DOKEZO Serikali Wilayani Ludewa chunguzeni mwenendo wa Mwalimu huyu, analalamikiwa na wengi

DOKEZO Serikali Wilayani Ludewa chunguzeni mwenendo wa Mwalimu huyu, analalamikiwa na wengi

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

try me

Member
Joined
Nov 8, 2024
Posts
16
Reaction score
11
Lamwike JF
Huku kijijini kwetu Njelela kilichopo Kata ya Mundindi, Wilaya ya Ludewa, Mkoa wa Njombe kuna Mwalimu anatutesa sana, kwa sasa amekaimu Utendaji wa Kijiji baada ya Mtendaji aliyekuwepo kwenda likizo ya uzazi.

Mwalimu huyo (jina nalihifadhi kwa muda) anachotutendea sisi Wakazi wa Njelela ni unyanyasaji na ukatili, kwanza akikuhisi umetenda kosa bila kutafuta ushahidi, bila kukuuliza anakuita na kukuadhibu.

Adhabu hiyo ni kukuchapa fimbo haijalishi wewe ni mtu mzima au kijana, anatandika kama anapiga nyoka.

Hivi karibuni alimchapa mtu mmoja baada ya kumkuta na kosa analolijua yeye. Baada ya kumchapa akampa faini ya shilingi laki tatu ikiwa atashindwa basi watauza nyumba yake akamwambia na mteja ameshapatikana.
IMG-20241227-WA0005.jpg

IMG-20241227-WA0003.jpg
Cha kusikitisha nyumba ile wameshaiuza na kijana wa watu hana pa kuishi tunajiuliza hizo pesa walizouza nyumba (milioni 6) ziko wapi?

Kubwa kuliko amempiga kijana mwingine juzi tu hadi akamvunja mguu wa kulia, tulipofika Hospitali ya Lugarawa wakasema hadi PF 3, Tulivyoenda Polisi wakamhitaji mtu aliyefanya unyama huo.

Mwalimu akaitwa alipofika akaomba jambo hilo limalizwe pembeni lisiende Mahakamani kwamba atagharamia matibabu ya mtu huyo.

Sasa sisi Wananjelela tutateswa na huyu mwalimu hadi lini? Kwakuwa yeye ana pesa kidogo anaona fahari kutufanyia ukatili. Anatubambikia kesi kwa makosa yasiyoeleweka akikuhisi tu kwa lolote. Unaadhibiwa. Sasa hivi amani imetoweka vijana na wazee wote tumejawa na uoga wa kufanyiwa lolote na mwalimu huyu.

FB_IMG_1734967890027 ziba.jpg
Sio Afisa Elimu aliyechukua hatua dhidi yake wala Mtendaji wa Kijiji, anafikiri tumesahau? Au kwakuwa yeye ni Mtumishi wa Serikali anajiona yuko juu ya Sheria kwa kufanya chochote atakacho?

Kupitia jukwaa hili tunaomba hatua zichukuliwe, tunataka amani ya kijiji chetu irudi hatutaki kuishi kwa hofu ya kumwogopa mtu. Tunataka tunywe ulanzi na ughimbi kwa amani ile tuliyoizoea.

Ujumbe huu umfikie Mkuu wa Wilaya, tunaomba sisi wananjelela tusikilizwe na tupewe haki yetu ya kusikilizwa endapo kuna makosa yametokea na sio kuadhibiwa kama watoto wadogo.

Nidaliha🙏
 
Kwanza niseme wanakijiji wote ni wajinga na hamna akili,mtu mmoja mwalimu tena failure mmoja ,
Yani nyie watu sijui mkoje mana mnatia hasira,huu upande wetu wa kanda maalumu akitokea mpumbavu mmoja kama huyu kesho yake kwao wanazika,
Trna wakati mwingine usiandike mambo ya kipuuzi kama haya,natamani ata ningekua karibu na wewe nikuchape ata vitasa kadhaa
 
Mwalimu chalaza kabisa viboko hao wanakijiji wasiojitambua. Si umeona sasa, baada ya kuwachalaza, akili zimeanza kuwakaa sawa.

Tungekuwa na walimu laki 1 tu kama wewe, naamini hata CCM isingeendelea kuwafanyia mamilioni ya wananchi mambo ya kipuuzi.
 
Watanzania wengi ni wajinga washazoea kupelekwa kama kondooo,imagine eti mnashitaki jamii forum mnashindwa kumbonda vizuri.Alafu hawa watu waliofeli shule wanapenda sana kutumia nguvu badala ya akili.
Asee inasikitisha juzi hapa mjini nilipata kumpeleka dada mmoja kliniki (zahanati)jamani wamama wanatukanwa na vile vinesi kama watoto wadogo yaani wanatukanwa hovyo hovyo.Nenda hospitali za government uone form four failures wanavyotukana wagonjwa.
Mimi ukiingia kwenye anga zangu utajuta mbona.
 
Back
Top Bottom