Wale wanaosema kwa nini kipande cha Dar-Moro hakijakamilika halafu bado tuna launch kuelekea Rwanda, muelewe kuwa hii reli inajengwa parallel, aim ni kumaliza kwa muda mfupi. Na ndio maana while kipande cha Dar-Moro hakijakamilika, tayari Moro-Makutupora wanaanza ujenzi, by the time reli imefika Moro, inaungwa moja kwa moja kuelekea Dodoma.
Hii reli haijengwi kama nyumba.. unaanza msingi then unaenda upward. This is the best approach so far.. na kama Kenya by the time mmeanza Mombasa mngekuwa mnajenga Nairobi-Naivasha ina maana leo hii mngekuwa tayari mnaelekea Uganda. Na kama Uganda wangekuwa serious, basi by 2022 reli ingekuwa imeshafika Sudan Kusini.
Bottom line hizi reli zinatusaidia sisi sote, Nchi zinazotuzunguka zinatutegemea na ili maendeleo ya Afrika Mashariki yaende mbele ni lazima tuwe na usafiri bora..