Serikali ya Wezi, Taifa la Waliodanganywa by Jay Alchemist

Serikali ya Wezi, Taifa la Waliodanganywa by Jay Alchemist

Jaya_lchemist

Senior Member
Joined
Oct 12, 2022
Posts
123
Reaction score
207

Serikali ya Wezi, Taifa la Waliodanganywa S01 Episodi 01​

*********

Ni Alfajiri hapa Mwiki,Kasarani jijini Nairobi. Alfajiri hii ni kama zile alfajiri nyingine nyingi za mwaka. Alfajiri hii haifanani na zile alfajiri za mwezi Julai. Julai, mwezi ule kila mtu analalamika kuwa baridi kawa baridi. Eti baridi sasa maana yake kamili inajulikana mwezi huu. Sasa maana ya alfajiri kujiri inaonekana na kushuhudiwa na kila mwenyeji hapa. Nimetumia neno mwenyeji kwa sababu mimi mgeni hapa. Ninashuhudia wenyeji wafanyabiashara wakianza kuzifungua biashara zao, huyu anatoa karai kutoka ndani ya duka anaiweka nje juu ya display yake, huyu anawasha jiko la makaa hapa ile ayaweke mafuta ya mandazi yaanze kuyeyuka ile ayachome maandazi. Yule naye kachukua mkokoteni anaanza kuuvuta kana kwamba ataishi kuuvuta milele daima- la wacha niseme hata wakati ule Mwokozi Yesu atarudi kuchukua Wacha Mwana na Mungu Mkuu.

Uchangamfu ndio unaotawala eneo hili. Kisa? Siku ikianza ni dalili ya jambo jema kutendeka. Wateja kuja, wateja kuleta wateja wengine, labda ule kiongozi wetu Mtukufu Rais Ruto atasusha gharama ya maisha. Lakini kwangu mimi naona hii ni ndoto. Naam zile ndoto tunajilazimisha kuamini zitatendeka ilhali dalili zote zinapinga ndoto kuwa kweli. Kwa nini niseme ni ndoto? Kwa nini nisiamini katika ndoto za wafanyabiashara kuwa Rais atabadilika? Abadilike vipi na tabia ni ngozi. Ameishi kuwa hivi toka enzi za Rais Moi. Wao walikuwa ndugu wa toka nitoke. Mwalimu na mwanafunzi wake, mwizi mahiri akimfunza mwanafunzi wake kanuni na taratibu za wizi. Naona ukijiuliza kwani wizi una kanuni na taratibu kama zile za nchi, zile za katiba ile ya 2010? Naam wizi una kanuni zake na taratibu. Ungekuwa wizi vipi bila kanuni. Tungemtambua vipi mwizi hodari na yule ambaye wizi aliuanza juzi. Huyu hodari anamwiba mama aliye na mtoto hadharani bila aibu. Anamtazama mtoto mdogo aliye mgongoni mwa mamaye anavyolia. Anageuza macho yake kwa mamaye na kuongeza uzito wa sauti yake,” Mama mtoto leta simu na cash uliyo nayo.” Mama anadondokwa na machozi, kitoto kama kinachojua mamaye ananyanyaswa kinaongeza nguvu na sauti ya kilio. Hili litamfanya pwagu au tumwite pwaguzi apate hata tone la hurume? Kama anayetupa jibu la swali letu, anatumbukiza mkono mfukoni wa jeans yake iliyochapa. Mkono unatoka ukiwa umenasa jisu lililojaa kutu. Mama anapiga nduru kali, kitoto hakilii sasa kinaomboleza kwa sauti inayoweza kumwamsha Mtukufu Rais wa kwanza wa Taifa kuu la Kenya.” Leta ganji na tenje haraka ama nimchinje mwanao!” Mama anatoa keshi na Smartphone na kumpa mnyama huyu asiye huruma.

