Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kukodishia visiwa 52 wawekezaji

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kukodishia visiwa 52 wawekezaji

Lady Whistledown

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2021
Posts
1,147
Reaction score
2,008
Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi ametema nyongo kuhusu mambo saba aliyosema yamekuwa yakipotoshwa kwa makusudi ili kumkatisha tamaa, lakini akasisitiza kuwa hatarudi nyuma hata hatua moja.

Dk Mwinyi alitoa kauli hiyo jana, wakati akizungumza na waandishi wa habari katika utaratibu wake wa kuzungumza nao kila mwisho wa mwezi, huku akitaja makundi matatu yanayofanya upotoshaji huo.

Eneo la kwanza lililotajwa na Rais Mwinyi akisema linapotoshwa, ni ukodishwaji wa visiwa akisema jambo hilo limekuwa likisemwa tofauti na uhalisia.

“Serikali imeamua kukodisha visiwa vidogo 52 na mpaka sasa tayari visiwa 10 vimeshapata wawekezaji, lakini watu wanapotosha kwamba Serikali imeuza visiwa hivyo, jambo ambalo halina uhalisia,” alisema

Aliongeza; “Uhalisia ni kwamba tumewekeza kwa kuangalia uwezo wa mwekezaji, kiasi atakachotanguliza kwa Serikali na kiasi cha mtaji alionao. Na kuweka sawa ukodishwaji wa visiwa haujaanza kwenye Serikali hii, sema sisi tumeboresha zaidi na wananchi watanufaika,” alisema.

Ufafanuzi huo wa Dk Mwinyi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, umekuja kufuatia mjadala miongoni mwa Wazanzibari, akiwamo aliyekuwa kada maarufu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Baraka Shamte, ambaye hivi karibuni alionekana katika kipande cha video akimtuhumu Rais huyo kwa mambo mbalimbali, ikiwamo ukodishwaji wa visiwa. Hata hivyo, siku chache baadaye, Shamte aliomba radhi kwa kauli alizotoa dhidi ya Rais.

Sula la ukodishwaji wa visiwa, pia liliwahi kuelezwa na mbunge wa zamani wa Malindi, Ally Saleh katika ukurasa wake wa Facebook, akisema hana shida na suala la ukodishwaji wa visiwa kwa miaka 99, lakini hoja yake iko kwenye visiwa ambavyo vinakaliwa na watu.

Akifafanua maelezo hayo baada ya kupigiwa simu na Mwananchi, Saleh alisema: “Visiwa ambavyo havina watu, mimi niko okay (sina tatizo navyo), isipokuwa kisiwa cha Misali. Hoja yangu kwenye kisiwa cha Misali ni sehemu nzuri, ni kama Ngorongoro ya baharini, ni kama Loliondo ya baharini, jinsi kilivyo na rasilimali.’’

Saleh aliongeza kwamba ukijenga hoteli kwenye kisiwa hicho, maana yake shughuli za kibinadamu zitaongezeka na hatimaye matumbawe yatakatwa, samaki watakimbia na mazalia ya samaki yatatoweka.

Chanzo: MWANANCHI
 
Serikali zetu licha ya kukusanya kodi zinashindwa kabisa kuwa na mipango endelevu kwa ajili ya haya masuala, wao kila kitu wanawaza wawekezaji, akili zao hazifanyi kazi tena.
 
Serikali zetu licha kukusanya kodi zinashindwa kabisa kuwa na mipango endelevu kwa ajili ya haya masuala, wao kila kitu wanawaza wawekezaji, akili zao hazifanyi kazi tena.

Ndio ccm hao wenye miaka zaidi ya 40 madarakani
 
Safi sana huku Loliondo na Ngorongoro kule Zanzibar uchumi wa buluu mtu na dadake wanaupiga mwingi.
 
Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi ametema nyongo kuhusu mambo saba aliyosema yamekuwa yakipotoshwa kwa makusudi ili kumkatisha tamaa, lakini akasisitiza kuwa hatarudi nyuma hata hatua moja.

Dk Mwinyi alitoa kauli hiyo jana, wakati akizungumza na waandishi wa habari katika utaratibu wake wa kuzungumza nao kila mwisho wa mwezi, huku akitaja makundi matatu yanayofanya upotoshaji huo.

Eneo la kwanza lililotajwa na Rais Mwinyi akisema linapotoshwa, ni ukodishwaji wa visiwa akisema jambo hilo limekuwa likisemwa tofauti na uhalisia.

“Serikali imeamua kukodisha visiwa vidogo 52 na mpaka sasa tayari visiwa 10 vimeshapata wawekezaji, lakini watu wanapotosha kwamba Serikali imeuza visiwa hivyo, jambo ambalo halina uhalisia,” alisema

Aliongeza; “Uhalisia ni kwamba tumewekeza kwa kuangalia uwezo wa mwekezaji, kiasi atakachotanguliza kwa Serikali na kiasi cha mtaji alionao. Na kuweka sawa ukodishwaji wa visiwa haujaanza kwenye Serikali hii, sema sisi tumeboresha zaidi na wananchi watanufaika,” alisema.

