Seven days in hell! (siku saba kuzimu)-1

Seven days in hell! (siku saba kuzimu)-1

nergomafioso

Senior Member
Joined
Apr 3, 2024
Posts
109
Reaction score
284
SEVEN DAYS IN HELL (SIKU SABA KUZIMU)

Episode-1

Damu nyingi zilikuwa zinanitoka upande wa kushoto wa kifua changu kiasi cha kunifanya nilowe chapachapa. Nilijitahidi kuinuka pale nilipokuwa nimelala huku damu nyingi zikiendelea kunitoka lakini maumivu makali yalinirudisha chini.


Kwa kutumia mikono yangu miwili, nilijaribu kuminya pale kwenye jeraha kubwa ili kuzuia damu isiendelee kunimwagika lakini nilijikuta mikono ikikosa nguvu, kadiri muda ulivyokuwa unasonga mbele ndivyo nilivyokuwa nazidi kuishiwa nguvu.

Watu wengi walianza kukimbilia pale nilipokuwa nimeanguka na kunizunguka, niliwasikia wengine wakishindwa kuficha hisia zao na kuanza kuangua vilio wakilitaja jina langu. Nadhani hali waliyoniona nayo iliwafanya waamini kwamba siwezi kabisa kupona kutokana na damu zilivyokuwa zinaendelea kunimwagika mithili ya bomba lililopasuka.

Nikiwa kwenye maumivu makali, nilijigeuza na kuanza kutazama angani, upeo wa macho yangu ukagota kwenye mawingu meupe na ya bluu yaliyokuwa yakilipendezesha anga, nikabaki nimetulia nikiwa kwenye hali hiyo.

Kelele za watu wengi waliokuwa wanazidi kuongezeka eneo la tukio kunishangaa, zilianza kupungua taratibu masikioni mwangu, zikazidi kupungua na baadaye nikawa nasikia kama watu wananong’ona. Kwa mbali nilisikia mlio wa ving’ora ambavyo hata hivyo sikujua ni vya nini.

Nikiwa naendelea kutazama angani, taswira ndani ya mboni za macho yangu ilianza kufifia taratibu na kadiri muda ulivyokuwa unazidi kusonga mbele ndivyo nayo ilivyozidi kufifia, japokuwa ilikuwa ni mchana, kigiza kikaanza kutanda kwenye macho yangu.

Nakumbuka neno la mwisho nililofanikiwa kulisema, ingawa ilikuwa ni kwa taabu kubwa kutokanana midomo yangu kuwa mizito, ilikuwa ni: Mungu nisaidie! Nikafumba macho na giza totoro likatawala kila sehemu, sikuelewa tena kilichoendelea baada ya hapo!

Katika hali ambayo sikuitegemea na ambayo mpaka leo huwa siwezi kuifafanua, muda mfupi baadaye nilijikuta nikizinduka lakini nikiwa kwenye hali ya tofauti kabisa. Nilizinduka nikiwa palepale nilipokuwa nimelala awali lakini katika hali ya ajabu, nilikuwa mwepesi sana.

Nikajikuta nikianza kupaa taratibu kuelekea juu. Nikiwa juu kidogo, niligeuka na kutazama pale nilipokuwa nimeangukia, nikashangaa kuona bado mwili wangu ulikuwa umelala palepale, damu nyingi zikiendelea kutoka kwenye jeraha la kifuani, tena safari hii zikitoka kwa mabongemabonge.

“Mungu wangu! Hiki ni kitu gani tena?” nilijikuta nikisema kwa sauti ya chini, ungeweza kudhani nilikuwa kwenye ndoto lakini haikuwa hivyo. Nilijiuliza kama mwili wangu bado ulikuwa pale chini, mimi niliyekuwa napaa nilikuwa ni nani?Sikupata majibu.

Niliendelea kupaa kuelekea juu mpaka nikafikia umbali wa mita kadhaa, ulioniwezesha kuona vizuri kila kitu kilichokuwa kinaendelea eneo la tukio. Niliwaona watuwakizidi kumiminika kwa wingi eneo la tukio, wengine wakishika vichwa vyao baada ya kuuona mwili wangu ukiwa kwenye hali ile.

Niliwaona watu kadhaa ambao nilikuwa nikiwafahamu wakiwa na nyuso za huzuni kali, wengine wakiangua vilio kwa nguvu. Nilimuona rafiki yangu na mfanyakazi mwenzangu ambaye muda mfupi kabla ya tukio nilikuwa naye, Justice akiwa analia kwa uchungu mno huku akilitaja jina langu.

Nilimuona pia Raya, msichana ambaye naye tulikuwa tukifanya naye kazi na ambaye alikuwa anapenda sana kuwa karibu na mimi ingawa mara kwa mara nilikuwa nikimkwepa (nitaeleza zaidi kuhusu msichana huyu baadaye), naweza kusema yeye ndiye aliyekuwa na hali mbaya kuliko watu wengine wote kwani alikuwa akilia kwa sauti ya juu huku akilitaja jina langu kiasi cha kusababisha muda mfupi baadaye aanguke na kupoteza fahamu.

Niliwaona pia baadhi ya watu wakiupiga picha mwili wangu kwa kutumia simu zao za mikononi, niliwaona pia waandishi kadhaa wa habari ambao nao walikuwa wakipiga picha nyingi eneo la tukio, za mnato na za video.

Muda mfupi baadaye, walifika askari wanne waliokuwa wamepakizana kwenye pikipiki mbili, maarufu kama tigo ambao niliwaona wakianza kuwarudisha watu nyuma kutoka pale mwili wangu ulipokuwa umelala.

Mmoja wao alisogea jirani kabisa, nikamuona akiuchunguza mwili wangu kisha akaugusa shingoni kama anayesikiliza mapigo ya moyo, nikamuona akiinuka na kuwasogelea wenzake, wakawa wanazungumza jambo ambalo sikuelewa ni nini. Mmoja akatoa simu ya upepo (radio call) na akawa anazungumza na upande wa pili.

Nikiwa bado naendelea kushangaa kwani kila kitu kilikuwa kigeni kwangu, nilianza kusikia ving’ora kwa mbali, nikakumbuka kwamba kabla sijapoteza fahamu kutokana na kutokwa na damu nyingi, nilivisikia tena ving’ora hivyo lakini tofauti yake ni kwamba sasa nilikuwa na uwezo wa kuona kila kilichokuwa kinaendelea.

Lilikuwa ni gari la kubebea wagonjwa (ambulance) ambalo lilikuwa likija kwa kasi eneo lile mwili wangu ulipokuwepo. Nyuma yake lilikuwa limeongozana na difenda ya polisi ambayo niliitambua kwa urahisi kutokana na namba zake za usajili na maandishi yaliyokuwa ubavuni yaliyosomeka ‘Police’.

Wale askari waliokuwepo eneo la tukio waliwatawanya watu upande ule ile ambulance ilikokuwa inatokea, gari likasogea mpaka jirani kabisa na pale mwili wangu ulipokuwepo.

Likasimama ambapo manesi wanne waliovalia nguo nyeupe waliteremka wakiwa na machela, sambamba na askari kadhaa waliokuwa kwenye ile difenda, wote wakasogea na kuuzunguka mwili wangu.

Wakasaidiana kuuinua mwili wangu pale chini na kuulaza kwenye machela kisha wakauingiza kwenye ambulance. Nilimuona Justice naye akipanda. Raya yeye alipakizwa kwenye lile gari la polisi akiwa hajitambui.

Gari likaondoka kwa kasi kubwa likifuatiwa na difenda kwa nyuma, wale askari wa pikipiki waliendelea kuwepo pale eneo la tukio kwa dakika kadhaa wakiwa makini kuwasikiliza watu walichokuwa wanakisema huku wakiwahoji wengine kadhaa.