Kwa hivyo, wizi ni kama mchezo. Kila mchezo una kanuni zake, kadanda ina kanuni moja kuu- piga pasi ukitumia miguu peke yake, usiutumie mkono au mikono kamwe, voliboli pia, chess vilevile imejaa kanuni. Kwa hivyo mchezaji mahiri wa kadanda ni ule anayezifuata kanuni za kadanda na ameziandika kanuni hizo moyoni. Kuna wale hata baada ya kuzijua kanuni wanazifuata kisha wanaona hawapati matokeo wanayoyapenda. Hili linazaa juhudi za wizi na kusoma mchezo huu kwa undani zaidi. Wanakosa kula, kunywa, kwenda haja ili wajue kuuiba mchezo huu. Mazao ya juhudi zao yataonekana Jumamosi katika mashindano baina ya Timu yao na Timu pinzani. Yetu macho tu,kimya.

Lakini mbona tuishi kimya? Pwagu na pwaguzi, mwizi mahiri na mwanafunzi wake wanaendelea kuishughulikia njaa yao ya utajiri. Baada ya kushiba na kutajwa kwenye orodha ya matajiri nchini na Afrika, hawatosheki. Kama vile mwandishi wangu kipenzi, Ben Ramadhan Mtobwa, anavyosema kuwa hawa baada ya kuikata kiu ya utajiri wanaendelea kuilinda shibe hiyo. Mungu ailaze roho yake pema peponi!

Ama tukae kimya tungoje wakati wa Yesu Kristo, wakati wa Jehova Mungu Mkuu? Huku mimi na wewe tukiomba na kuamini kuwa Shibe Itawamaliza. Lakini mbona tuwaombee mabaya wakati Messia alituasa tuwaombee mema maadui zetu? Hawa ni maadui wetu. Maadui wa Taifa la Kenya. Toka zile enzi za Shujaa Dedan Kimathi alipoikomboa nchi. Toka zile enzi tulimvika urais msaliti aliyeisaliti Maumau. Aliyelisaliti Taifa lake akavikwa Shujaa namba wani. Tukampa zawadi ya kutuongoza aliyewapa wazungu wazungukaji Dedan Kimathi kama kafara. Kwa nini tulifanya hivi? Kwa nini wakenya hawakuelewa kilichoendelea? Wakati wakimkebehi na kumtukana Ndirangu Mau aliyempiga Dedan Kimathi risasi tarehe Octoba 21, 1956, tunampigia makofi yule aliyemsaliti. Hatubaki hapo, tunamvika mwanae msaliti huyu urais. Nielewe, sina ugomvi na mwana mimi. Mimi siamini kuwa mbegu mbaya ya mzazi ina asilimia mia moja ya uweza wa kumdhuru mwana. La! Nimewashuhudia mashetani ya wazazi yakiwazaa malaika wanaomwabudu Jehova na Roho Mtakatifu na Mungu Mwana kwa roho na kweli. Mwana hafai kuadhibiwa makosa ya mzazi. Mimi kamwe sina shida na uongozi wa mwana. Wale wezi mahiri ndio wanaoyoyakereketa maini yangu. Wale bweha waliovaa ngozi ya kondoo. Hata bweha wengine bila aibu, wanaenda kwenye taifa ya wanakondoo na kusimama kandamnasi.”I promise I will be a Vegetarian!” Vegetarian anavikwa uongozi na wanakondoo waliokosa kumcha Jehova na Mwanaye. Waliokosa kumsihi Mwenyezi Mungu awape kiongozi. Kama zile enzi za Daudi, Sauli na Wanaisraeli, Mungu anamchagua kiongozi. Wanaopiga magoti na kumsihi Jehova awape Rais watamwona akiwapa Daudi au Solomoni. Lakini wanataifa wakikosa kumsihi Mungu awape kiongozi, watamchagua Sauli. Wanamchagua vegetarian. Kisa? Alilia mbele yao na kuwapa matumaini na fake promises. Mimi ni rais wa wanyonge. Bottom up!!! Mazao ya maamuzi yao, anazitoa kucha zake akiupata urais. Anaanza kumla kondoo mmoja baada ya mwingine huku akiwa kwenye Telly akiwapa wanakondoo fake promises. Wale wenye hekima watanielewa kwa kina ninachomaanisha sio kondoo wanaomwamini bweha vegetarian mbele yao.

********

Sasa fikra zinarudi kwenye nganya hii ya Kanairo. Haya mawazo yote yaliibuka nilipowaona wafanyabiashara wa kiike kwa kiume wakichapa bizna vilivyo.

