Serikali ya JK kuhamisha Wanakijiji kumpa mwekezaji ardhi

Watanzania

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2009
Posts
727
Reaction score
44
Serikali yetu ni inashangaza. Jana TBC1 imeripoti kuwa mkuu wa wilaya huko Kilombero anasimamia mchakato wa kutaka kuhamisha wanakijji wa kijiji cha Namawala huko Kilombero kinyume na matakwa yao ili mwekazaji apewe ardhi ya kijiji kulima miwa.

Yaani Wanakijiji watanzania wanaokaa katika kijiji kisheria wahamishwe kutoka kwenye ardhi yao yenye rutuba apewe Mnyonyaji. Hii tabia ya serikali inayoota mizizi inatofautiana vipi na wakoloni ambao walichukua ardhi yetu yenye utajiri wa maliasili? Hivi wanakijiji ndio wanaostahili kukaa maeneo yasiyofaa? Tumesikia huko Loliondo sasa wanaelekea Kilombero, hii ni serikali gani isiyojali wananchi wake kwa kiwango hiki? Hivi serikali inaajenda ya siri ya kurudisha ukoloni nchini kwetu? Wananchi wanataabika tayari kwa hali ngumu ya maisha, serikali ikiendekeza sera ya kunyang’anya ardhi watanzania ambayo ndiyo tegemeo lao na kuwapa wanyonyaji hali itakuwaje?
 
Mumeangalia ile video ya Bulyankulu? Ndizo sera za serikali ya kifisadi hizo. Mzungu kwanza, fisadi anafuata na wananchi ole wenu.
 
Mumeangalia ile video ya Bulyankulu? Ndizo sera za serikali ya kifisadi hizo. Mzungu kwanza, fisadi anafuata na wananchi ole wenu.

Tufanye nini sasa kujiokoa, manake wananchi hawataki, wanaharakati wanapinga lakini...
 
Haya ndio waliofanyiwa Wazimbabwe na waingereza, Waafrica Kusini na Makaburu ikawaletea umaskini mpaka leo. Tusipoangalia vizuri tukiwaachia hawa viongozi wetu wenye njaa na ufinyu wa mawazo, tutajapigania uhuru wetu upya very soon. Kuna haja ya wanaharakati kungilia kati kuzuia operation kama hizi hata ikibidi kutumia nguvu.
 
Ndo Kilomo Kwanza Hiyo imeanza!! Hamna kilichobaki kuuza wameona bora wauze ardhi sasa!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…