Serikali yaweka ukomo michango kujiunga kidato cha tano. Yaelekeza wanafunzi kutokataliwa kisa michango

Serikali yaweka ukomo michango kujiunga kidato cha tano. Yaelekeza wanafunzi kutokataliwa kisa michango

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
6,067
Reaction score
10,938
Serikali imenuia kupunguza mzigo wa gharama za michango kwa wazazi wa wanafunzi wanaojiunga na masomo ya kidato cha tano. Serikali imeweka ukomo wa michango kuwa Sh80,000 kwa shule za bweni na Sh50,000 kwa shule za kutwa. Hatua hii ni sehemu ya utekelezaji wa sera ya elimu na mafunzo ya mwaka 2014 toleo la 2023, ambayo inalenga kuhakikisha elimu ya awali, msingi na sekondari inatolewa bila ada katika mfumo wa umma.

Naibu Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Zainab Katimba, alieleza kuwa waraka wa elimu namba tatu wa mwaka 2016 unabainisha majukumu ya wadau wote na utaratibu wa kuomba michango. Ili michango yoyote iidhinishwe, ni lazima kupata kibali cha mkuu wa wilaya.

Aidha, Katimba alisisitiza kuwa wanafunzi hawatakiwi kuachwa nyumbani kwa sababu ya kukosa fedha za michango. Alisisitiza kwamba wazazi wanapaswa kuwapeleka watoto wao shule hata kama hawajakamilisha michango. Serikali inajitahidi kuhakikisha kwamba michango inakuwa nafuu na inaratibiwa vizuri ili wazazi na wanafunzi wasikumbwe na mzigo mkubwa wa gharama.

Katika kujibu maswali ya nyongeza kutoka kwa Mbunge wa Konde, Mohamed Said Issa, Katimba alisema kwamba waraka wa elimu unataja aina za michango inayoruhusiwa kuombewa kibali, na akawahimiza wakuu wa shule kuwa na moyo wa uvumilivu kwa wanafunzi ambao hawana uwezo wa kulipa michango hiyo kwa wakati. Hii ni hatua muhimu katika kuhakikisha elimu inapatikana kwa wote bila ubaguzi wa kiuchumi.

Pia soma hoja ya mdau DOKEZO - Wanafunzi wa kidato cha tano kukataliwa kisa hawajamaliza michango ni usumbufu kwa wanaotoka mbali
 
Waache kujizungusha, waseme tu kwamba wametoa bei elekezi ya Ada kwa wanafunzi wanao jiunga A-Level
 
Waache kujizungusha, waseme tu kwamba wametoa bei elekezi ya Ada kwa wanafunzi wanao jiunga A-Level
 
Michango imezidi ada ya Tsh 70,000/= tuliyokuwa tunalipia kwa mwaka.

Tulitegemea michango isizidi Tsh 20,000/= kwa bweni na Tsh 10,000/= kutwa.

Lakini jamaa wamekuja na njia mbadala ya kulipa ada ile ile kwa jina tofauti.
 
Serikali imenuia kupunguza mzigo wa gharama za michango kwa wazazi wa wanafunzi wanaojiunga na masomo ya kidato cha tano. Serikali imeweka ukomo wa michango kuwa Sh80,000 kwa shule za bweni na Sh50,000 kwa shule za kutwa. Hatua hii ni sehemu ya utekelezaji wa sera ya elimu na mafunzo ya mwaka 2014 toleo la 2023, ambayo inalenga kuhakikisha elimu ya awali, msingi na sekondari inatolewa bila ada katika mfumo wa umma.

Naibu Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Zainab Katimba, alieleza kuwa waraka wa elimu namba tatu wa mwaka 2016 unabainisha majukumu ya wadau wote na utaratibu wa kuomba michango. Ili michango yoyote iidhinishwe, ni lazima kupata kibali cha mkuu wa wilaya.

Aidha, Katimba alisisitiza kuwa wanafunzi hawatakiwi kuachwa nyumbani kwa sababu ya kukosa fedha za michango. Alisisitiza kwamba wazazi wanapaswa kuwapeleka watoto wao shule hata kama hawajakamilisha michango. Serikali inajitahidi kuhakikisha kwamba michango inakuwa nafuu na inaratibiwa vizuri ili wazazi na wanafunzi wasikumbwe na mzigo mkubwa wa gharama.

Katika kujibu maswali ya nyongeza kutoka kwa Mbunge wa Konde, Mohamed Said Issa, Katimba alisema kwamba waraka wa elimu unataja aina za michango inayoruhusiwa kuombewa kibali, na akawahimiza wakuu wa shule kuwa na moyo wa uvumilivu kwa wanafunzi ambao hawana uwezo wa kulipa michango hiyo kwa wakati. Hii ni hatua muhimu katika kuhakikisha elimu inapatikana kwa wote bila ubaguzi wa kiuchumi.

Pia soma hoja ya mdau DOKEZO - Wanafunzi wa kidato cha tano kukataliwa kisa hawajamaliza michango ni usumbufu kwa wanaotoka mbali
Ni mchozo wa kuigiza vile.
Yaani baada ya mheshimiwa Lissu kuibua haya mamichango kwenye mikutano yake ndio mnaliona Sasa. Kweli huku kuyumbishana kuelekea chaguzi hizi!!
 
Back
Top Bottom