Sasa watu wameongezeka kwenye nganya hii. Bikizee sasa ameketi nami sako kwa bako. Viti vilivyo kando yetu vimewahifadhi mtu na mpenziwe. Hawa walianza kwa mzaha. Huyu wa kike akiutalii mwili wa boyfriend wake. Alianza kwa kuviteleza vidole toka kwenye shingo yake. Boyfriend naye kakaa kama ambaye hajaguswa kimahaba na beb wake. Ama hisia zake ziko mbali sana kutoka kwenye ulimwengu wa mahaba ama anaona aibu kujibu mguso wenyewe mbele ya ajuza aliye kando yangu. Binti wa watu hatulii. Anaupeleka mkono kifuani mwa babe. Hapa anakaa kwa sekundi asilimia kumi na tano. Beb naye katulia kama maji mtungini. Msichana hafi moyo aliutelezesha mkono wake hadi kwenye mapaja ya mpenziwe. Jitu sasa limeanza kujibu miguso. Linaanza kumshika msichana wa watu nywele. Knotless braids zinapelekwa mbele, sasa zinalalia kifua cha binti. Anapata nafasi kwenye shingo. Anaulaza mkono hivi kwamba vidole vyote vinne vimemnasa babygal shingoni kwa nyuma. Namtazama ajuza alivyozubaa. Sasa mdomo wa boyfriend unasafiri upatane na wa beb ama tumwite babygal. Binti Sasa ako kwenye dunia yake. Mtego alioutega sasa umefyatuka. Anaanza kuguna. Hapa wacha niseme kama alivyosema Lil Wayne kwenye ngoma itwaayo Corazon: “French kissing like they in Paris.” Ajuza sasa aliwacha kuzubaa. Sasa alianza kutukana:”Vijana wamekosa adabu!” Wapenzi hawasikii ama labda walimsikia lakini wakaamua kumpuuza. Aliona hilo halifanyi kazi sasa alianza kumwomba Mwene Nyaga. Hilo halikutosha, kamnyang’anya binti aliye mbele yetu Mango Delmonte aliyoishika kama washikavyo martini glass ya Cocktail pale kwenye klabu. Kafungua dirisha kaimwaga nje ya nganya. Kasonya alipoona imemwagika kwenye cabro blocks pale kwenye stop ya mat na hizi nganya. Kafyatuka nje kakimbia asilimia mita kumi na tano na kuimwaga Delmonte kwenye mchanga. Kaanza kumwomba Mwene Nyaga.

Binti aliyenyang’anywa Cocktail yake sasa siye binti mpole niliyemwona sasa namwona kageuka kawa kama yule Mitchelle Mjaka Mfine wa TikTok. Kawa kama yale majimama ya coast yanayoamka na kuifunga dera vizuri ili wavamiane kama majichui mawili ya vijike. Baluni ambazo ni kama hazijapulizwa ziliyo kifuani sasa zinaenda mbele nyuma kama ile pendulum ya Physics pale Highschool. Kasi kamwendea bikizee. Watu sasa wanashuka mmoja baada ya mwingine washuhudie. Jeshi ya Nduthi ama tuiite boda sasa wameziamkia nduthi zao waione sinema vizuri. Jimama kando yangu mlangoni mwa nganya linasema “Netflix ni ya bure leo.” Shosh wa watu sasa anaelekea kwamka tabasamu usoni- mababu wametuliza hasira. Kwa hivyo kofi hakulitarajia. Bare lilitua barabara usoni ama kama vile msomi anayeheshimika kijijini angesema the slap has reached ama the kofi has hit shosh vizuri. Msomi sasa anaheshimiwa na wanakijiji. Kizungu kilikuja na meli mwanakijiji aliyesikia hivyo angesema. Kilio kinatamalaki eneo. Jeshi ya boda linamshika Mjaka Mfine na kumvaa kofi. Mbona umpige kofi bikizee kama huyu??
 