Kwa muda wote huo, bado nilikuwa najiuliza kilichotokea bila kupata majibu, sikuelewa nipo kwenye hali gani kwa sababu kama ni mwili wangu, tayari ulishapakizwa kwenye ambulance na kukimbizwa hospitali lakini nilishangaa mimi bado nipo eneo lile nikielea angani.

Nilijiuliza ule mwili wangu unapelekwa wapi lakini pia sikupata majibu. Ghafla nilipata wazo la kuifukuzia ile ambulance ili nijue wanaupeleka wapi mwili wangu. Wazo nililoona linafaa, ilikuwa ni kushuka chini na kuchukua bodaboda kwani niliamini kutokana na foleni iliyokuwepo na kasi ya ambulance, ni usafiri huo pekee ndiyo unaoweza kuniwahisha.

Nilishuka jirani kabisa na pale mwili wangu ulipokuwepo muda mfupi uliopita, watu wakawa wameshaanza kutawanyika huku wengine wakijikusanya vikundivikundi pembeni na kujadiliana kuhusu kilichotokea. Nilimsikia mzee mmoja akiwaambia wenzake: “Kwa hali aliyonayo, hawezi kupona, lazima afe.”

Nikashtuka sana kusikia kauli hiyo kwa sababu sikujua wanamzungumzia nani kwamba lazima afe wakati mimi bado nilikuwa hai na nilikuwa nawasikia wanachokisema.

Sikutaka kupoteza muda, harakaharaka nilisogea pembeni ya barabara na kupunga mkono kusimamisha bodaboda, japokuwa dereva alikuwa akija upande wangu, nilishangaa akinipita kama hajaniona. Akaja wa pili naye licha ya kumpungia mkono kwa nguvu hakusimama, akanipita kwa kasi.

Nilijitazama vizuri mwilini kwani nilihisi huenda wanaogopa kusimama kutokana na mwili wangu kulowa damu lakini kituambacho pia nilishindwa kukielewa, shati nililokuwa nimevaa halikuwa na hata tone la damu. Lilikuwa ni shati lilelile ambalo mwili wangu wakati unatolewa eneo lile lilikuwa halitamaniki kwa damu.

Nilishindwa kuelewa ni nini hasa kimetokea, nikajitazama vizuri mwili wangu na kugundua kwamba ulikuwa na hali fulani kama ya kung’aa kusiko kwa kawaida, nilijishika pale kifuani lakini hapakuwa na alama kwamba nilikuwa nimejeruhiwa vibaya, nikazidi kuchanganyikiwa.

Ilibidi nisogee mpaka kwenye maegesho ya bodaboda nikiamini pale itakuwa rahisi kuzungumza na dereva yoyote ili aniwahishe kabla ile ambulance haijapotea kabisa.

Nilipopiga hatua moja nilijiona kuwa mwepesi sana halafu tambo lilikuwa refu sana tofauti na kawaida. Sehemu ambayo ningetembea hata hatua ishirini, nilipiga hatua mbili tu, nikawa nimeshafika pale kwenye bodaboda.

Je, nini kitafuatia? Usikose
 
Damu nyingi zilikuwa zinanitoka upande wa kushoto wa kifua changu kiasi cha kunifanya nilowe chapachapa. Nilijitahidi kuinuka pale nilipokuwa nimelala huku damu nyingi zikiendelea kunitoka lakini maumivu makali yalinirudisha chini.


Kwa kutumia mikono yangu miwili, nilijaribu kuminya pale kwenye jeraha kubwa ili kuzuia damu isiendelee kunimwagika lakini nilijikuta mikono ikikosa nguvu, kadiri muda ulivyokuwa unasonga mbele ndivyo nilivyokuwa nazidi kuishiwa nguvu.

Watu wengi walianza kukimbilia pale nilipokuwa nimeanguka na kunizunguka, niliwasikia wengine wakishindwa kuficha hisia zao na kuanza kuangua vilio wakilitaja jina langu. Nadhani hali waliyoniona nayo iliwafanya waamini kwamba siwezi kabisa kupona kutokana na damu zilivyokuwa zinaendelea kunimwagika mithili ya bomba lililopasuka.

Nikiwa kwenye maumivu makali, nilijigeuza na kuanza kutazama angani, upeo wa macho yangu ukagota kwenye mawingu meupe na ya bluu yaliyokuwa yakilipendezesha anga, nikabaki nimetulia nikiwa kwenye hali hiyo.

Kelele za watu wengi waliokuwa wanazidi kuongezeka eneo la tukio kunishangaa, zilianza kupungua taratibu masikioni mwangu, zikazidi kupungua na baadaye nikawa nasikia kama watu wananong’ona. Kwa mbali nilisikia mlio wa ving’ora ambavyo hata hivyo sikujua ni vya nini.

Nikiwa naendelea kutazama angani, taswira ndani ya mboni za macho yangu ilianza kufifia taratibu na kadiri muda ulivyokuwa unazidi kusonga mbele ndivyo nayo ilivyozidi kufifia, japokuwa ilikuwa ni mchana, kigiza kikaanza kutanda kwenye macho yangu.

Nakumbuka neno la mwisho nililofanikiwa kulisema, ingawa ilikuwa ni kwa taabu kubwa kutokanana midomo yangu kuwa mizito, ilikuwa ni: Mungu nisaidie! Nikafumba macho na giza totoro likatawala kila sehemu, sikuelewa tena kilichoendelea baada ya hapo!

Katika hali ambayo sikuitegemea na ambayo mpaka leo huwa siwezi kuifafanua, muda mfupi baadaye nilijikuta nikizinduka lakini nikiwa kwenye hali ya tofauti kabisa. Nilizinduka nikiwa palepale nilipokuwa nimelala awali lakini katika hali ya ajabu, nilikuwa mwepesi sana.

Nikajikuta nikianza kupaa taratibu kuelekea juu. Nikiwa juu kidogo, niligeuka na kutazama pale nilipokuwa nimeangukia, nikashangaa kuona bado mwili wangu ulikuwa umelala palepale, damu nyingi zikiendelea kutoka kwenye jeraha la kifuani, tena safari hii zikitoka kwa mabongemabonge.

“Mungu wangu! Hiki ni kitu gani tena?” nilijikuta nikisema kwa sauti ya chini, ungeweza kudhani nilikuwa kwenye ndoto lakini haikuwa hivyo. Nilijiuliza kama mwili wangu bado ulikuwa pale chini, mimi niliyekuwa napaa nilikuwa ni nani?Sikupata majibu.

Niliendelea kupaa kuelekea juu mpaka nikafikia umbali wa mita kadhaa, ulioniwezesha kuona vizuri kila kitu kilichokuwa kinaendelea eneo la tukio. Niliwaona watuwakizidi kumiminika kwa wingi eneo la tukio, wengine wakishika vichwa vyao baada ya kuuona mwili wangu ukiwa kwenye hali ile.

Niliwaona watu kadhaa ambao nilikuwa nikiwafahamu wakiwa na nyuso za huzuni kali, wengine wakiangua vilio kwa nguvu. Nilimuona rafiki yangu na mfanyakazi mwenzangu ambaye muda mfupi kabla ya tukio nilikuwa naye, Justice akiwa analia kwa uchungu mno huku akilitaja jina langu.

Nilimuona pia Raya, msichana ambaye naye tulikuwa tukifanya naye kazi na ambaye alikuwa anapenda sana kuwa karibu na mimi ingawa mara kwa mara nilikuwa nikimkwepa (nitaeleza zaidi kuhusu msichana huyu baadaye), naweza kusema yeye ndiye aliyekuwa na hali mbaya kuliko watu wengine wote kwani alikuwa akilia kwa sauti ya juu huku akilitaja jina langu kiasi cha kusababisha muda mfupi baadaye aanguke na kupoteza fahamu.

Niliwaona pia baadhi ya watu wakiupiga picha mwili wangu kwa kutumia simu zao za mikononi, niliwaona pia waandishi kadhaa wa habari ambao nao walikuwa wakipiga picha nyingi eneo la tukio, za mnato na za video.

