Serikali yawatelekeza wanafunzi 29 Ukraine

Mkjj, Hizi copy umezituma kwenye vyombo vya habari vinavyotangaza kwa kiswahili duniani?
 
jamani watu wengine nao wanaweza kusaidia mambo haya madogo ama sivyo.. na miye shamba langu huku litakauka...!
 
jamani watu wengine nao wanaweza kusaidia mambo haya madogo ama sivyo.. na miye shamba langu huku litakauka...!

Kazi nzuri Lakini ziko wapi barua walizothibitishiwa na wizara kupewa mikopo na kwamba waende watalipiwa na wajilipie tiketi.Hizo ni za upande mmoja toka kwao na za upande wa wizara au bodi walizopewa hao wanafunzi ziko wapi?
 
hivi hivo tulizozitumia tumezitumia kivipi ndani ya miezi sita.. tunakitu cha kuonesha?
 
Kazi... hivi umesikia kuna barua toka wizarani inayosema "haiwatambui" wanafunzi hao...? hata hivyo usiwe na shaka.. ushahidi unaendelea kukusanywa...
 
hizi thread za ukraine naona sasa zimezidi, moderator ebu ziweke pamoja !!!!

ahsante !!
 
hapana, siyo kwa wakati huu. tumeshaunganisha ile kuu iko hapo juu.. hizi nyingine zinahusu na specific issues. Hii ni ya kujadili ushahidi mtupu.. ile nyingine ya kutaka Msolla ajiuzulu... na ile nyingine ya vijana kushambuliwa. Likiisha hili jambo (kwa uzuri au ubaya) basi wanaweza kuunganisha. Unasemaje?
 
sawa nimekubali hapo mzee !! bila ya shaka mambo yatakuwa shwari kwa wanafunzi.

Mikono juu mkuu !! Nimekuelewa
 
hivi hivo tulizozitumia tumezitumia kivipi ndani ya miezi sita.. tunakitu cha kuonesha?
Wamezitumia kama ifuatavyo Kila kukicha kushindana PM na PRESIDENT Mmoja akienda mkoa huu na mwengine mkoa ule na wote wana wapambe wanaofuatana nao na magari yanachoma mafuta na posho ya kila aliyemo kwenye msafara ,safari za nje PM,president,mawaziri,manaibu mawaziri na wabunge,Kuwaita wakurugenzi wote wa mikoa na wilaya,halmashauri,makatibu tawala wa mikoa na wilaya,wakuu wa mikoa na wilaya kujadili ripoti ya mkaguzi mkuu wa mahesabu wa serikali.Kuwaita wakuu wa mikoa kadhaa kujadili ripoti ya elimu ya mikoa na wanaongozana na wajumbe wa kamati zao za mikoa kuja Dar kumuona waziri mkuu na kila ujumbe unaonwa kwa siku yake, semina elekezi wakurugenzi tena ,wakuu wa mikoa,makatibu wakuu,mawaziri na manaibu mawaziri Kuna mengi tu...ninaweza kukesha huelewi hawataki kukaa maofisini kwasababu kwao kuzunguka ni kutafuta fedha na kuitisha vikao mara kwa mara visivyo vya lazima ni kuwapa posho jamaa zao ambao hawakupata nafasi zenye posho kubwa kubwa na malipo makubwa baada ya uchaguzi.
 
tetesi zinazonifikia ni kuwa serikali ina ukata mkubwa...! why? I don't even want to guess

Hizi pesa walizokopeshwa zilikuwa katika bajeti yake, ukata serikalini hauwezi kuwa sababu ya kutokuwalipia hawa wanafunzi. Kuna mchezo mchafu sana kuhusu swala zima. Kama tunavyoona JK analifahamu vizuri sana swala hili.
 