Attachments

  • Serikali ya Wezi Article.png
    Serikali ya Wezi Article.png
    782 KB · Views: 4
Mwendelezo ni kila Jumatano na Jumamosi kila wiki. Naitwa Jay Alchemist mwandishi toka Afrika Mashariki. Uongozi wa taifa za Afrika ndio hutufanya waafrika tuwe nyuma. Tunaitwa The Dark Continent. Kisa? Viongozi wetu ni walafi na kama mwandishi wangu kipenzi BEN R MTOBWA alivyoandika: Hawa wanafakamia mali ya umma kwa njaa ile ya umaskini. Baada ya shibe, wanaendelea kufakamia mali ya jamii ili wailinde shibe hiyo. Jiunge nami katika hii safari ya wazalendo wa Afrika. Tusome hii simulizi iitwayo: Serikali ya Wezi, Taifa La Waliodanganywa. Simulizi hii ni sehemu Kijasusi kama ile series ya Joram Kiango ya Ben Mtobwa sehemu ya Kimaisha na sehemu kubwa riwaya kama zile za Ken Walibora
 

Attachments

  • Your paragraph text.png
    Your paragraph text.png
    1.8 MB · Views: 4
Kesho ni Jumatano: endelezo la simulizi yetu yenye utani na uandishi wenye kipaji kama waandishi wetu watukufu wa Afrika Mashariki. Katikati ya saa 6pm-8pm EAT.
Tutamwona binti mwenye mini anavyomtesa fisi mtaani!
 

Attachments

  • Jamii.jpg
    Jamii.jpg
    783.9 KB · Views: 3
Simulizi naiposti hapa saa moja kamili EAT. Lakini endelezo nitakaloposti liko kwenye website yangu already. Bila malipo yoyote, unaclick link hii hapa chini kisha inakupeleka moja kwa moja kwenye simulizi yote. Huko nimezipanga zikiwa kama pages:
Page 1: Serikali ya Wezi, Taifa La Waliodanganywa S01 E01
Page 2: Serikali ya Wezi, Taifa La Waliodanganywa S01 E02
Page 3: Serikali ya Wezi, Taifa La Waliodanganywa S01 E03
Subscribe baada ya kuisoma hapo. Nikiposti kwenye website, unajulishwa moja kwa moja kwenye email yako. Mimi silipishi hata senti. Simulizi nilianza kuiposti sina budi ila niposti hadi the very last season and the very last episode

 

Attachments

  • Jamii.jpg
    Jamii.jpg
    783.9 KB · Views: 4
******

Mjaka Mfine kakaa kitini mle kwenye driver’s cockpit ama niwaige vijana rika langu kuiita sehemu hii, baze ya dere. Kwa hivyo sijui kanuna ama kafanya tabasamu la kuigiza ama la kulazimisha. Hili nalo tunaliita grin ya masponyo. Masponyo mwawajua. Wale wazee ambao huitwa baby na magirlfriends wenu vijana wa kiume. Dem mmoja kaketi umbali wa mita nne toka nilipo. Mini kama hanchifu ndiyo inayojaribu kuyaficha mapaja. Hanchifu haifanikiwi kwa sababu paja moja nene jekundu laini lipo wazi. Sekunde kadhaa, conductor anafika,” Leta ya Kaizari sister!” Sister naye kageukia Gucci Horsebit 1955 card case wallet ya brown.

Hapa napatwa na msisimko nikijaribu kuimagine vile akina Dingo na Ngeta wangeinyakua begi hilo. Dingo angeinyakua toka kwenye mikono hii laini kama sponge bila kutoa hata tone ya nguvu zake. Nikijua vile Ngeta angeisnatch msisimko unageuka na kuwa kicheko. Nakiangua.

Kristo nisamehe! Sifai kucheka kwenye mambo serious kama haya.“Baby stop it. I’ll pay!” Sijui nimwite huyu kiumbe aliye karibu na dem wa hanchifu mzee ama nini. Wacha nikueleze alivyo uniambie kama amepita qualifications za kuitwa mzee. Huyu sio kijana, sio mzee wa makamo! Hii ni sahani ya zamani ambayo imejikunja kama gazeti lililokaa kwa mvua. Ngozi yake ni kama mabati ya mabanda ya kule Korogocho na Dandora, Kanairo. Lakini hizi ni za enzi ya Mpenda Rungu. Hizi enzi za Zakayo, labda tuseme Kibera.