Muda mfupi baadaye, walifika askari wanne waliokuwa wamepakizana kwenye pikipiki mbili, maarufu kama tigo ambao niliwaona wakianza kuwarudisha watu nyuma kutoka pale mwili wangu ulipokuwa umelala.

Mmoja wao alisogea jirani kabisa, nikamuona akiuchunguza mwili wangu kisha akaugusa shingoni kama anayesikiliza mapigo ya moyo, nikamuona akiinuka na kuwasogelea wenzake, wakawa wanazungumza jambo ambalo sikuelewa ni nini. Mmoja akatoa simu ya upepo (radio call) na akawa anazungumza na upande wa pili.

Nikiwa bado naendelea kushangaa kwani kila kitu kilikuwa kigeni kwangu, nilianza kusikia ving’ora kwa mbali, nikakumbuka kwamba kabla sijapoteza fahamu kutokana na kutokwa na damu nyingi, nilivisikia tena ving’ora hivyo lakini tofauti yake ni kwamba sasa nilikuwa na uwezo wa kuona kila kilichokuwa kinaendelea.

Lilikuwa ni gari la kubebea wagonjwa (ambulance) ambalo lilikuwa likija kwa kasi eneo lile mwili wangu ulipokuwepo. Nyuma yake lilikuwa limeongozana na difenda ya polisi ambayo niliitambua kwa urahisi kutokana na namba zake za usajili na maandishi yaliyokuwa ubavuni yaliyosomeka ‘Police’.

Wale askari waliokuwepo eneo la tukio waliwatawanya watu upande ule ile ambulance ilikokuwa inatokea, gari likasogea mpaka jirani kabisa na pale mwili wangu ulipokuwepo.

Likasimama ambapo manesi wanne waliovalia nguo nyeupe waliteremka wakiwa na machela, sambamba na askari kadhaa waliokuwa kwenye ile difenda, wote wakasogea na kuuzunguka mwili wangu.

Wakasaidiana kuuinua mwili wangu pale chini na kuulaza kwenye machela kisha wakauingiza kwenye ambulance. Nilimuona Justice naye akipanda. Raya yeye alipakizwa kwenye lile gari la polisi akiwa hajitambui.

Gari likaondoka kwa kasi kubwa likifuatiwa na difenda kwa nyuma, wale askari wa pikipiki waliendelea kuwepo pale eneo la tukio kwa dakika kadhaa wakiwa makini kuwasikiliza watu walichokuwa wanakisema huku wakiwahoji wengine kadhaa.

Kwa muda wote huo, bado nilikuwa najiuliza kilichotokea bila kupata majibu, sikuelewa nipo kwenye hali gani kwa sababu kama ni mwili wangu, tayari ulishapakizwa kwenye ambulance na kukimbizwa hospitali lakini nilishangaa mimi bado nipo eneo lile nikielea angani.

Nilijiuliza ule mwili wangu unapelekwa wapi lakini pia sikupata majibu. Ghafla nilipata wazo la kuifukuzia ile ambulance ili nijue wanaupeleka wapi mwili wangu. Wazo nililoona linafaa, ilikuwa ni kushuka chini na kuchukua bodaboda kwani niliamini kutokana na foleni iliyokuwepo na kasi ya ambulance, ni usafiri huo pekee ndiyo unaoweza kuniwahisha.

Nilishuka jirani kabisa na pale mwili wangu ulipokuwepo muda mfupi uliopita, watu wakawa wameshaanza kutawanyika huku wengine wakijikusanya vikundivikundi pembeni na kujadiliana kuhusu kilichotokea. Nilimsikia mzee mmoja akiwaambia wenzake: “Kwa hali aliyonayo, hawezi kupona, lazima afe.”

Nikashtuka sana kusikia kauli hiyo kwa sababu sikujua wanamzungumzia nani kwamba lazima afe wakati mimi bado nilikuwa hai na nilikuwa nawasikia wanachokisema.

Sikutaka kupoteza muda, harakaharaka nilisogea pembeni ya barabara na kupunga mkono kusimamisha bodaboda, japokuwa dereva alikuwa akija upande wangu, nilishangaa akinipita kama hajaniona. Akaja wa pili naye licha ya kumpungia mkono kwa nguvu hakusimama, akanipita kwa kasi.

Nilijitazama vizuri mwilini kwani nilihisi huenda wanaogopa kusimama kutokana na mwili wangu kulowa damu lakini kituambacho pia nilishindwa kukielewa, shati nililokuwa nimevaa halikuwa na hata tone la damu. Lilikuwa ni shati lilelile ambalo mwili wangu wakati unatolewa eneo lile lilikuwa halitamaniki kwa damu.

Nilishindwa kuelewa ni nini hasa kimetokea, nikajitazama vizuri mwili wangu na kugundua kwamba ulikuwa na hali fulani kama ya kung’aa kusiko kwa kawaida, nilijishika pale kifuani lakini hapakuwa na alama kwamba nilikuwa nimejeruhiwa vibaya, nikazidi kuchanganyikiwa.

Ilibidi nisogee mpaka kwenye maegesho ya bodaboda nikiamini pale itakuwa rahisi kuzungumza na dereva yoyote ili aniwahishe kabla ile ambulance haijapotea kabisa.

Nilipopiga hatua moja nilijiona kuwa mwepesi sana halafu tambo lilikuwa refu sana tofauti na kawaida. Sehemu ambayo ningetembea hata hatua ishirini, nilipiga hatua mbili tu, nikawa nimeshafika pale kwenye bodaboda.

Je, nini kitafuatia? Usikose
Mh??? Ukiendelea nitag!
 

SEVEN DAYS IN HELL (SIKU SABA KUZIMU)​


Episode-2

ILIBIDI nisogee mpaka kwenye maegesho ya bodaboda nikiamini pale itakuwa rahisi kuzungumza na dereva yeyote ili aniwahishe kabla ile ‘ambulance’ haijapotea kabisa. Nilipopiga hatua moja, nilijiona kuwa mwepesi sana halafu tambo lilikuwa refu sana tofauti na kawaida.

Sehemu ambayo ningetembea hata hatua ishirini, nilipiga hatua mbili tu, nikawa nimeshafika pale kwenye bodaboda.

SASA ENDELEA…
“OYA mambo vipi mkubwa!” nilimsalimu dereva wa bodaboda aliyekuwa pembeni yangu kwa bashasha kubwa lakini hakuniitikia, akawa anaendelea kuifutafuta bodaboda yake.

Nilirudia kumsalimu lakini bado hakunijibu chochote na wala hakuonyesha kama ananisikia. Nilimgusa begani lakini bado ilikuwa ni kazi bure, aliendelea kufutafuta bodaboda yake, nikabaki nimepigwa na butwaa.

Ilibidi nimsogelee dereva mwingine wa bodaboda, naye nikamsalimia kwa bashasha lakini hakunijibu, nikarudia tena na tena lakini bado hali ilikuwa ileile, nikaenda kwa watatu ambaye alikuwa akipiga stori na wenzake, naye akaonyesha kutonisikia.

“Kwani imekuwaje? Mbona sielewi kinachoendelea?” nilijisemea huku nikianza kutetemeka kwa hofu kubwa, mwisho niliamua kufanya jambo moja, nilipaza sauti kwa nguvu nikiita ‘bodabodaaa!’ niliamini yeyote ambaye atakuwa wa kwanza kuniona basi nitamchukua huyohuyo lakini wapi! Kila mmoja aliendelea na mambo yake.
Ni hapo ndipo nilipogundua kwamba huenda nilikuwa sionekani kwa macho ya kawaida wala sauti yangu haisikiki licha ya ukweli kwamba mwenyewe nilikuwa najisikia vizuri tu.

