kalacha mateo
Senior Member
- Sep 27, 2021
- 119
- 240
Waziri wa Fedha na Mipango Dk Mwigulu Nchemba amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuimarisha sekta binafsi inayoiwezesha nchi kukuza uchumi na kupata maendelo.
Dk Mwigulu aliwaeleza washirika wa kongamano la kodi Dar es Salaam jana kuwa watanzania wanatakiwa kutafakari uhusiano uliopo kati ya kodi na maendeleo ya taifa kwa sababu kuna kulegalega katika kukubali kuwa kuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya kodi na maendeleo ya nchi.
Dk Mwigulu anasema ujenzi wa barabara, madarasa, kituo cha afya, mbolea, maji au umeme au kitu chochote kinachohusiana na masuala ya maendeleo kina uhusiano wa moja kwa moja na kodi na kwamba hata nchi ikikopeshwa marejesho yake yataangalia kodi.
Yoyote atakayeanzisha shughuli za uzalishaji, watendaji wote serikalini wanatakiwa wamkimbilie baada ya kumkatisha tamaa. Watu milioni moja wanaingia kwenye soko la ajira kila mwaka kutoka shuleni na vyuoni hivyo Taifa linahitaji sekta binafsi imara ili kuongeza wigo wa walipa kodi.
Dk Mwigulu aliwaeleza washirika wa kongamano la kodi Dar es Salaam jana kuwa watanzania wanatakiwa kutafakari uhusiano uliopo kati ya kodi na maendeleo ya taifa kwa sababu kuna kulegalega katika kukubali kuwa kuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya kodi na maendeleo ya nchi.
Dk Mwigulu anasema ujenzi wa barabara, madarasa, kituo cha afya, mbolea, maji au umeme au kitu chochote kinachohusiana na masuala ya maendeleo kina uhusiano wa moja kwa moja na kodi na kwamba hata nchi ikikopeshwa marejesho yake yataangalia kodi.
Yoyote atakayeanzisha shughuli za uzalishaji, watendaji wote serikalini wanatakiwa wamkimbilie baada ya kumkatisha tamaa. Watu milioni moja wanaingia kwenye soko la ajira kila mwaka kutoka shuleni na vyuoni hivyo Taifa linahitaji sekta binafsi imara ili kuongeza wigo wa walipa kodi.