Serikali yaondoa ushuru wa Tsh. 382 kwenye gesi asilia ya magari

Serikali yaondoa ushuru wa Tsh. 382 kwenye gesi asilia ya magari

Wild Flower

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2023
Posts
378
Reaction score
766
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Oran Njeza amesema Serikali imekubali mapendekezo ya wabunge ya kuondoa ushuru ya Sh382 kwenye gesi inayotumika katika magari.

Amesema hayo leo Juni 27,2024 wakati akiwasilisha maoni ya kamati yake kuhusu Muswada wa Sheria ya Fedha ya Mwaka 2024.

Amesema kamati imefikia uamuzi huo kwa kuzingatia kuwa sekta ya gesi bado ni changa na inaendelea kukua taratibu na hadi sasa haijaweza kutumika kikamilifu nchini kutokana na gharama za kufunga mfumo wa kutumia gesi pamoja na uhaba wa vituo vya kujazia gesi.

Pia, soma=> Watumiaji wa gesi asilia kwenye magari wamefikiwa, wawekewa tozo ya 382 kwa kila kilo

===

Serikali imekubali mapendekezo ya wabunge ya kuondoa ushuru ya Sh382 kwenye gesi asilia inayotumika katika magari.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Oran Njeza amesema hayo leo Alhamisi Juni 27,2024 wakati akiwasilisha maoni ya kamati yake kuhusu Muswada wa Sheria ya Fedha ya Mwaka 2024.

Tangu kuanza kwa mjadala ya Bajeti ya Serikali ya mwaka 2024/25, wabunge wamekuwa wakilalamikia kuhusiana na kodi hiyo kuwa inarudisha nyuma jitihada za Watanzania kuingia katika matumizi ya gesi asilia ambayo inapatikana nchini.

Amesema kamati hiyo ilikubaliana na mapendekezo ya Serikali ya kuelekeza mapato ya ziada (windfall profit) kwa ajili ya kutunisha Mfuko wa Barabara.

Hata hivyo, Kamati haikukubaliana na uanzishwaji wa ushuru Sh382 kwa kila kilo ya gesi asilia inayotumika kwenye magari.

Amesema kamati imefikia uamuzi huo kwa kuzingatia kuwa sekta ya gesi bado ni changa na inaendelea kukua taratibu na hadi sasa haijaweza kutumika kikamilifu nchini kutokana na gharama za kufunga mfumo wa kutumia gesi pamoja na uhaba wa vituo vya kujazia gesi.

“Hivyo, Kamati iliishauri Serikali kuondoa pendekezo hili na Serikali iliridhia,” amesema.
 
Serikali imekubali mapendekezo ya wabunge ya kuondoa ushuru ya Sh382 kwenye gesi asilia inayotumika katika magari.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Oran Njeza amesema hayo leo Alhamisi Juni 27,2024 wakati akiwasilisha maoni ya kamati yake kuhusu Muswada wa Sheria ya Fedha ya Mwaka 2024.

Tangu kuanza kwa mjadala ya Bajeti ya Serikali ya mwaka 2024/25, wabunge wamekuwa wakilalamikia kuhusiana na kodi hiyo kuwa inarudisha nyuma jitihada za Watanzania kuingia katika matumizi ya gesi asilia ambayo inapatikana nchini.

Amesema kamati hiyo ilikubaliana na mapendekezo ya Serikali ya kuelekeza mapato ya ziada (windfall profit) kwa ajili ya kutunisha Mfuko wa Barabara.

Hata hivyo, Kamati haikukubaliana na uanzishwaji wa ushuru Sh382 kwa kila kilo ya gesi asilia inayotumika kwenye magari.

Amesema kamati imefikia uamuzi huo kwa kuzingatia kuwa sekta ya gesi bado ni changa na inaendelea kukua taratibu na hadi sasa haijaweza kutumika kikamilifu nchini kutokana na gharama za kufunga mfumo wa kutumia gesi pamoja na uhaba wa vituo vya kujazia gesi.

“Hivyo, Kamati iliishauri Serikali kuondoa pendekezo hili na Serikali iliridhia,” amesema.
 
Waziri wa fedha hatuna ni vile anaongoza Nchi iliyolala haitaki watu wake wawe kwenye kiwango kizuri cha maisha yeye anawaza kukandamiza tu zipo kodi kero nyingi kaziongeza hapo ni vile ni mtu asieshaurika..
 
Ni suala la muda tu!

Hiyo kodi mwakani lazima iongezwe!

Chura kiziwi hana mbinu ya kukusanya kodi ndio maana anaangalia wapi pa kupata hela bila jasho ndio matokeo yake kama hayo.
 
Kwanini chanzo kikuu cha mapato ni kuongeza mzigo wa kodi kwa wananchi?

Kwanini isiwe kubana bajeti ya matumizi ya Serikali, kuachana na manunuzi ya magari ya anasa. Ishafika hadi STN namba ya gari
 
Huu Udokta wa Uchumi wa Mwigulu huwa siuelewi kabisa!, yeye na timu yake wamekosa ubunifu kabisa katika kutafuta vyanzo vya kodi?, qjabu sana
Hii habari ya gesi asilia ni mihemko, no body is serious how to utilize that natural gas labda Mwijage.
Nadhani tutafute Kagame au Museveni na hata Ruto wasimamia gesi asilia yetu. Kwa sababu tumeshindwa totally.
 
Hii habari ya gesi asilia ni mihemko,no body is serious how to utilize that natural gas labda Mwijage.
Nadhani tutafute Kagame,au Museveni na hata Ruto wasimamia gesi asilia yetu.Kwa sababu tumeshindwa totally.
Mbwa wako wengi humu, hivi kabla ya ujio wa bwawa la Nyerere unajua kuwa zaidi ya asilimia 60 ya umeme ilitokana na gesi asilia?
 
Serikali imekubali mapendekezo ya wabunge ya kuondoa ushuru ya Sh382 kwenye gesi asilia inayotumika katika magari.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Oran Njeza amesema hayo leo Alhamisi Juni 27,2024 wakati akiwasilisha maoni ya kamati yake kuhusu Muswada wa Sheria ya Fedha ya Mwaka 2024.

Tangu kuanza kwa mjadala ya Bajeti ya Serikali ya mwaka 2024/25, wabunge wamekuwa wakilalamikia kuhusiana na kodi hiyo kuwa inarudisha nyuma jitihada za Watanzania kuingia katika matumizi ya gesi asilia ambayo inapatikana nchini.

Amesema kamati hiyo ilikubaliana na mapendekezo ya Serikali ya kuelekeza mapato ya ziada (windfall profit) kwa ajili ya kutunisha Mfuko wa Barabara.

Hata hivyo, Kamati haikukubaliana na uanzishwaji wa ushuru Sh382 kwa kila kilo ya gesi asilia inayotumika kwenye magari.

Amesema kamati imefikia uamuzi huo kwa kuzingatia kuwa sekta ya gesi bado ni changa na inaendelea kukua taratibu na hadi sasa haijaweza kutumika kikamilifu nchini kutokana na gharama za kufunga mfumo wa kutumia gesi pamoja na uhaba wa vituo vya kujazia gesi.

“Hivyo, Kamati iliishauri Serikali kuondoa pendekezo hili na Serikali iliridhia,” amesema.
AGIZA GESI YA KUPIKIA HAPOHAPO ULIPO USIONDOKE KAA HAPOHAPO MTAANI KWAKO
Gesi zote zipo: Oryx Gas, Taifa Gas, Manjis Gas, O-Gas, Total Gas, Mihan Gas, na Puma Gas: zote zinapatikana hapo
 
Back
Top Bottom