“Sasa nitafanyaje?” nilisema huku nikigeuka kuitazama ile ‘ambulance’, tayari ilishapotea kwenye upeo wa macho yangu lakini akili zangu zilinituma kuamini kwamba lazima itakuwa imeupeleka mwili wangu Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

“Nataka nikashuhudie kila kitu kinachoendelea,” nilisema huku nikianza kutafuta mbinu nyingine ya kunifikisha hospitalini hapo. Sijui nilipata wapi akili hizo lakini nilijikuta tu nikiamua kuanza kutimua mbio kuelekea kule ile ambulance ilikoelekea.

Nilipopiga hatua chache tu, nilijikuta nikiwa napaa angani kwa kasi kubwa, nikawa naitazama mitaa ya jiji kutokea angani. Kuna wakati akili zangu zilinituma kuamini kabisa kwamba nilikuwa kwenye ndoto ya kutisha ambayo muda wowote itaisha lakini akili nyingine zikawa zinaniambia kwamba siyo ndoto, kila kitu kilikuwa kikitokea kwa uhalisia.

Wakati ambulance ikiwasili kwenye geti kuu la kuingilia Muhimbili, na mimi tayari nilikuwa nimeshafika eneo hilo, geti likafunguliwa na likaingia moja kwa moja mpaka kwenye eneo la ‘emergency’ ambalo wagonjwa wenye hali mbaya ndipo walipokuwa wanafikia.

Milango ya ambulance ilifunguliwa, manesi waliokuwa ndani ya ile ambulance pamoja na wengine waliokuwa pale mapokezi, walisaidiana kuushusha mwili wangu na kukimbizwa mpaka ndani, nikawa nashuhudia kila kitu kilichokuwa kinaendelea.

Harakaharaka nilianza kupewa huduma ya kwanza, nikamuona nesi mmoja akichukua mkasi na kukata shati nililokuwa nimevaa, nilipoliona jeraha lililokuwa kifuani wangu, nilisisimka mno. Nilijiuliza iweje mtu anifanyie ukatili mkubwa kiasi hicho, tena bila sababu ya msingi?

Japokuwa vitabu vya dini vinakataza kulipa kisasi, nilijikuta nikipandwa na ari kubwa ya kulipa kisasi, nilikuwa nimejeruhiwa sana. Niliwaona hata wale manesi akitetemeka kila walipokuwa wanalitazama jeraha langu.
Kwa bahati nzuri, madaktari wa kiume waliingia, huwa naamini siku zote kwamba sisi wanaume Mungu ametuumba na ujasiri mkubwa kuliko wanawake. Wakaanza kunifanyia kile ambacho

kitaalamu huwa kinaitwa ‘dressing’, yaani kusafisha jeraha kabla ya kuanza kutibiwa. Muda mfupi baadaye, tayari nilikuwa nimesafishwa jeraha hilo, nikahamishwa na kupelekwa chumba cha wagonjwa mahututi nikiwa bado sijitambui huku madaktari na manesi wakiendelea kuhangaika kudhibiti damu zilizokuwa zinaendelea kunitoka kwa wingi.

Nilipoingizwa kwenye chumba cha wagonjwa mahututi, harakaharaka niliunganishwa kwenye mashine ya kunisaidia kupumua huku dripu ikitiririka kwa kasi kuingia kwenye mishipa yangu.

“He has lost a great deal of blood, he need an urgent transfusion,” (Amepoteza damu nyingi sana, anahitaji kuongezewa damu haraka iwezekanavyo) alisema daktari mmoja kwa Kiingereza, kwa kuwa na mimi shule ilikuwepo kiasi chake kichwani, nilimuelewa vizuri.

Niendelee kusisitiza kwamba wakati haya yote yakitokea, katika ulimwengu wa kawaida sikuwa na fahamu hata kidogo, nilikuwa nimefumba macho na kulala pale kitandani kama maiti, nikiwa nimeunganishwa na mashine ya kunisaidia kupumua lakini katika ulimwengu mwingine ambao hata sijui niuiteje, nilikuwa nimesimama kwenye pembe moja ya ile wodi, nikishuhudia kila kilichokuwa kinaendelea.

Kazi ya kuokoa maisha yangu iliendelea, madaktari na manesi wakawa wanapishana huku na kule, huyu kabeba dawa, huyu kabeba chupa ya damu, huyu mikasi na sindano, ilimradi kila mmoja alikuwa bize.
Nilijisikia ahueni kubwa ndani ya moyo wangu kuona watu ambao pengine hata hawakuwa wakinijua, wakipigana kuokoa maisha yangu.

Niliendelea kuwatazama wanavyohangaika, kuna wakati machozi ya uchungu yalikuwa yakinitoka kwa sababu ya kilichotokea, nikawa naendelea kujiuliza maswali mengi yaliyokosa majibu.

Nilivuta kumbukumbu ya jinsi mambo yote yalivyoanza kutokea.
***
Januari 16, 2012
Mikocheni, Dar es Salaam.
“Haloo!”
“Haloo, nani mwenzangu.”
“Mh! Kwani namba yangu hujaisevu Moses, mbona una visa wewe.”

“Samahani, utakuwa umekosea namba, mimi siitwi Moses wala sikufahamu.”

“Ooh! Basi samahani kaka yangu nitakuwa nimechanganya namba. Samahani sana.”

“Usijali, kuwa makini,” yalikuwa ni mazungumzo kati yangu na mtu aliyepiga simu na kunifananisha.

Nilikata simu na kubonyeza kitufe kwenye rimoti ya runinga yangu kubwa (flat screen) niliyokuwa nimekata sauti (mute) baada ya kuona simu yangu inaita. Nikawa naendelea kutazama muvi kwani miongoni mwa vitu nilivyokuwa navipenda, ilikuwa ni kutazama muvi, kuangalia mpira na kusikiliza muziki, hasa muda ninaokuwa nyumbani baada ya kutoka kazini.

Haukupita muda mrefu, simu yangu ikawa inaita tena, nilikasirika kwa sababu muvi ilikuwa imefika sehemu nzuri na sikutaka inipite hata sehemu moja, safari hii nilibonyeza kitufe cha ‘pause’ kuisimamisha ili isiendelee, nilipotazama namba ya mpigaji, ilikuwa ni ileile ya yule mtu aliyedai kukosea namba.

“Samahani mpendwa najua nakusumbua, nimeangalia vizuri simu yangu na kugundua kuwa ni kweli nilikosea namba wakati nakupigia.”

“Usijali dada, tufanye yameisha.”

“Ahsante kwa kunisamehe kaka yangu, japo sikujui lakini unaonekana mstaarabu sana. Mimi naitwa Shenaiza sijui mwenzangu unaitwa nani.”

“Naitwa Jamal au kwa kifupi Jay,” nilimjibu kwa kifupi kwa sababu niliona kama ananiletea stori zisizo na kichwa wala miguu.

“Ooh! Nimefurahi kukufahamu kaka Jamal. Unaishi wapi vile?”

“Mikocheni,” nilimjibu na safari hii niliamua kubonyeza tena rimoti, muvi ikaendelea kwani niliona hana chochote cha maana cha kuniambia, nikawa nimeiweka simu sikioni huku nikiendelea kuangalia muvi.
“Mbona kuna kelele kwani uko wapi?”

Alihoji msichana huyo lakini sikumjibu chochote, naona baadaye alijishtukia mwenyewe, akaamua kukata simu. Nikaiweka simu pembeni na kuendelea kutazama muvi.
Baadaye ilipoisha, nilichukua simu yangu na kugundua kuwa kulikuwa na meseji nyingi zimeingia bila mwenyewe kushtukia, nikaanza kuzisoma moja baada ya nyingine.

Nilishangaa kugundua kwamba ukiachilia mbali meseji mbili za rafiki zangu, Justice na Prosper, nyingine zote zilikuwa zimetoka kwa yule msichana aliyekosea namba ya simu, nikashusha pumzi ndefu na kuanza kuzisoma, moja baada ya nyingine nikiwa na shauku kubwa ya kutaka kuona ameandika nini.