Eti sasa Zakayo kayaona matatizo ya hawa viumbe wasio mbele wala nyuma. Eti kamwona mama watoto ambaye kawachwa na baby wake wa umri usiopungua miaka 60. Sasa kawachiwa familia nzima ya The former President of The Republic of Kenya. Ndiye huyu Jomo Kenyatta, ndiye huyu Jaba Kenyatta ndiye yule Ngina Uhuru.

Lakini hawa nikiwafananisha na kina Ngina nitakufanya uunde picha na kuwaona hawa watoto wa raisi wetu wa 2013-2022 kuwa wana sura zisizovutia. Hasa lile ambalo lingeniumiza moyo ni wewe kumwona Ngina asivyo. Wacha umwone binti wa kipekee wa Uhuru alivyo. Alex Mwai niko tayari unipige mabare kwa kumsifu mkeo. Lakini mbona nisimsifu maumbile yake ya nje na ya ndani? Hapa namkumbuka mwalimu wangu wa Fasihi kule Nyandarua Highschool akitusomea Kigogo hizi enzi za post-corona:

“Kenga anashangaa: Eti urembo wa ndani. Sisi hatutembei na mashine za eksirei aise! Urembo ni wa nje period!

Sitaki hata kufikiria jinsi Dunia ingekuwa kavu bila hawa viumbe kama Ngina. Sasa wewe kwenye akili yako ushaanza kuwaona hawa wa TikTok wanaozichezesha nyash zao ili jidume jinga liwape like na follow. Kisha kwenye live, jidume linamnunulia gift! Kwa kweli kuna mafala kwenye hii dunia! Kama hao ndio unadhani namaanisha, wewe umeongoza kwenye darasa tukianzia nyuma. Wewe kwa ufupi, ni mvuta mkia.

Kama Dunia ni bustani, basi Ngina Uhuru ni waridi lililonyunyizwa na mvua ya kwanza ya asubuhi. Uso wake ni mwanga wa alfajiri, mwenye macho yenye utulivu wa Bahari Hindi na tabasamu lake halivunjiki hata tetemeko la ardhi!

Mwendo wake ni wa heshima sio wa mabibi ya Kongowea Market yakiwinda punguzo. Hapana! Anatembea kwa mpangilio wa muziki wa Tungamira wa The Unveiled toka pale Zibambwe, harmonies zipo asilimia tisini na tisa nukta tisa tisa…. Kila symphony ni ya busara. Sketi yake inakumbatia upepo kwa ustaarabu ikivuka magoti kwa heshima sio zile za hawa Tiktokers wanaopendwa na vijidume vya Afrika Mashariki. Nilikuwa mojawapo ya vijidume hivi lakini neno la Baba humbadili shetani anawa malaika nayo Dunia na miili yetu vilevile yaweza kumgeuza malaika kuwa shetani. Kama huamini haya, mtazame Lucifer aliyekuwa bila hata tone la dhambi. Sasa hivi yeye ndiye mfalme wa dhambi na giza! Nina uhakika asilimia mia moja hata wewe kijana umetamani haya manyama ya TikTok. Mwone Njoki Murira anavyotikisa makalio kama ng’ombe wa shamba wakikimbia. Huyu anajua kuyatumia manyama yake kama silaha. Wewe ukiona hivi mashetani yote yanaamka. Mwingine bila aibu anasema,”Huyu shoti kadhaa akinipa, manii ya shoti ya mwanzo nitawamwagia mababu! Ili kuwashukuru!” Bila kujua afanyacho, ashaclick follow button pale TikTok, amekimbia IG amemfollow mwenye manyama. Reels za mwenye manyama zinatazamwa takriban masaa manne mfululizo.

******

Sasa mzuka umetulia! Hii ni baada yake kujifungia na kuingia kwenye pron site. Kampata Alicia Kanini akilawitiwa laivu pale mtandaoni. Hapa mzuka unapanda mara mia. “Mtoto kazaliwa!” Anakubali kimoyomoyo.

