Serikali yaagiza kufumuliwa kwa safu ya utendaji ya MSD kufikia Septemba 30

Serikali yaagiza kufumuliwa kwa safu ya utendaji ya MSD kufikia Septemba 30

Lady Whistledown

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2021
Posts
1,147
Reaction score
2,008
Waziri wa Afya nchini, Ummy Mwalimu ameipa bodi mpya ya wadhamini ya Bohari ya Dawa (MSD)hadi ifikapo September 30 bohari hiyo iwe imebadilishwa kiutendaji na kurudishwa kwa mifumo ya tehama iliyosaidia kudhibiti mianya ya ubadhirifu ndani ya taasisi hiyo.

“Tumeondoa wale wakuu wa Idara lakini sasa badilisheni kama kuna mfanyakazi amekaa kitengo muda mrefu miaka mingi badilisheni. Hapa MSD mnaweza kusema ni mkurugenzi kumbe hata mtu wa chini anayepokea barua anafanya ubadhirifu. Sitaki tuingie tena kwenye masuala ya ubadhirifu”

Mnamo Mei 17, 2022 Wakurugenzi watano wa MSD waliondolewa kwenye nyadhifa zao kwa makosa ya ubadhirifu, yakiwemo yaliyotokana na Ripoti ya Mkaguzi Mkurugenzi wa Hesabu za Serikali (CAG)

Chanzo: Mwananchi
 
Tatizo la mwizi linaanzia juu kushuka chini hivyo ni ngumu sn hata awekwe nani pale bado hata fanya chochote
 
Nakumbuka hata ile ya Tanesco ilifumuliwa lakini bado sijaona la maana, zaidi ya mipango ya kipigaji tu mfano milioni 500/= za kuhamasisha matumizi ya gesi
 
Tatizo la mwizi linaanzia juu kushuka chini hivyo ni ngumu sn hata awekwe nani pale bado hata fanya chochote
Watz wanachembechembe za wizi,kuwabadikisha shurti wafyonzwe damu na wawekewe damu isiyo na chembechembe za wizi🏃
 
Kuna mameneja pale wako zaidi ya miaka 10 kwenye kazi hiyo hiyo hawana tija tena wanaishi pale kwa desturi tu na kugawana nafasi kihisia, pia wapo wengine umri wao wote wako hapo bila ubunifu
 
Mradi matatizo ya MSD yanafahamika patasafishika tuu, vuteni subira! Mahali kama hapo hapahitaji pupa maana hilo ndio tatizo letu, kufanya maamuzi ya haraka haraka na kukubali vimemo mwishowe tatizo linabaki pale pale.
 
Nimependa hapo aliposema waondolewe waliokaa muda mrefu. Hata Mimi ninaafiki waondoke ikiwezekana kuanzia miaka 5 maana hao wanaokaa muda mrefu ndio wazee wa deal halafu wanapiga jungu na fitina kwa wale wanaokwamisha wizi wao.

Wakurugenzi wanakuja na kuondoka wao wapo tu. Ili MSD ikae sawa kunatakiwa baadhi ya watumishi kuondolewa kabisa kwenye mfumo wa MSD ikiwezekana wahamishiwe taasisi au wizara zingine.
 
Back
Top Bottom