Je, nini kitafuatia? Meseji zinahusu nini? Usikose
 

SEVEN DAYS IN HELL (SIKU SABA KUZIMU)​


Episode-2

ILIBIDI nisogee mpaka kwenye maegesho ya bodaboda nikiamini pale itakuwa rahisi kuzungumza na dereva yeyote ili aniwahishe kabla ile ‘ambulance’ haijapotea kabisa. Nilipopiga hatua moja, nilijiona kuwa mwepesi sana halafu tambo lilikuwa refu sana tofauti na kawaida.

Sehemu ambayo ningetembea hata hatua ishirini, nilipiga hatua mbili tu, nikawa nimeshafika pale kwenye bodaboda.

SASA ENDELEA…
“OYA mambo vipi mkubwa!” nilimsalimu dereva wa bodaboda aliyekuwa pembeni yangu kwa bashasha kubwa lakini hakuniitikia, akawa anaendelea kuifutafuta bodaboda yake.

Nilirudia kumsalimu lakini bado hakunijibu chochote na wala hakuonyesha kama ananisikia. Nilimgusa begani lakini bado ilikuwa ni kazi bure, aliendelea kufutafuta bodaboda yake, nikabaki nimepigwa na butwaa.

Ilibidi nimsogelee dereva mwingine wa bodaboda, naye nikamsalimia kwa bashasha lakini hakunijibu, nikarudia tena na tena lakini bado hali ilikuwa ileile, nikaenda kwa watatu ambaye alikuwa akipiga stori na wenzake, naye akaonyesha kutonisikia.

“Kwani imekuwaje? Mbona sielewi kinachoendelea?” nilijisemea huku nikianza kutetemeka kwa hofu kubwa, mwisho niliamua kufanya jambo moja, nilipaza sauti kwa nguvu nikiita ‘bodabodaaa!’ niliamini yeyote ambaye atakuwa wa kwanza kuniona basi nitamchukua huyohuyo lakini wapi! Kila mmoja aliendelea na mambo yake.
Ni hapo ndipo nilipogundua kwamba huenda nilikuwa sionekani kwa macho ya kawaida wala sauti yangu haisikiki licha ya ukweli kwamba mwenyewe nilikuwa najisikia vizuri tu.

“Sasa nitafanyaje?” nilisema huku nikigeuka kuitazama ile ‘ambulance’, tayari ilishapotea kwenye upeo wa macho yangu lakini akili zangu zilinituma kuamini kwamba lazima itakuwa imeupeleka mwili wangu Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

“Nataka nikashuhudie kila kitu kinachoendelea,” nilisema huku nikianza kutafuta mbinu nyingine ya kunifikisha hospitalini hapo. Sijui nilipata wapi akili hizo lakini nilijikuta tu nikiamua kuanza kutimua mbio kuelekea kule ile ambulance ilikoelekea.

Nilipopiga hatua chache tu, nilijikuta nikiwa napaa angani kwa kasi kubwa, nikawa naitazama mitaa ya jiji kutokea angani. Kuna wakati akili zangu zilinituma kuamini kabisa kwamba nilikuwa kwenye ndoto ya kutisha ambayo muda wowote itaisha lakini akili nyingine zikawa zinaniambia kwamba siyo ndoto, kila kitu kilikuwa kikitokea kwa uhalisia.

Wakati ambulance ikiwasili kwenye geti kuu la kuingilia Muhimbili, na mimi tayari nilikuwa nimeshafika eneo hilo, geti likafunguliwa na likaingia moja kwa moja mpaka kwenye eneo la ‘emergency’ ambalo wagonjwa wenye hali mbaya ndipo walipokuwa wanafikia.

Milango ya ambulance ilifunguliwa, manesi waliokuwa ndani ya ile ambulance pamoja na wengine waliokuwa pale mapokezi, walisaidiana kuushusha mwili wangu na kukimbizwa mpaka ndani, nikawa nashuhudia kila kitu kilichokuwa kinaendelea.

Harakaharaka nilianza kupewa huduma ya kwanza, nikamuona nesi mmoja akichukua mkasi na kukata shati nililokuwa nimevaa, nilipoliona jeraha lililokuwa kifuani wangu, nilisisimka mno. Nilijiuliza iweje mtu anifanyie ukatili mkubwa kiasi hicho, tena bila sababu ya msingi?

Japokuwa vitabu vya dini vinakataza kulipa kisasi, nilijikuta nikipandwa na ari kubwa ya kulipa kisasi, nilikuwa nimejeruhiwa sana. Niliwaona hata wale manesi akitetemeka kila walipokuwa wanalitazama jeraha langu.
Kwa bahati nzuri, madaktari wa kiume waliingia, huwa naamini siku zote kwamba sisi wanaume Mungu ametuumba na ujasiri mkubwa kuliko wanawake. Wakaanza kunifanyia kile ambacho

kitaalamu huwa kinaitwa ‘dressing’, yaani kusafisha jeraha kabla ya kuanza kutibiwa. Muda mfupi baadaye, tayari nilikuwa nimesafishwa jeraha hilo, nikahamishwa na kupelekwa chumba cha wagonjwa mahututi nikiwa bado sijitambui huku madaktari na manesi wakiendelea kuhangaika kudhibiti damu zilizokuwa zinaendelea kunitoka kwa wingi.

Nilipoingizwa kwenye chumba cha wagonjwa mahututi, harakaharaka niliunganishwa kwenye mashine ya kunisaidia kupumua huku dripu ikitiririka kwa kasi kuingia kwenye mishipa yangu.

“He has lost a great deal of blood, he need an urgent transfusion,” (Amepoteza damu nyingi sana, anahitaji kuongezewa damu haraka iwezekanavyo) alisema daktari mmoja kwa Kiingereza, kwa kuwa na mimi shule ilikuwepo kiasi chake kichwani, nilimuelewa vizuri.

Niendelee kusisitiza kwamba wakati haya yote yakitokea, katika ulimwengu wa kawaida sikuwa na fahamu hata kidogo, nilikuwa nimefumba macho na kulala pale kitandani kama maiti, nikiwa nimeunganishwa na mashine ya kunisaidia kupumua lakini katika ulimwengu mwingine ambao hata sijui niuiteje, nilikuwa nimesimama kwenye pembe moja ya ile wodi, nikishuhudia kila kilichokuwa kinaendelea.

Kazi ya kuokoa maisha yangu iliendelea, madaktari na manesi wakawa wanapishana huku na kule, huyu kabeba dawa, huyu kabeba chupa ya damu, huyu mikasi na sindano, ilimradi kila mmoja alikuwa bize.
Nilijisikia ahueni kubwa ndani ya moyo wangu kuona watu ambao pengine hata hawakuwa wakinijua, wakipigana kuokoa maisha yangu.

Niliendelea kuwatazama wanavyohangaika, kuna wakati machozi ya uchungu yalikuwa yakinitoka kwa sababu ya kilichotokea, nikawa naendelea kujiuliza maswali mengi yaliyokosa majibu.

Nilivuta kumbukumbu ya jinsi mambo yote yalivyoanza kutokea.
***
Januari 16, 2012
Mikocheni, Dar es Salaam.
“Haloo!”
“Haloo, nani mwenzangu.”
“Mh! Kwani namba yangu hujaisevu Moses, mbona una visa wewe.”

“Samahani, utakuwa umekosea namba, mimi siitwi Moses wala sikufahamu.”

“Ooh! Basi samahani kaka yangu nitakuwa nimechanganya namba. Samahani sana.”

“Usijali, kuwa makini,” yalikuwa ni mazungumzo kati yangu na mtu aliyepiga simu na kunifananisha.

Nilikata simu na kubonyeza kitufe kwenye rimoti ya runinga yangu kubwa (flat screen) niliyokuwa nimekata sauti (mute) baada ya kuona simu yangu inaita. Nikawa naendelea kutazama muvi kwani miongoni mwa vitu nilivyokuwa navipenda, ilikuwa ni kutazama muvi, kuangalia mpira na kusikiliza muziki, hasa muda ninaokuwa nyumbani baada ya kutoka kazini.