hii mijadala ya humu saa nyengine inafurahisha kweli.wanafunzi 29 wametelekezwa na serikali basi ndo mawaziri wajiuzulu.mmmmhhh vichekesho! mungu nijaalie niishi sana ili nione mengi.hawa mamilioni ya watanzania hapa nyumbani waliokuwa hawana maji wala umeme,na hawajui jioni watakula nini wala watalala wapi? wao serikali isijiuzulu,nimeamini sasa kuwa ukiwa nje ya tanzania ndo unathaminiwa .angalau wao wanalala ubalozini hapa tz kuna watu wanalala pembeni ya majaa na uvundo wa minyamafu.sijaona mtu akaanzisha petition hapa kuhusu hilo.hebu namie nende majuu wee nianzishiwe petition yangu.
 
shemzigwa.
hihiiiiiiiiiii najitahidi kufuatilia.naona hapa wanafunzi 29 wanapigiwa debe na ikibidi mawaziri wajiuzulu.am i wrong? wanalala ubalozini mwa uingereza .right? mie mmoja nataka serikali yote ijiuzulu but not for this. nataka ijiuzulu kwasababu mamilioni ya watanzania hawana pa kulala sio kwasababu watanzania wamelala ubalozi wa uingereza.home sweeeeeeeet home.
 
Under Age kama unavyojiita...akili zako hazijakomaa kuweza kuchambua mambo...Kimsingi hao vijana wamekwenda huko na watakuwa ndio wafanyakazi wa kuwasaidia mamilioni ya watanzania wanaopata tabu. Humo tuna madaktari na wataalam wengine ambao watasaidia millions ya watu...na hili la serikali au wazir kuachia madaraka kila ktk uozo watu wanasema...inawezekana waliokutuma wamefanya makosa kukuchagua uje humu kuchangia..
 
Kuna mtu ana-contact ya simu ya hao vijana? kama ipo naomba iwekwe wazi ili mtu yoyote akipata wasaa aweze kuwapigia simu. Baadhi wanahoji kwanini Ukraine?...na ikumbukwe kuwa hata wa UDSM nao walipgiwa Debe...na ikumbukwe kuwa wao wapo ugenini na hawana pa kwenda..tofauti na wale wa UDSM ambao wengi wanandugu au marafiki na nature ya wa-TZ wana ukarimu mno huwezi kuulinganisha na nchi hata ya Kenya....
 
well done chuma. mchango wako ni mzuri lakini na hao mnaowataka wajiuzulu walipokwenda kusoma mlisema watakuja kuwasaidia watanzania wanaopata tabu na sasa mnawataka wajiuzulu.mmmmh !! mambo leo!! kutambua shida ya watu 29 ugenini ukaacha ya mamilioni nyumbani just kwakuwa ni wasomi!! mmmh tulonyimwa nafasi ya kwenda shule kumbe hatuna thamani .! hebu weeeee .shwaaaaaaaaaa.nazama
 

Swadakta! Watanzania siyo wajinga kiasi hicho. Kila siku tunaona watu tuliowasomesha kwa kodi zetu wakikimbilia kwenda kuwahudumia watu wa nchi zingine! Ukiuliza, wanasema etí sie tunawalipa mishahara kiduchu! kwa hiyo hakuna cha kuja kutuhudumia wala nini, wanahangaikia njaa zao tu, basi. Na pia hili ni funzo kwa wengine, kama hamna uwezo, bakini nyumbani. KUlikuwa na zaidi ya hamsini waliopata hizo nafasi, hao wachache ndo wakasema wana uwezo wa nauli, si wajilipie na ya kurudi au walifikiri wataenda baki huko? Tuna watoto kibao wnakufa kila siku bongo kwa kukosa maji safi ya kunywa, vyandarua vya mbu nk.
 

Ibrahim Haruna Lipumba (CUF)………………………………..
Augustino Mrema ( TLP )……………………………….
James Mbatia (NCCR-MAGEUZI)………………………………
Freman Mbowe (CHADEMA )……………………………………
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…