Cute Wife
JF-Expert Member
- Nov 17, 2023
- 1,906
- 5,000
Wakuu,
Haya maelezo yanatishia mashaka, kwamba wanafunzi hawakai chini ila walikuwa wanafanya masahihisho ya mitihani, tena chini ya mti, kama vyumba vinawatosha kwanini wasifanyie hayo darasani? Hapa panatia mashaka.
Ila pia mnataka kutuambia kuwa THRDC walikurupuka, kwamba hawakuwa na taarifa sahihi hawakaja tululisha kachumbari huku?
Lakini pia historia inawaangusha, si tulishuhudia mlivyohenyesha mwandishi wa habari wa habari aliyepiga picha kwenye shule iliyopo Mbeya, ambao nao walikuwa wakikaa chini, kama sikosei jambo lilifika mpaka kwa Waziri Mkuu?
Kama stori hiyo ilikupita soma hapa:
- Mbeya: Mwalimu aliyesambaza picha za Wanafunzi wamekaa chini, aingia matatani
- Mwalimu wa field aliyesambaza picha za watoto wamekaa chini kufukuzwa (uhaba wa madawati)
Halafu mnatupanga hapa kwamba mko open kuwaacha waandishi wa habari wafanye kazi yao bila bugudha?
=====
Kumekuwa na taarifa inayosambaa kwenye mitandai ya kijamii kuhusu Mkuu wa Wilaya ya Ubungo kumkamata mwandishi wa habari ambaye pia ni Mhariri wa biashara na Mkuu wa Kitengo cha Mtandao (digital) Ndugu Dickson Ng’hily kutoka gazeti la The Guardian.
Taarifa hiyo imeeleza pia mwandishi huyo alipigwa sana na kuumizwa kwenye mkono na simu yake kuvunjiwa kioo huku sababu ikielezwa kuwa ni kupiga picha wanafunzi wa shule ya msingi Kwembe waliokuwa wanasoma chini ya mti. Taarifa hiyo iliendelea kueleza kuwa mwandishi hiyo alipelekwa ofisi ya Serikali ya Mtaa na baadaye kushikiliwa katika ofisi ya Mkuu wa Wilya ya Ubungo.
Kupata mwanzo wa stori hii soma: Mwandishi wa Habari wa The Guardian anadai amepigwa na Walimu baada ya kupiga picha Wanafunzi wakisoma chini ya miti
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo anapenda kukanisha taarifa hiyo iliyoleta taharuki kwa wananchi na waandishi wa habari. Ukweli ni kwamba mwandishi huyo hakupingwa na mtu yeyote isipokuwa aliulizwa na Mwalimu Mkuu kwa nini anapiga picha bila ridhaa yao wala kujitambulisha.
Baada ya mwandishi huyo kukataa kutoa ushirikiano alipelekwa ofisi ya Serikali ya Mtaa na baadaye akapelekwa ofisi ya Mkuu wa Wilaya kwaajili ya kujiridhisha kama kweli ni mwandishi na ana kibali cha kufanya kazi hiyo.
Kupata tamko la THRDC kukemea kitendo hicho soma: THRDC yakemea Mwandishi wa Habari kukamatwa kwa kupiga picha Wanafunzi wa Shule ya Msingi Kwembe wakisoma chini ya mti
Hata hivyo leo Julai 10, 2024, Mhe. Mkuu wa Wilaya alikuwa kwenye ziara ya Waziri wa Mambo ya Ndani kwaajili ya kusikiliza kero za wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kata ya Mburahati na hivyo hakuhusika wala kutoa amri yoyote kuhusu kukamatwa kwa mwandishi huyo.
Aidha, ni kweli kuwa wanafundi walikuwa nje ya madarasa yao kwaajili ya progeamu maalum ya kufanya masahihisho ya mitihani wa Utamilifu (mock) Mkoa, hivyo kimsingi shule haina wanafunzi wanaosomea nje kwa kukosa madarasa.
Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo inathamini na kutoa ushirikiano kwa waandishi wa habari katika kufanikisha kazi yao muhimu ya kuhabarisha umma juu ya shughuli mbalimbali za maendeleo. Hata hivyo, ni muhimu waandishi wa habari kufanya kazi kwa kuzingatia Sheria, Kanuni, taratibu na miongozo katika kutimiza haki yao ya kutafuta, kuchakata na kusambaza habari.