Haukupita muda mrefu, simu yangu ikawa inaita tena, nilikasirika kwa sababu muvi ilikuwa imefika sehemu nzuri na sikutaka inipite hata sehemu moja, safari hii nilibonyeza kitufe cha ‘pause’ kuisimamisha ili isiendelee, nilipotazama namba ya mpigaji, ilikuwa ni ileile ya yule mtu aliyedai kukosea namba.

“Samahani mpendwa najua nakusumbua, nimeangalia vizuri simu yangu na kugundua kuwa ni kweli nilikosea namba wakati nakupigia.”

“Usijali dada, tufanye yameisha.”

“Ahsante kwa kunisamehe kaka yangu, japo sikujui lakini unaonekana mstaarabu sana. Mimi naitwa Shenaiza sijui mwenzangu unaitwa nani.”

“Naitwa Jamal au kwa kifupi Jay,” nilimjibu kwa kifupi kwa sababu niliona kama ananiletea stori zisizo na kichwa wala miguu.

“Ooh! Nimefurahi kukufahamu kaka Jamal. Unaishi wapi vile?”

“Mikocheni,” nilimjibu na safari hii niliamua kubonyeza tena rimoti, muvi ikaendelea kwani niliona hana chochote cha maana cha kuniambia, nikawa nimeiweka simu sikioni huku nikiendelea kuangalia muvi.
“Mbona kuna kelele kwani uko wapi?”

Alihoji msichana huyo lakini sikumjibu chochote, naona baadaye alijishtukia mwenyewe, akaamua kukata simu. Nikaiweka simu pembeni na kuendelea kutazama muvi.
Baadaye ilipoisha, nilichukua simu yangu na kugundua kuwa kulikuwa na meseji nyingi zimeingia bila mwenyewe kushtukia, nikaanza kuzisoma moja baada ya nyingine.

Nilishangaa kugundua kwamba ukiachilia mbali meseji mbili za rafiki zangu, Justice na Prosper, nyingine zote zilikuwa zimetoka kwa yule msichana aliyekosea namba ya simu, nikashusha pumzi ndefu na kuanza kuzisoma, moja baada ya nyingine nikiwa na shauku kubwa ya kutaka kuona ameandika nini.

Je, nini kitafuatia? Meseji zinahusu nini? Usikose
Very attractive
 
SEVEN DAYS IN HELL (SIKU SABA KUZIMU)

Episode-1

Damu nyingi zilikuwa zinanitoka upande wa kushoto wa kifua changu kiasi cha kunifanya nilowe chapachapa. Nilijitahidi kuinuka pale nilipokuwa nimelala huku damu nyingi zikiendelea kunitoka lakini maumivu makali yalinirudisha chini.


Kwa kutumia mikono yangu miwili, nilijaribu kuminya pale kwenye jeraha kubwa ili kuzuia damu isiendelee kunimwagika lakini nilijikuta mikono ikikosa nguvu, kadiri muda ulivyokuwa unasonga mbele ndivyo nilivyokuwa nazidi kuishiwa nguvu.

Watu wengi walianza kukimbilia pale nilipokuwa nimeanguka na kunizunguka, niliwasikia wengine wakishindwa kuficha hisia zao na kuanza kuangua vilio wakilitaja jina langu. Nadhani hali waliyoniona nayo iliwafanya waamini kwamba siwezi kabisa kupona kutokana na damu zilivyokuwa zinaendelea kunimwagika mithili ya bomba lililopasuka.

Nikiwa kwenye maumivu makali, nilijigeuza na kuanza kutazama angani, upeo wa macho yangu ukagota kwenye mawingu meupe na ya bluu yaliyokuwa yakilipendezesha anga, nikabaki nimetulia nikiwa kwenye hali hiyo.

Kelele za watu wengi waliokuwa wanazidi kuongezeka eneo la tukio kunishangaa, zilianza kupungua taratibu masikioni mwangu, zikazidi kupungua na baadaye nikawa nasikia kama watu wananong’ona. Kwa mbali nilisikia mlio wa ving’ora ambavyo hata hivyo sikujua ni vya nini.

Nikiwa naendelea kutazama angani, taswira ndani ya mboni za macho yangu ilianza kufifia taratibu na kadiri muda ulivyokuwa unazidi kusonga mbele ndivyo nayo ilivyozidi kufifia, japokuwa ilikuwa ni mchana, kigiza kikaanza kutanda kwenye macho yangu.

Nakumbuka neno la mwisho nililofanikiwa kulisema, ingawa ilikuwa ni kwa taabu kubwa kutokanana midomo yangu kuwa mizito, ilikuwa ni: Mungu nisaidie! Nikafumba macho na giza totoro likatawala kila sehemu, sikuelewa tena kilichoendelea baada ya hapo!

Katika hali ambayo sikuitegemea na ambayo mpaka leo huwa siwezi kuifafanua, muda mfupi baadaye nilijikuta nikizinduka lakini nikiwa kwenye hali ya tofauti kabisa. Nilizinduka nikiwa palepale nilipokuwa nimelala awali lakini katika hali ya ajabu, nilikuwa mwepesi sana.

Nikajikuta nikianza kupaa taratibu kuelekea juu. Nikiwa juu kidogo, niligeuka na kutazama pale nilipokuwa nimeangukia, nikashangaa kuona bado mwili wangu ulikuwa umelala palepale, damu nyingi zikiendelea kutoka kwenye jeraha la kifuani, tena safari hii zikitoka kwa mabongemabonge.

“Mungu wangu! Hiki ni kitu gani tena?” nilijikuta nikisema kwa sauti ya chini, ungeweza kudhani nilikuwa kwenye ndoto lakini haikuwa hivyo. Nilijiuliza kama mwili wangu bado ulikuwa pale chini, mimi niliyekuwa napaa nilikuwa ni nani?Sikupata majibu.

Niliendelea kupaa kuelekea juu mpaka nikafikia umbali wa mita kadhaa, ulioniwezesha kuona vizuri kila kitu kilichokuwa kinaendelea eneo la tukio. Niliwaona watuwakizidi kumiminika kwa wingi eneo la tukio, wengine wakishika vichwa vyao baada ya kuuona mwili wangu ukiwa kwenye hali ile.

Niliwaona watu kadhaa ambao nilikuwa nikiwafahamu wakiwa na nyuso za huzuni kali, wengine wakiangua vilio kwa nguvu. Nilimuona rafiki yangu na mfanyakazi mwenzangu ambaye muda mfupi kabla ya tukio nilikuwa naye, Justice akiwa analia kwa uchungu mno huku akilitaja jina langu.

Nilimuona pia Raya, msichana ambaye naye tulikuwa tukifanya naye kazi na ambaye alikuwa anapenda sana kuwa karibu na mimi ingawa mara kwa mara nilikuwa nikimkwepa (nitaeleza zaidi kuhusu msichana huyu baadaye), naweza kusema yeye ndiye aliyekuwa na hali mbaya kuliko watu wengine wote kwani alikuwa akilia kwa sauti ya juu huku akilitaja jina langu kiasi cha kusababisha muda mfupi baadaye aanguke na kupoteza fahamu.

Niliwaona pia baadhi ya watu wakiupiga picha mwili wangu kwa kutumia simu zao za mikononi, niliwaona pia waandishi kadhaa wa habari ambao nao walikuwa wakipiga picha nyingi eneo la tukio, za mnato na za video.

Muda mfupi baadaye, walifika askari wanne waliokuwa wamepakizana kwenye pikipiki mbili, maarufu kama tigo ambao niliwaona wakianza kuwarudisha watu nyuma kutoka pale mwili wangu ulipokuwa umelala.

Mmoja wao alisogea jirani kabisa, nikamuona akiuchunguza mwili wangu kisha akaugusa shingoni kama anayesikiliza mapigo ya moyo, nikamuona akiinuka na kuwasogelea wenzake, wakawa wanazungumza jambo ambalo sikuelewa ni nini. Mmoja akatoa simu ya upepo (radio call) na akawa anazungumza na upande wa pili.

