Serikali ya wanafunzi DIT yapinga matokeo ya supplementary

Serikali ya wanafunzi DIT yapinga matokeo ya supplementary

A JUSTMAN

JF-Expert Member
Joined
Oct 5, 2012
Posts
439
Reaction score
555
Matokeo ya mitihani ya supplementary yalotolewa tar.17 jumatano iliyopita yanapingwa vikali na serikali ya wanafunzi 'Dar es salaam Institute of Technology Student Organization-DITSO.

Kupitia barua iliyoandikwa tar.18 juzi inayoelekezwa bodi ya chuo haiyatambui matokeo hayo yalotolewa bila kusainiwa na DITSO, na inadai dhuluma imetumika ili kufelisha wengi walongoza mgomo kupigania wanafunzi walozuiwa kufanya mitihani FE kwa kutokamilisha registration. Haijafahamika DITSO itachukua hatua ipi.
 
Naomba mods tafadhari mhamishie huu uzi jukwaa la siasa kwa kuwa utawala mbovu usiojali elimu bora, haujali taasisi hizi nyeti za kielimu zinaendeshwa kwa utaratibu upi.

Tazama elimu mbovu wanayopata vijana hivi sasa itawakomboa vipi kifikra na maisha kwa ujumla?

Wengi wanafeli na wasiofeli hupata bora elimu 'elimu vyeti' sio ujuzi na maarifa. Hapa siasa inahusika kwa utawala wa nchi kuwa mbovu ndio mana naomba iende jukwaa la siasa.
 
hayo ndo matokeo yenu sasa lawama za nini? ukipanda bangi utavuna bangi...
Sio kweli, mwaka ambao uongozi wa wanafunzi umepigania wanafunzi waliozuiliwa kufanya mtihani kwa madai ya kutolipa ada kwa wakati ( kitu ambacho hakikua kweli) hadi wakafanya, mwaka huo huo matokeo ndo yawe mabaya haiwezekeni uwalaumu wanafanzi kuwa ni wamefeli tu, kuna kitu zaidi ya hicho hapo.

Iko wazi uongozi wa chuo utafanya lolote kuwa-eliminate viongozi wa DITSO.
 
chuo kikiwashika kwenye academic level hakuna kuchomoka tena hapo..hata waende kwa raisi....hauwezi kupanda mahindi uka expect kuvuna maharage
 
Nachofahamu ni hivi ukifeli na wewe unahakika mtihani umejibu kwa usahihi, hapo unahaki ya kukata rufaa na mtihani ule utarudiwa kusahishwa kwa mara nyingine na mwalimu tofauti. Pia mwanafunzi yuko na haki ya kufungua mashtaka mbele ya mahakama.

Jamaa katika kutafuta haki msikie Martin King JR alisema "every step towards the goal of justice requires SACRIFICE, SUFFERING and STRUGGLE the tireless exertion and passionate concern of dedicated individual". Mie nimemnukuu tu hapo.
 
achene siasa mbona wengine tometoka tena kwa CLEAN SHEET bila kwend 120(suppimentary) na pepa ilikua moja, na tuliandamana wote.

Tuwaombee kwa Mungu waliodakwa mara a pili watoke katika Retake zao. OVA
 
Back
Top Bottom