Serikali yasema inajenga vituo vingine vitatu vya Nishati ya gesi ya magari

Serikali yasema inajenga vituo vingine vitatu vya Nishati ya gesi ya magari

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Naibu.jpg

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti imefanya ziara ya ukaguzi wa miundombinu ya Mradi wa Umeme wa Kinyerezi One ambao pia itatumika katika Mradi wa Reli ya Kisasa ya SGR na kueleza kufurahishwa na maendeleo ya mradi huo, leo Jumatano Desemba 13, 2023.

Akizungumza mara baada ya ukaguzi wa Kamati hiyo, Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga amesema Kamati ilifika eneo hilo kukamilisha ziara ambayo ilianzia Mkoani Morogoro kukagua miundombinu ya umeme ambayo inawezesha mradi wa Reli wa SGR.

Amesema Kamati hiyo imeshauri mambo kadhaa ikiwemo kuongeza na kuchagiza mambo yanayoweza kuboresha Uchumi wa Wananchi, mfano kuwekeza kwenye gesi inayotumika kwenye magari.

Mwenyekiti.jpg

Daniel Sillo
Akifanua zaidi amesema “Wizara kupitia TPDC tayari tuna mkakati huo, tuna vituo vitatu na tunajenga vituo vitatu vingine, tumeingia ubia na sekta binafsi kwa ajili ya uendelezaji wa kujenga vituo vingi zaidi ili Wananchi wapate moyo wa kubadilisha mfumo wa magari yao kuwa ya matumizi ya gesi kwa kuwa watakuwa wanapata gesi kwa wepesi zaidi.

“Tunafahamu kuna changamoto ya foleni kwa wenye magari wanaotumia nishati ya gesi, lakini uwekezaji ambao Serikali inafanya wa kuendelea kuboresha huduma ya nishati ya gesi ili uwe na mazingira rafiki zaidi.”

Ameongeza “Pia Kamati imetushauri taasisi ambazo zina watu zaidi ya 100 waendelee kufungiwa gesi kwenye taasisi zao, hilo tumelipokea na tutalifanyia kazi.”
Neno la Kamati
Akizungumza mara baada ya ukaguzi huo, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Daniel Sillo ambaye pia ni Mbunge wa Babati Vijijini amesema Watanzania wana hamu ya kuona safari za Reli ya SGR zinaanza, hivyo lengo la ziara yao ni kuona maendeleo na hatua zilipofikia.

Amesema “Kamati tumekuja kushuhudia kazi inayofanyika katika chanzo cha umeme unapozalishwa, tumeona Lot 1 (Awamu ya SGR) ya Dar es Salaam hadi Moro imekamilika kwa 100% ikitimua gharama ya Tsh. Bilioni 76.23, eneo linalofuata kutoka Morogoro hadi Dodoma kiasi kilichotumika ni Tsh. Bilioni 97.75 na imefikia 99%, tunaipongeza Serikali kwa hatua hii.”

Naibu Katibu Mkuu
Naye, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Athumani Mbuttuka amesema Wizara ya Nishati kupitia Shirikisha la Umeme Tanzania (TANESCO) imejiandaa kwa ajili ya Mradi wa SGR na ziara hiyo ambayo pia ilihusisha eneo la Msamvu (Morogoro) kabla ya kufika Kinyerezi inalenga kubaini maendeleo ya kazi zilipofikia.
Naibu katibu.jpg

Athumani Mbuttuka

Amesema “Kamati imeridhika na kazi ambayo imefanyika, ziara hii pia imetembelea GASCO ambao ni wasambazaji wa nishati ya gesi kwa ajili ya uzalishaji, wametoa maelekezo ambayo tumeyachukua.

“Wakati huohuo, tumewaelekeza mipango yetu kama Serikali ili kuongeza uzalishaji wa gesi.

“Aidha amesema kuwa Bwawa la Mwalimu Nyerere litakapoanza uzalishaji wa umeme Januari 2024 litaweza kupunguza matumizi ya gesi ambayo itahamishiwa kwenye matumivi ya viwandani.”

Pia, soma;

695912db-bf3d-4cd8-bb40-51f93e4fd0a7.jpg
6bbbcab7-3999-49c6-b0f8-a9b338b8b7f1.jpg
695912db-bf3d-4cd8-bb40-51f93e4fd0a7.jpg
20231213_144106.jpg
20231213_132611.jpg
 
Back
Top Bottom