Nikiwa bado naendelea kushangaa kwani kila kitu kilikuwa kigeni kwangu, nilianza kusikia ving’ora kwa mbali, nikakumbuka kwamba kabla sijapoteza fahamu kutokana na kutokwa na damu nyingi, nilivisikia tena ving’ora hivyo lakini tofauti yake ni kwamba sasa nilikuwa na uwezo wa kuona kila kilichokuwa kinaendelea.

Lilikuwa ni gari la kubebea wagonjwa (ambulance) ambalo lilikuwa likija kwa kasi eneo lile mwili wangu ulipokuwepo. Nyuma yake lilikuwa limeongozana na difenda ya polisi ambayo niliitambua kwa urahisi kutokana na namba zake za usajili na maandishi yaliyokuwa ubavuni yaliyosomeka ‘Police’.

Wale askari waliokuwepo eneo la tukio waliwatawanya watu upande ule ile ambulance ilikokuwa inatokea, gari likasogea mpaka jirani kabisa na pale mwili wangu ulipokuwepo.

Likasimama ambapo manesi wanne waliovalia nguo nyeupe waliteremka wakiwa na machela, sambamba na askari kadhaa waliokuwa kwenye ile difenda, wote wakasogea na kuuzunguka mwili wangu.

Wakasaidiana kuuinua mwili wangu pale chini na kuulaza kwenye machela kisha wakauingiza kwenye ambulance. Nilimuona Justice naye akipanda. Raya yeye alipakizwa kwenye lile gari la polisi akiwa hajitambui.

Gari likaondoka kwa kasi kubwa likifuatiwa na difenda kwa nyuma, wale askari wa pikipiki waliendelea kuwepo pale eneo la tukio kwa dakika kadhaa wakiwa makini kuwasikiliza watu walichokuwa wanakisema huku wakiwahoji wengine kadhaa.

Kwa muda wote huo, bado nilikuwa najiuliza kilichotokea bila kupata majibu, sikuelewa nipo kwenye hali gani kwa sababu kama ni mwili wangu, tayari ulishapakizwa kwenye ambulance na kukimbizwa hospitali lakini nilishangaa mimi bado nipo eneo lile nikielea angani.

Nilijiuliza ule mwili wangu unapelekwa wapi lakini pia sikupata majibu. Ghafla nilipata wazo la kuifukuzia ile ambulance ili nijue wanaupeleka wapi mwili wangu. Wazo nililoona linafaa, ilikuwa ni kushuka chini na kuchukua bodaboda kwani niliamini kutokana na foleni iliyokuwepo na kasi ya ambulance, ni usafiri huo pekee ndiyo unaoweza kuniwahisha.

Nilishuka jirani kabisa na pale mwili wangu ulipokuwepo muda mfupi uliopita, watu wakawa wameshaanza kutawanyika huku wengine wakijikusanya vikundivikundi pembeni na kujadiliana kuhusu kilichotokea. Nilimsikia mzee mmoja akiwaambia wenzake: “Kwa hali aliyonayo, hawezi kupona, lazima afe.”

Nikashtuka sana kusikia kauli hiyo kwa sababu sikujua wanamzungumzia nani kwamba lazima afe wakati mimi bado nilikuwa hai na nilikuwa nawasikia wanachokisema.

Sikutaka kupoteza muda, harakaharaka nilisogea pembeni ya barabara na kupunga mkono kusimamisha bodaboda, japokuwa dereva alikuwa akija upande wangu, nilishangaa akinipita kama hajaniona. Akaja wa pili naye licha ya kumpungia mkono kwa nguvu hakusimama, akanipita kwa kasi.

Nilijitazama vizuri mwilini kwani nilihisi huenda wanaogopa kusimama kutokana na mwili wangu kulowa damu lakini kituambacho pia nilishindwa kukielewa, shati nililokuwa nimevaa halikuwa na hata tone la damu. Lilikuwa ni shati lilelile ambalo mwili wangu wakati unatolewa eneo lile lilikuwa halitamaniki kwa damu.

Nilishindwa kuelewa ni nini hasa kimetokea, nikajitazama vizuri mwili wangu na kugundua kwamba ulikuwa na hali fulani kama ya kung’aa kusiko kwa kawaida, nilijishika pale kifuani lakini hapakuwa na alama kwamba nilikuwa nimejeruhiwa vibaya, nikazidi kuchanganyikiwa.

Ilibidi nisogee mpaka kwenye maegesho ya bodaboda nikiamini pale itakuwa rahisi kuzungumza na dereva yoyote ili aniwahishe kabla ile ambulance haijapotea kabisa.

Nilipopiga hatua moja nilijiona kuwa mwepesi sana halafu tambo lilikuwa refu sana tofauti na kawaida. Sehemu ambayo ningetembea hata hatua ishirini, nilipiga hatua mbili tu, nikawa nimeshafika pale kwenye bodaboda.

Je, nini kitafuatia? Usikose
Good story
 
SEVEN DAYS IN HELL (SIKU SABA KUZIMU)

Episode-1

Damu nyingi zilikuwa zinanitoka upande wa kushoto wa kifua changu kiasi cha kunifanya nilowe chapachapa. Nilijitahidi kuinuka pale nilipokuwa nimelala huku damu nyingi zikiendelea kunitoka lakini maumivu makali yalinirudisha chini.


Kwa kutumia mikono yangu miwili, nilijaribu kuminya pale kwenye jeraha kubwa ili kuzuia damu isiendelee kunimwagika lakini nilijikuta mikono ikikosa nguvu, kadiri muda ulivyokuwa unasonga mbele ndivyo nilivyokuwa nazidi kuishiwa nguvu.

Watu wengi walianza kukimbilia pale nilipokuwa nimeanguka na kunizunguka, niliwasikia wengine wakishindwa kuficha hisia zao na kuanza kuangua vilio wakilitaja jina langu. Nadhani hali waliyoniona nayo iliwafanya waamini kwamba siwezi kabisa kupona kutokana na damu zilivyokuwa zinaendelea kunimwagika mithili ya bomba lililopasuka.

Nikiwa kwenye maumivu makali, nilijigeuza na kuanza kutazama angani, upeo wa macho yangu ukagota kwenye mawingu meupe na ya bluu yaliyokuwa yakilipendezesha anga, nikabaki nimetulia nikiwa kwenye hali hiyo.

Kelele za watu wengi waliokuwa wanazidi kuongezeka eneo la tukio kunishangaa, zilianza kupungua taratibu masikioni mwangu, zikazidi kupungua na baadaye nikawa nasikia kama watu wananong’ona. Kwa mbali nilisikia mlio wa ving’ora ambavyo hata hivyo sikujua ni vya nini.

Nikiwa naendelea kutazama angani, taswira ndani ya mboni za macho yangu ilianza kufifia taratibu na kadiri muda ulivyokuwa unazidi kusonga mbele ndivyo nayo ilivyozidi kufifia, japokuwa ilikuwa ni mchana, kigiza kikaanza kutanda kwenye macho yangu.

Nakumbuka neno la mwisho nililofanikiwa kulisema, ingawa ilikuwa ni kwa taabu kubwa kutokanana midomo yangu kuwa mizito, ilikuwa ni: Mungu nisaidie! Nikafumba macho na giza totoro likatawala kila sehemu, sikuelewa tena kilichoendelea baada ya hapo!

Katika hali ambayo sikuitegemea na ambayo mpaka leo huwa siwezi kuifafanua, muda mfupi baadaye nilijikuta nikizinduka lakini nikiwa kwenye hali ya tofauti kabisa. Nilizinduka nikiwa palepale nilipokuwa nimelala awali lakini katika hali ya ajabu, nilikuwa mwepesi sana.

