#COVID19 Serikali yaondoa ulazima wa kuvaa barakoa

#COVID19 Serikali yaondoa ulazima wa kuvaa barakoa

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2021
Posts
577
Reaction score
2,595
Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amesema kuwa Serikali imeondoa ulazima wa kuvaa barakoa isipokuwa pale inapobidi, mfano kwa wale wenye magojwa ya mfumo wa hewa na kwenye mikusanyiko ya ndani.

Hii inatokana na kupungua kwa maambukizi ya ugonjwa wa UVIKO-19 nchini na Duniani kote.

Kulingana na mwenendo huu, Serikali imeamua kufanya yafuatayo;
  • Kuendelea kuelimisha na kuhamasisha wananchi kupata chanjo ya UVIKO-19
  • Kuendelea kufanya uchunguzi wa afya dhidi ya magonjwa ya milipuko kwa wasafiri wa kimataifa katika viwanja ya ndege vya kimataifa, bandari na mipaka ya chi kavu. Aidha, matumizi ya vipimajoto (thermoscans) kuchunguza COVID-19 kwa wasafiri hao yamesitishwa.
  • Kusitisha kufanya kipimo cha haraka (Rapid Test) kwa wasafiri wanaoingia nchini kutoka nchi zote wenye yeti ya chanjo ya UVIKO-19 au cheti cha RT - PCR.
  • Kuongeza umri wa watoto kutoka nje ya nchi wanaotakiwa kusamehewa kupima UVIKO-19 kabla hawajaingia nchini kutoka umri wa miaka 5 (iliyokuwa awali) hadi miaka 12.
  • Kuondoa sharti la kipimo cha RT-PCR kwa madereva wa malori na magari ya abiria yanayoingia nchini kwa waliopata chanjo ya UVIKO-19.
Kwa kuwa ugonjwa bado upo, wananchi wanaombwa kuendelea kufuata afua zote za kujikinga na ugonjwa huu pamoja na kupata chanjo kamili.

Jumla ya visa 35,747 na vifo 808 vimethibika kuwepo nchini tangu kuripotiwa kwa mgonjwa wa kwanza mnamo Machi 2020

Covid.jpg


5AA5E622-E15F-4A50-B5EA-849ACF908229.jpeg
EA27322C-41F8-4CF3-8962-FEA44DEBA0CF.jpeg
 


Taarifa kutoka Wizara ya Afya imesema Serikali imeondoa ulazima wa kuvaa barakoa isipokuwa kwa wenye Magonjwa ya Mfumo wa Hewa na kwenye mikusanyiko ya ndani pale inapobidi

Hatua hii ni kutokana na kupungua kwa maambukizi ya Ugonjwa wa Corona Nchini na Duniani kote

Aidha, Takwimu za Wizara ya Afya zimeonesha kuwa tokea kutangazwa kwa uwepo wa #UVIKO19 nchini Machi 2020 hadi kufikia Septemba 7, 2022, Watu 35,747 walithibitishwa kuugua huku kukiwa na vifo 808
 
Walikuwa wanavaa wao huko kufurahisha mabwenyenye zao ili wapate misaada!
 
Back
Top Bottom