Service ya gari lililotumika mara tu unapolitia mikononi baada ya kulinunua kutoka nje

Service ya gari lililotumika mara tu unapolitia mikononi baada ya kulinunua kutoka nje

muuza ubuyu

JF-Expert Member
Joined
Nov 23, 2010
Posts
3,539
Reaction score
3,551
Hi JF,
Na imani mmepumzika majumbani kwenu baada ya kutoka church (wakristu) mkimalizia weekend yenu. Kutokana na uzoefu na elimu nzuri itolewayo bure hapa JF na wanaJF waungwana, ningependa kujuzwa yafuatayo;

Kwa kawaida sisi watu wa uchumi wa kawaida huwa tunanunua magari yaliyotumika (mtumba) haswa haswa kutoka japan. Magari haya huwa hatujui mtumiaji alikuwa analitumiaje na hata namna alivyokuwa analifanyia service/alivyo replace vile vitu muhimu. Sasa basi, kutokana na mazingira haya ningependa kujua ni vitu gani vya kuangalia ama kubadili kabisa (hasa gari likiwa above 100,000km) kabla ya kuanza kulitumia!

Katika pita pita zangu humu JF na uzoefu wangu mdogo wa kutumia gari, nimeona ni muhimu kufanya yafuatayo;-
  1. Kumwaga oil engine yote na kusafisha kabisa kwani magari mengine oil yake inakuwa imetumika mda mrefu bila kubadirishwa na hivyo kugandiana huko chini na kuzuia oil kupanda pindi engine inapowashwa.
  2. Oxygen sensor, wataalam wanashauri vitu hivi kubadirishwa ili kusaidia gari lako kutumia mafuta vizuri.
  3. Kubadirisha timing chain na kuangalia belts zote kama bado zipo kwenye ubora. Timing chain ndiyo sababu yangu mimi kuanzisha uzi huu kwani nimeona uzi humu JF unaoongelea kitu hiki kwani kuna mtu amepoteza jamaa yake kwa sababu ya timing chain kukatika na hivyo vitu vyote kugoma kufanya kazi. Na hili ni tatizo kubwa hasa likitokea kwenye magari yetu haya ambayo ni automatic.
  4. Vingine ni kama kucheki break system, steering, ubora wamatairi (usitishwe na upya wa matairi hujui yalikaa store kwa muda gani tangu kutengenezwa kwake, unaweza kuta tayari yalisha expire!)
Mimi siyo fundi, ningependa mafundi waliomo humu JF waje washushe utaalamu wao humu wa vitu vya msingi kuangalia kwenye hii mitumba yetu ya magari pindi tu unapolipokea/linunua kabla ya kuanza kulitumia ili kunusuru uchumi wa familia na nchi kwa ujumla kwani ajali zinapoteza nguvu kazi kubwa.
Lakini pia inasaidia mtu kuchukua hatua za mapema ili aangalie gari lake asilitumie bila service ya maana na hivyo kuliharibu kabisa na hivyo kupoteza pesa alizo save miaka nenda miaka rudi ama kukopa ili aweze kujiokoa katika suala zima la usafiri!

Pia ningependa kujua na gereji gani nzuri na yenye uaminifu kwa hapa mwanza bila kujari gharama zao!!!

Nawasilia 'ubuyu' wangu!
 
jamani tunawasubiri wenye uelewa wa hili jambo kwani nimuhim sana
 
Sijawahi kubadikisha(ga) oxygen sensor..... kuna mwanga nimepata hapa.......
 
Sijawahi kubadikisha(ga) oxygen sensor..... kuna mwanga nimepata hapa.......
Kubadilisha siyo lazima mkuu ila unaweza kwenda kwa mafundi wazuri wenye gereji za kisasa wakakuchekia hiyo kitu kama nzima ama la! Hii itakusaidia mfuko wako usitoboke kwa sababu ya kutokujua!

Kuendesha gari nzima isiyo na tatizo ni muhimu sana kwani maisha hayajaribiwi mkuu!
 
Wakuu kimya sana, naombeni ajuaye gereji itoayo huduma nzuri kwa wateja (usijali gharama zako) hapo Mwanza!
 
Muhimu kufanya general service ya gari..engine oil na oil filter, gearbox oil, sparkplugs, aircleaner, ac airfilter, na ukiweza badilisha matairi km una safari ya masafa au usafiri usiku. Sio muhimu kubadilisha timing belt/chain unless imepita km 100k..
 
Muhimu kufanya general service ya gari..engine oil na oil filter, gearbox oil, sparkplugs, aircleaner, ac airfilter, na ukiweza badilisha matairi km una safari ya masafa au usafiri usiku. Sio muhimu kubadilisha timing belt/chain unless imepita km 100k..
Asante sana mkuu kwa mchango wako!
 
Back
Top Bottom