Nikajikuta nikianza kupaa taratibu kuelekea juu. Nikiwa juu kidogo, niligeuka na kutazama pale nilipokuwa nimeangukia, nikashangaa kuona bado mwili wangu ulikuwa umelala palepale, damu nyingi zikiendelea kutoka kwenye jeraha la kifuani, tena safari hii zikitoka kwa mabongemabonge.

“Mungu wangu! Hiki ni kitu gani tena?” nilijikuta nikisema kwa sauti ya chini, ungeweza kudhani nilikuwa kwenye ndoto lakini haikuwa hivyo. Nilijiuliza kama mwili wangu bado ulikuwa pale chini, mimi niliyekuwa napaa nilikuwa ni nani?Sikupata majibu.

Niliendelea kupaa kuelekea juu mpaka nikafikia umbali wa mita kadhaa, ulioniwezesha kuona vizuri kila kitu kilichokuwa kinaendelea eneo la tukio. Niliwaona watuwakizidi kumiminika kwa wingi eneo la tukio, wengine wakishika vichwa vyao baada ya kuuona mwili wangu ukiwa kwenye hali ile.

Niliwaona watu kadhaa ambao nilikuwa nikiwafahamu wakiwa na nyuso za huzuni kali, wengine wakiangua vilio kwa nguvu. Nilimuona rafiki yangu na mfanyakazi mwenzangu ambaye muda mfupi kabla ya tukio nilikuwa naye, Justice akiwa analia kwa uchungu mno huku akilitaja jina langu.

Nilimuona pia Raya, msichana ambaye naye tulikuwa tukifanya naye kazi na ambaye alikuwa anapenda sana kuwa karibu na mimi ingawa mara kwa mara nilikuwa nikimkwepa (nitaeleza zaidi kuhusu msichana huyu baadaye), naweza kusema yeye ndiye aliyekuwa na hali mbaya kuliko watu wengine wote kwani alikuwa akilia kwa sauti ya juu huku akilitaja jina langu kiasi cha kusababisha muda mfupi baadaye aanguke na kupoteza fahamu.

Niliwaona pia baadhi ya watu wakiupiga picha mwili wangu kwa kutumia simu zao za mikononi, niliwaona pia waandishi kadhaa wa habari ambao nao walikuwa wakipiga picha nyingi eneo la tukio, za mnato na za video.

Muda mfupi baadaye, walifika askari wanne waliokuwa wamepakizana kwenye pikipiki mbili, maarufu kama tigo ambao niliwaona wakianza kuwarudisha watu nyuma kutoka pale mwili wangu ulipokuwa umelala.

Mmoja wao alisogea jirani kabisa, nikamuona akiuchunguza mwili wangu kisha akaugusa shingoni kama anayesikiliza mapigo ya moyo, nikamuona akiinuka na kuwasogelea wenzake, wakawa wanazungumza jambo ambalo sikuelewa ni nini. Mmoja akatoa simu ya upepo (radio call) na akawa anazungumza na upande wa pili.

Nikiwa bado naendelea kushangaa kwani kila kitu kilikuwa kigeni kwangu, nilianza kusikia ving’ora kwa mbali, nikakumbuka kwamba kabla sijapoteza fahamu kutokana na kutokwa na damu nyingi, nilivisikia tena ving’ora hivyo lakini tofauti yake ni kwamba sasa nilikuwa na uwezo wa kuona kila kilichokuwa kinaendelea.

Lilikuwa ni gari la kubebea wagonjwa (ambulance) ambalo lilikuwa likija kwa kasi eneo lile mwili wangu ulipokuwepo. Nyuma yake lilikuwa limeongozana na difenda ya polisi ambayo niliitambua kwa urahisi kutokana na namba zake za usajili na maandishi yaliyokuwa ubavuni yaliyosomeka ‘Police’.

Wale askari waliokuwepo eneo la tukio waliwatawanya watu upande ule ile ambulance ilikokuwa inatokea, gari likasogea mpaka jirani kabisa na pale mwili wangu ulipokuwepo.

Likasimama ambapo manesi wanne waliovalia nguo nyeupe waliteremka wakiwa na machela, sambamba na askari kadhaa waliokuwa kwenye ile difenda, wote wakasogea na kuuzunguka mwili wangu.

Wakasaidiana kuuinua mwili wangu pale chini na kuulaza kwenye machela kisha wakauingiza kwenye ambulance. Nilimuona Justice naye akipanda. Raya yeye alipakizwa kwenye lile gari la polisi akiwa hajitambui.

Gari likaondoka kwa kasi kubwa likifuatiwa na difenda kwa nyuma, wale askari wa pikipiki waliendelea kuwepo pale eneo la tukio kwa dakika kadhaa wakiwa makini kuwasikiliza watu walichokuwa wanakisema huku wakiwahoji wengine kadhaa.

Kwa muda wote huo, bado nilikuwa najiuliza kilichotokea bila kupata majibu, sikuelewa nipo kwenye hali gani kwa sababu kama ni mwili wangu, tayari ulishapakizwa kwenye ambulance na kukimbizwa hospitali lakini nilishangaa mimi bado nipo eneo lile nikielea angani.

Nilijiuliza ule mwili wangu unapelekwa wapi lakini pia sikupata majibu. Ghafla nilipata wazo la kuifukuzia ile ambulance ili nijue wanaupeleka wapi mwili wangu. Wazo nililoona linafaa, ilikuwa ni kushuka chini na kuchukua bodaboda kwani niliamini kutokana na foleni iliyokuwepo na kasi ya ambulance, ni usafiri huo pekee ndiyo unaoweza kuniwahisha.

Nilishuka jirani kabisa na pale mwili wangu ulipokuwepo muda mfupi uliopita, watu wakawa wameshaanza kutawanyika huku wengine wakijikusanya vikundivikundi pembeni na kujadiliana kuhusu kilichotokea. Nilimsikia mzee mmoja akiwaambia wenzake: “Kwa hali aliyonayo, hawezi kupona, lazima afe.”

Nikashtuka sana kusikia kauli hiyo kwa sababu sikujua wanamzungumzia nani kwamba lazima afe wakati mimi bado nilikuwa hai na nilikuwa nawasikia wanachokisema.

Sikutaka kupoteza muda, harakaharaka nilisogea pembeni ya barabara na kupunga mkono kusimamisha bodaboda, japokuwa dereva alikuwa akija upande wangu, nilishangaa akinipita kama hajaniona. Akaja wa pili naye licha ya kumpungia mkono kwa nguvu hakusimama, akanipita kwa kasi.

Nilijitazama vizuri mwilini kwani nilihisi huenda wanaogopa kusimama kutokana na mwili wangu kulowa damu lakini kituambacho pia nilishindwa kukielewa, shati nililokuwa nimevaa halikuwa na hata tone la damu. Lilikuwa ni shati lilelile ambalo mwili wangu wakati unatolewa eneo lile lilikuwa halitamaniki kwa damu.

Nilishindwa kuelewa ni nini hasa kimetokea, nikajitazama vizuri mwili wangu na kugundua kwamba ulikuwa na hali fulani kama ya kung’aa kusiko kwa kawaida, nilijishika pale kifuani lakini hapakuwa na alama kwamba nilikuwa nimejeruhiwa vibaya, nikazidi kuchanganyikiwa.

Ilibidi nisogee mpaka kwenye maegesho ya bodaboda nikiamini pale itakuwa rahisi kuzungumza na dereva yoyote ili aniwahishe kabla ile ambulance haijapotea kabisa.

Nilipopiga hatua moja nilijiona kuwa mwepesi sana halafu tambo lilikuwa refu sana tofauti na kawaida. Sehemu ambayo ningetembea hata hatua ishirini, nilipiga hatua mbili tu, nikawa nimeshafika pale kwenye bodaboda.

Je, nini kitafuatia? Usikose
Ok
 
Haijalishi umecopy au umeiba, iendeleze kaka imefika patamu. Pliz nitag ukiendelea.
 
Back
Top Bottom