Pia soma:
Haya maelezo yanatishia mashaka, kwamba wanafunzi hawakai chini ila walikuwa wanafanya masahihisho ya mitihani, tena chini ya mti, kama vyumba vinawatosha kwanini wasifanyie hayo darasani? Hapa panatia mashaka.
Ila pia mnataka kutuambia kuwa THRDC walikurupuka, kwamba hawakuwa na taarifa sahihi hawakaja tululisha kachumbari huku?
Lakini pia historia inawaangusha, si tulishuhudia mlivyohenyesha mwandishi wa habari wa habari aliyepiga picha kwenye shule iliyopo Mbeya, ambao nao walikuwa wakikaa chini, kama sikosei jambo lilifika mpaka kwa Waziri Mkuu?
Kama stori hiyo ilikupita soma hapa:
- Mbeya: Mwalimu aliyesambaza picha za Wanafunzi wamekaa chini, aingia matatani
- Mwalimu wa field aliyesambaza picha za watoto wamekaa chini kufukuzwa (uhaba wa madawati)
Halafu mnatupanga hapa kwamba mko open kuwaacha waandishi wa habari wafanye kazi yao bila bugudha?
=====
KUKANUSHA TAARIFA YA KUKAMATWA KWA MWANDISHI DICKSON NG’HILY NA MKUU WA WILAYA YA UBUNGO
Kumekuwa na taarifa inayosambaa kwenye mitandai ya kijamii kuhusu Mkuu wa Wilaya ya Ubungo kumkamata mwandishi wa habari ambaye pia ni Mhariri wa biashara na Mkuu wa Kitengo cha Mtandao (digital) Ndugu Dickson Ng’hily kutoka gazeti la The Guardian.
Taarifa hiyo imeeleza pia mwandishi huyo alipigwa sana na kuumizwa kwenye mkono na simu yake kuvunjiwa kioo huku sababu ikielezwa kuwa ni kupiga picha wanafunzi wa shule ya msingi Kwembe waliokuwa wanasoma chini ya mti. Taarifa hiyo iliendelea kueleza kuwa mwandishi hiyo alipelekwa ofisi ya Serikali ya Mtaa na baadaye kushikiliwa katika ofisi ya Mkuu wa Wilya ya Ubungo.
Kupata mwanzo wa stori hii soma: Mwandishi wa Habari wa The Guardian anadai amepigwa na Walimu baada ya kupiga picha Wanafunzi wakisoma chini ya miti
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo anapenda kukanisha taarifa hiyo iliyoleta taharuki kwa wananchi na waandishi wa habari. Ukweli ni kwamba mwandishi huyo hakupingwa na mtu yeyote isipokuwa aliulizwa na Mwalimu Mkuu kwa nini anapiga picha bila ridhaa yao wala kujitambulisha.
Baada ya mwandishi huyo kukataa kutoa ushirikiano alipelekwa ofisi ya Serikali ya Mtaa na baadaye akapelekwa ofisi ya Mkuu wa Wilaya kwaajili ya kujiridhisha kama kweli ni mwandishi na ana kibali cha kufanya kazi hiyo.
Kupata tamko la THRDC kukemea kitendo hicho soma: THRDC yakemea Mwandishi wa Habari kukamatwa kwa kupiga picha Wanafunzi wa Shule ya Msingi Kwembe wakisoma chini ya mti
Hata hivyo leo Julai 10, 2024, Mhe. Mkuu wa Wilaya alikuwa kwenye ziara ya Waziri wa Mambo ya Ndani kwaajili ya kusikiliza kero za wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kata ya Mburahati na hivyo hakuhusika wala kutoa amri yoyote kuhusu kukamatwa kwa mwandishi huyo.
Aidha, ni kweli kuwa wanafundi walikuwa nje ya madarasa yao kwaajili ya progeamu maalum ya kufanya masahihisho ya mitihani wa Utamilifu (mock) Mkoa, hivyo kimsingi shule haina wanafunzi wanaosomea nje kwa kukosa madarasa.
Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo inathamini na kutoa ushirikiano kwa waandishi wa habari katika kufanikisha kazi yao muhimu ya kuhabarisha umma juu ya shughuli mbalimbali za maendeleo. Hata hivyo, ni muhimu waandishi wa habari kufanya kazi kwa kuzingatia Sheria, Kanuni, taratibu na miongozo katika kutimiza haki yao ya kutafuta, kuchakata na kusambaza habari.
Signed
Joina Nzali
KAIMU MKUU WA KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
===Joina Nzali
KAIMU MKUU WA KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
Pia soma: