Serikali ya Marekani yakiri kuwa na madeni, yaahidi kulipa, wapinzani wasema kiwango cha kukopa kinatia wasiwasi

Serikali ya Marekani yakiri kuwa na madeni, yaahidi kulipa, wapinzani wasema kiwango cha kukopa kinatia wasiwasi

benzemah

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2014
Posts
1,533
Reaction score
3,187
Rais wa Marekani, Joe Biden amejaribu kuwahakikishia Viongozi wa Ulimwengu kuwa Marekani haitoshindwa kulipa deni lake licha ya kiwingu kinachogubika mazungumzo ya kuongeza ukomo wa Serikali yake kukopa.

Akiongea kabla ya kukutana na Viongozi wa kundi la Mataifa manne linalofahamika kama QUAD pembezoni mwa mkutano wa G7 huko Hiroshima nchini Japan, Biden amesema hakuna sababu ya ulimwengu kuwa na wasiwasi juu ya deni la Marekani.

Amesema anaamini mazungumzo yanayoendelea kati yake na Wabunge wa Republican yatazaa matunda huku akitolea mfano kuwa duru ya pili na ya tatu ya mazungumzo hayo yamepata mafanikio fulani ya kutia moyo.

Serikali ya Biden inatanga kuongeza uwezo wake wa kukopa kufikia dola Trilioni 31.4 lakini Wabunge kutoka Chama cha Republican wanapinga mapendekezo hayo kwa hoja kwamba deni la Nchi hiyo tayari limefikia kiwango cha kutia wasiwasi.
 
Ujue hata China nayo inadaiwa deni kubwa tu
 
Mo akisema adaiwa na mkulima kutoka mchambawima akasema anadaiwa! Sijui kwa akili ya kawaida utajua mwenye shida ya pesa ni nani kati yao hao wawili.
 
Rais wa Marekani, Joe Biden amejaribu kuwahakikishia Viongozi wa Ulimwengu kuwa Marekani haitoshindwa kulipa deni lake licha ya kiwingu kinachogubika mazungumzo ya kuongeza ukomo wa Serikali yake kukopa.

Akiongea kabla ya kukutana na Viongozi wa kundi la Mataifa manne linalofahamika kama QUAD pembezoni mwa mkutano wa G7 huko Hiroshima nchini Japan, Biden amesema hakuna sababu ya ulimwengu kuwa na wasiwasi juu ya deni la Marekani.

Amesema anaamini mazungumzo yanayoendelea kati yake na Wabunge wa Republican yatazaa matunda huku akitolea mfano kuwa duru ya pili na ya tatu ya mazungumzo hayo yamepata mafanikio fulani ya kutia moyo.

Serikali ya Biden inatanga kuongeza uwezo wake wa kukopa kufikia dola Trilioni 31.4 lakini Wabunge kutoka Chama cha Republican wanapinga mapendekezo hayo kwa hoja kwamba deni la Nchi hiyo tayari limefikia kiwango cha kutia wasiwasi.
Kwani hayo madeni analipwa nani?
 
Back
Top Bottom