Kisha anaingia pale Telegram anazitazama habari zinazotrend. Baltasar Ebang Engonga Avomo. Yule mbwamwitu-fisi anayenusa kila mahali kisha anaanza kutenda yasiyosemeka. Sijui kama waafrika wengine ni ujinga uliojaa akilini ama ni kurogwa walirogwa na mababu zao ama ni Mwenyezi Mungu aliwanyima akili kwa sababu ya kujaza maovu moyoni. Ama tuseme ni Ibilisi hawa. Twadhani watu kumbe Ibilisi kafanya incarnation na tunazitazama comments zake pale Fb, X, IG, Whatsapp groups, Telegram Groups hadi wengine wapo Reddit. Wewe unatazama comments uyatie mawazo ya watu kwenye ratiri

“Ninataka mwanaume kama huyu ili anichambue vizuri anifanye nitapetape kama samaki nchini kavu. ” Picha kwenye profile ni ya kitoto cha takriban miaka kumi na tano. Nacho chataka kiongezwe kwenye listi ya wanawake sijui mia nne!! Kitapatape. Kifanye tendo la wanandoa na fisi!


Mbwamwitu-fisi huyu pia bila aibu alifanya mapenzi na mke wa ndugu yake!! Mimi niwe kwenye nafasi ya ndugu yake ningefanyeje? Ungefanyeje? Wewe kama Engonga ungemtazamaje nduguyo machoni tena? Ungewasalimu vipi watoto wa nduguyo wakwitao Uncle. Labda hata wewe ndiwe uliyekuwa role model wao. Sitaki hata kuimagine aibu aliyopitia huyu incarnation ya fisi.
Tufanye utani kidogo. Aliyekuwa Officer wa National Agency ya Financial Investigation kwenye nchi tukufu Equatorial Guinea, alilala na wake wa watu, mabinti na majimama. Wote wakiunganishwa ni wanawake takriban 300-400.
Sasa kwenye nchi ya Germany kuna mji unaoitwa Arnis. Arnis ina watu takriban mia tatu. Sasa inamaana mbwamwitu-fisi wetu tumpendaye wa Afrika alilala na wanawake wote wa Arnis- watoto wachanga, teenagers, mabinti wa umri wa yule Mjaka Mfine, bikizee. Wote.
Usisahau watu wote Arnis inawahesabu pia wanaume. Hapa Engonga nitavuka mipaka kidogo. Nisamehe! Kwa hivyo ina maana mbwamwitu-fisi wetu alilala pia na wanaume wote. Amewalawiti wote. Yaani nikisema hili watu hawashangai!

Mwanaume kulala na mwanaume mwenzake limekuwa jambo la kawaida duniani. Ingia pale YouTube umwone Lil Nas X anavyofanya ngoma chafu zikisifu the LGBTQ+ community. Mwone anavyojigamba kuwa yeye ni gay. Mtazame huyu Diddy anavyotumia Johnson’s Baby Oil kwa wanaume wenzake!
Yatizame magereza yetu hapa Afrika Mashariki: Kamiti Prison. Prison warden anakukaribisha na tabasamu kali, sio la kulazimisha, huku akikwambia utajionea ya Musa! Kijana alikuwa kaamua awe Original Gangster(O.G) ama kaziona ngoma nyingi za 2pac ama yeye ni mpenda nyimbo za Youngboy Never Broke Again.


“Bi***tch I’ll send them hitters to hit at you boy don’t say shi***t to me!” Anasikika akimwiga Kentrell huku kafanya mkono wake umbo la pistol. Kamwua aliye kando yake! Siku yake ya kwanza pale gerezani. Usiku unaingia kwa fujo. Tai wametamalaki eneo la gereza. Giza nalo sio giza la saa tatu. La! Hili ni giza la usiku wa manane. Kwani lajaribu kuficha nini leo? Cell Roomies ama tuwaite homies wake wanaingia kwenye cell yake: Cell 3 Block 1. Curtains zinatolewa vitandani zinafungwa vyema kwenye mianya ambayo ndiyo milango ya gereza. Sasa ni kama leo twarudishwa pale Nyandarua Highschool kutizama tamthilia ya Tumbo Lisiloshiba na Kigogo ikiigizwa!

