la damu. Dua ziendeleeeeee tu Mungu atajibu.
 
Back
Top Bottom