Ufafanuzi huo wa Dk Mwinyi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, umekuja kufuatia mjadala miongoni mwa Wazanzibari, akiwamo aliyekuwa kada maarufu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Baraka Shamte, ambaye hivi karibuni alionekana katika kipande cha video akimtuhumu Rais huyo kwa mambo mbalimbali, ikiwamo ukodishwaji wa visiwa. Hata hivyo, siku chache baadaye, Shamte aliomba radhi kwa kauli alizotoa dhidi ya Rais.

Sula la ukodishwaji wa visiwa, pia liliwahi kuelezwa na mbunge wa zamani wa Malindi, Ally Saleh katika ukurasa wake wa Facebook, akisema hana shida na suala la ukodishwaji wa visiwa kwa miaka 99, lakini hoja yake iko kwenye visiwa ambavyo vinakaliwa na watu.

Akifafanua maelezo hayo baada ya kupigiwa simu na Mwananchi, Saleh alisema: “Visiwa ambavyo havina watu, mimi niko okay (sina tatizo navyo), isipokuwa kisiwa cha Misali. Hoja yangu kwenye kisiwa cha Misali ni sehemu nzuri, ni kama Ngorongoro ya baharini, ni kama Loliondo ya baharini, jinsi kilivyo na rasilimali.’’

Saleh aliongeza kwamba ukijenga hoteli kwenye kisiwa hicho, maana yake shughuli za kibinadamu zitaongezeka na hatimaye matumbawe yatakatwa, samaki watakimbia na mazalia ya samaki yatatoweka.

Chanzo: MWANANCHI
Mradi muwe makini tu. Msijikute mnakosa hata pa kutemea mate. Mchanga wa kujengea tayari mnachukua huku bara.

Msisitizo
Kuweni makini
 
Mwekezaji atachukua ardhi kwa miaka 99,
DUH!!!
Hapa nilipo nina miaka 26 Ila nikucheki urefu wa muda nilioshi na madiliko ya kimazingira na ongezeko la watu ndani ya miaka hiyo 26 ni makubwa sana , Je vp kwa miaka 99
 
Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi ametema nyongo kuhusu mambo saba aliyosema yamekuwa yakipotoshwa kwa makusudi ili kumkatisha tamaa, lakini akasisitiza kuwa hatarudi nyuma hata hatua moja.

Dk Mwinyi alitoa kauli hiyo jana, wakati akizungumza na waandishi wa habari katika utaratibu wake wa kuzungumza nao kila mwisho wa mwezi, huku akitaja makundi matatu yanayofanya upotoshaji huo.

Eneo la kwanza lililotajwa na Rais Mwinyi akisema linapotoshwa, ni ukodishwaji wa visiwa akisema jambo hilo limekuwa likisemwa tofauti na uhalisia.

“Serikali imeamua kukodisha visiwa vidogo 52 na mpaka sasa tayari visiwa 10 vimeshapata wawekezaji, lakini watu wanapotosha kwamba Serikali imeuza visiwa hivyo, jambo ambalo halina uhalisia,” alisema

Aliongeza; “Uhalisia ni kwamba tumewekeza kwa kuangalia uwezo wa mwekezaji, kiasi atakachotanguliza kwa Serikali na kiasi cha mtaji alionao. Na kuweka sawa ukodishwaji wa visiwa haujaanza kwenye Serikali hii, sema sisi tumeboresha zaidi na wananchi watanufaika,” alisema.

Ufafanuzi huo wa Dk Mwinyi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, umekuja kufuatia mjadala miongoni mwa Wazanzibari, akiwamo aliyekuwa kada maarufu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Baraka Shamte, ambaye hivi karibuni alionekana katika kipande cha video akimtuhumu Rais huyo kwa mambo mbalimbali, ikiwamo ukodishwaji wa visiwa. Hata hivyo, siku chache baadaye, Shamte aliomba radhi kwa kauli alizotoa dhidi ya Rais.

Sula la ukodishwaji wa visiwa, pia liliwahi kuelezwa na mbunge wa zamani wa Malindi, Ally Saleh katika ukurasa wake wa Facebook, akisema hana shida na suala la ukodishwaji wa visiwa kwa miaka 99, lakini hoja yake iko kwenye visiwa ambavyo vinakaliwa na watu.

Akifafanua maelezo hayo baada ya kupigiwa simu na Mwananchi, Saleh alisema: “Visiwa ambavyo havina watu, mimi niko okay (sina tatizo navyo), isipokuwa kisiwa cha Misali. Hoja yangu kwenye kisiwa cha Misali ni sehemu nzuri, ni kama Ngorongoro ya baharini, ni kama Loliondo ya baharini, jinsi kilivyo na rasilimali.’’

Saleh aliongeza kwamba ukijenga hoteli kwenye kisiwa hicho, maana yake shughuli za kibinadamu zitaongezeka na hatimaye matumbawe yatakatwa, samaki watakimbia na mazalia ya samaki yatatoweka.

Chanzo: MWANANCHI
Miaka 95 ameuza sio kukodisha hiyo miaka ikiisha ata yeye hatakuwep tn.,
 
Back
Top Bottom