Serikali ya Mzee Jommo Kenyatta inahusishwaje na kifo cha Dk Barack Hussein Obama?

kbm

JF-Expert Member
Joined
Oct 5, 2012
Posts
5,224
Reaction score
1,677
Dk Barack Hussein Obama, Sir.

"Obama anaipenda Afrika, ni bara alilozaliwa baba yake mzazi, Dk Barack Hussein Obama, Sir. Baba yake alikufa katika ajali ya gari Nairobi, ni baada ya kuandamwa na mfumo wa Serikali ya Mzee Jommo Kenyatta, kwa vile tu, babayake Obama alikuwa anafikiri tofauti na watawala.
Baba yake Obama alikuwa rafiki wakaribu sana wa Tom Mboya aliyeuawa katika mazingira ya kutatanisha. Inaaminika, aliuawa kwa vile alifikiri tofauti na watawala, baba yake Obama inadaiwa alikuwa ana siri juu ya kifo cha Mboya. Obama anazijua vizuri siasa za Afrika."

Source: MCL
 
Kwhyo kama mwaikyusa alivyojua i$$ue ya balali....Team Mafioso
 
Hii hudhihirisha ukweli juu ya kifo cha huyo muheshimiwa, na ndio maana hata president obama wa U.S.A. Hua na kigugumizi na utawala wa nchi ya kenya.
 
Tom Mboya,
JM Kariuki,
Barack Hussein Obama Sr,
Robert Ouko...
 
Rubbish!!!
Barack Obama sr. was killed by his own recklesness, driving while drunk. Aliaga mnamo mwaka wa 1982, miaka minne baada ya Jomo Kenyatta kuondoka madarakani.
Ni hiyo haikuwa mara yake ya kwanza kuhusika katika ajali ya aina hiyo, aliwahi kukanywa mara nyingi asiendeshe gari akiwa amelewa, akawa anakaidi.

Hakuuliwa na mtu yeyote, hizo taarifa za OP ni uvumi zisizo na msingi wowote.
 
Sijui Jomo Kenyatta alimuuaje Barrack Hussein Obama Snr wakati yeye mwenyewe alikuwa tayari ni mwendazake. Au ni ile sayansi ya kiafrika? Siwaelewi.
 
Sijui Jomo Kenyatta alimuuaje Barrack Hussein Obama Snr wakati yeye mwenyewe alikuwa tayari ni mwendazake. Au ni ile sayansi ya kiafrika? Siwaelewi.

Huwa siwaelewi Watanzania, wanapenda kujadili siasa za Kenya bila kuzifanyia utafiti, marehemu babake Obama ameaga dunia miaka kadhaa baada ya kifo cha Kenyatta, yaani ni kama Kenyatta alifufuka akamuua halafu akarudi kaburini.
 
Huwa siwaelewi Watanzania, wanapenda kujadili siasa za Kenya bila kuzifanyia utafiti, marehemu babake Obama ameaga dunia miaka kadhaa baada ya kifo cha Kenyatta, yaani ni kama Kenyatta alifufuka akamuua halafu akarudi kaburini.
Kuna mtu ana bifu zake na U.Kenyatta ndo maana anakurupuka na kumtaja babake. Waambie sio Uhuru ndo aliyemualika Tundu Lissu Kenya. Wao wenyewe wanajua vizuri kilichomfanya aje Kenya.
 
Wakenya nadhani watakua wanafahamu ukweli dhahili juu ya hili....


Wakenya mkuje hapa mtupe ukweli wa jambo
 
Tatizo LA Elimu ya kukariri....someni vitabu sio mnakimbilia past papers ...j3 uwahi shule sawa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…