Ni Tumbo lipi Lisiloshiba? Si ni hawa viongozi wetu wapendwa. Fasihi imeficha haya yote kwenye simulizi. Lakini mimi sifichi lolote. Nimechoka tunavyowafunika hawa fisi tuitao viongozi. Shuka Zakayo shuka ndilo ombi la kila Mkenya. Niko tayari Kasongo awatume DCI wanifuate na Subaru zao! Miili kama ya manguruwe huku suti zilizowatighten. Wanakaa viboko. Niko tayari kwa lolote. Kama mapenzi ya Baba wa Mbinguni ni eti nimalizwe na Zakayo, sina la kuogopa! Kama sio mapenzi yake basi injili hii ya Bwana itaendelea. Injili ya mafisi hawa tuwaitao viongozi lazima ikome!!!!!

Youngboy wetu wa Afrika Mashariki anaangua kilio. Analia kwa nini? Kashurutishwa aokote sabuni iliyoangushwa kimadharau na jisura hili linalochukiza. Litazame lilivyonuna, lione lilivyo na manyama kama hippo, ebu nusa jasho.Yaone makwapa!
Siendelei tena! Hata picha yenyewe sitaki kuivuta zaidi ya hapo.

Kisha pale mtaani unamwona comrade amesubscribe kule Netflix. Anatazama series iitwayo Sex Education akiimaliza anaitazama nyingine: Elite. Sasa series zote amezimaliza na wiki mbili. Muda anaupata wapi? Sasa anajidanganya,”Wacha niwatch Fear Street kiasi nianze kuokoa sem!”
Hapa nitasema wazi. Netflix ndiyo movie Inc. inayokuza mbegu ya LGBTQ+. Mtoto mchanga anayaona majitu mawili ya kiume yakishikana ndevu yakikiss. Kisha unamwona Bishop Mariann Edgar Budde akipiga makofi akisema,“You are now husband and wife!” I can’t bottle up my curiosity,” Who is the husband who is the wife?”

Ama husband-wife atamlipia wife-husband plastic surgery awe wa ‘kike!’ Wife-husband anavaa wigi kama ya Rihanna iitwayo Crown wig. Husband-wife atafanya picha ya Rihanna ikifanya mapenzi na mwanaume mwenzake!

“Kijana leta ya Kaizari!” Nasikia kwa umbali. Naipuuza sauti hii.
Kofi la bega ndilo linalonitoa kwenye ulimwengu wa mawazo.

“Rwabe mkuu!” Naitoa simu yangu ya Neon Ray 2. Nampatia aweke digits.
Wewe! Unajua nimesema digits ukadhani anaiweka contact yake niisave.
Nitakuuliza kama Simon Kaggwa Njala,” Why are you gay?”
M-Pesa message namwonyesha. Transaction fee iliyomezwa, na hawa wenye Tumbo Lisiloshiba ama uwajuavyo Safaricom, inafanya nilalamike kimoyomoyo. Sasa nganya inasimama.

******

Kuna hawa wasichana ambao hutumia maumbile yao ya kiike kutuadhibu sisi wanaume. Hawa huwaumiza wanaume wengi mno. Kwangu mimi huwatazama na kumwambia Mungu,”Huyu ulimuumba akaumbika!”
Lakini ni dhahiri ya kwamba huyu kavaa hivi ili apate fursa ya kutazamwa na wanaume ili wamtamani. Naam, kafanikiwa kwenye lengo lake. Nimemtamani!
Lakini sio kama wanavyomtamani wale wanaume wengine wengi. Mimi ninakubali kimoyomoyo kuwa kaumbika lakini sitamvua mavazi kimachomacho kama mafisi wafanyavyo. Sitamwona kwenye akili nikifanya mapenzi naye kitandani hotelini
. Naam, pia mimi nilikuwa nikifanya haya yote kwenye mawazo. Zile enzi!

Naam. Zile enzi!

Lakini mbona nimvue mtoto wa watu nguo kimoyomoyo? Kisha bila idhini yake nalala naye kitandani cha 6 foot 6 hotelini nikifanya naye mapenzi kama wafanyavyo actors wa pron kwenye akili.
Mbona nisikize sauti yake anavyoongea kisha niiweke sauti hiyo kwenye mizani ya ngono kwenye moyo nikikadiria atakavyolia kitandani ama wasemavyo atakavyomourn kitandani kwa faraja anayoipata?
Hapa utamwona fisi akitabasamu bila sababu lakini sisi tushajua sababu itakayomfanya atabasamu.

