mwakani naolewa
Senior Member
- Jul 25, 2024
- 148
- 426
Serikali ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania yaahidi kuunganisha bara la Afrika kwa nishati ya umeme kupitia mradi mkubwa wa usafirishaji umeme unaohusisha ujenzi wa njia za usafirishajiumeme wa msongo wenye kilovoti 400 kutoka iringa hadi Sumbawanga na kuunganisha Tanzania na Zambia {TAZA} pamoja na vituo vya kupoza umeme vya Tagameza, Kisada, Iganjo, Nkemango na Malangalali.
Ameyasema hayo Naibu Waziri mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt Doto Biteko huko Sumbawanga mkoani Rukwa akiweka jiwe la msingi la utekelezaji wa mradi huo kutoka Tunduma hadi Nakonde mpakani mwa Tanzania na Zambia
Aidha Waziri Biteko ametaja miradi mingine inayotekelezwa kua ni umeme wa jua Kishapu(MW150), Malagarasi(MW49.5) na mradi wa gesi asilia lengo likiwa ni kupata umeme wa uhakika.
Ameyasema hayo Naibu Waziri mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt Doto Biteko huko Sumbawanga mkoani Rukwa akiweka jiwe la msingi la utekelezaji wa mradi huo kutoka Tunduma hadi Nakonde mpakani mwa Tanzania na Zambia
Aidha Waziri Biteko ametaja miradi mingine inayotekelezwa kua ni umeme wa jua Kishapu(MW150), Malagarasi(MW49.5) na mradi wa gesi asilia lengo likiwa ni kupata umeme wa uhakika.