Anamwendea binti. “When I saw you I wished I could die if you were not to be in my life!” Mwenye miniskirt anapata faraja iliyopita mizani. Mtego umenasa palipo!
Huku kajifanya halijui lengo la fisi, anauliza kwa macho ya kiwizi,” Why?”
Fisi sasa hatabasamu kwenye uso tu. Sasa tabasamu liko dhahiri machoni, mapuani, masikioni na kote apendako. Sijui ama labda hata tabasamu la level hiyo ni silaha yake pia ama ni furaha ya kikweli. Mwindaji ama mwindwa, sijui nimwiteje anajibu kwa furaha: “Because I see you as my whole world. Everything else in it seems useless.”
Hapa kicheko cha mwenye mini kinamjibu jibu lake mwindaji ama mwindwa.

Yupi mwindaji yupi mwindwa? Fisi kaja kwenye mwenye miniskirt akiwa kajihami na mtego. Mtego una dalili zote za kunasa. Mtoto anatabasamu. Checki tabasamu alilonizawadi kwa pick-up line yangu!
Mwone anavyocheka ni kama kaambiwa the joke of all time na Chally Chaplin ama na Mr Mbilimbili wa pale Tiktok. Mwenye mini skirt naye kajihami na mapaja yanayomeremeta. Mwili unaoshurutisha macho ya kiume kuuona. Nyama laini inayoomba mikono ya kiume kuipapasa na kuimiminya. Nyoyo zinazomlilia. Nyute zinazotoka kwa fuja mdomoni, ishara ya kutamani. Figure 8 nayo iko dhahiri machoni. Hili linayaamsha mashetani ya kila mwanaume. Ona huyu aliye mbele yake. Yeye hajaficha tamanio lake. Kaja kumteka. Kaja kumwingiza box. “Atafanikiwa?”

“Wewe ni mrembo mbele ya warembo wote nilipowaona. Moyo wangu unapiga kasikasi ishara ya mapenzi yangu. Nipe mobile number yako babygal!

Atapewa phone contact ama asemavyo Crazy Kennar atapewa digits? Swali utalijibu mwenyewe baada ya kumwona dem huyu mwenye miniskirt aliyekuwa amesimama hapa kwenye hii stage.
Sijui ni wapi hapa lakini naona kama ni OTC. Nitajua baadaye. Wacha nimtie huyu aliye na mini mizani nimwone kama ni tofauti na wale wengine.
Wale wengine tuwajuao mimi na wewe. Wao ni wapenda senti. Sijui kama ataliendea lile bati zee la Kibera linalolelewa na binti yule anayeimiliki ile porch ya Gucci.
Anamlea kivipi?
Msichana wa watu aliona zee la wenyewe limechoka kukalia kiti hiki kigumu. Kaamua kumfanya mtoto wa miaka miwili.
Sasa jizee limeketi mapajani mwa dada wetu. Mapaja ya msichana wa watu yapo wazi. Hana hata tone la aibu. Kosa! Jizee halijaketi. Limelala. Ninagundua hili baada ya kulisikia likitoa mng’oroto kama ule wa nguruwe. Hili linaota likipata watoto wengi wajaze ulimwengu. Mama yao huyu aliyemkalia. Huyu anayemlea. Huyu afaaye kuitwa mjukuu ama kitukuu wake.

Perfume ndiyo inayoyakata mawazo yangu. Hiyo lazima iwe ni ya Dior. Niliiona pale kwenye website ya Jumia nilipokuwa nikiyafurahisha macho yangu kwa kuvitazama viombo na vidude vinavyonunuliwa na matajiri. Hii hapa wacha niite ile iliyonivutia zaidi. Dior J’adore.

Sasa binti anazipanda stairs za nganya hii bila haraka. Conductor kabaki nyuma aione ngozi ya mapaja vizuri. Aione.
Siyo kuigusa. Niione tu! Pia wewe uione……

Endelezo Jumamosi 4pm-6pm EAT

I can also add you to the Serikali ya Wezi, Taifa la Waliodanganywa Series Whatsapp group. My Business Contact is: +254 79226 5091
 

Attachments

  • Jamii.jpg
    Jamii.jpg
    783.9 KB · Views: 3
Back
Top Bottom