ANCIENT FROM EGYPT
JF-Expert Member
- Oct 24, 2015
- 927
- 1,136
Tawi la WanaYanga Wilayani Sikonge, Mkoani Tabora Wameondokewa na shabiki wao aliyekuwa na mapenzi ya dhati na Timu ya Yanga ambaye alifarikia siku ya jana katika ajali ya basi iliyotokea wilayani Sikonge.
Mwanamama huyo aliyefahamika na wengi kwa jina la Rebeca Miyeye, alikuwa shabiki kindakindaki wa Timu ya Yanga wilayani Sikonge na Tabora Kwa ujumla.
Enzi za uhai wake Bi Rebeca alifahamika kama shabiki wa Yanga mwenye mbwembwe nyingi sana hasa pale anapokutana na watani wa jadi. Na ndipo watu walipompa jina la "Mama Wa Yanga"
Natoa pole kwa familia pamoja na ndugu na jamaa waliofikwa na Msiba Huo.
NB: Samahani sana, Sina habari Za Kina juu ya Ajali hiyo ya Basi ambayo ilitokea jana.
Mwanamama huyo aliyefahamika na wengi kwa jina la Rebeca Miyeye, alikuwa shabiki kindakindaki wa Timu ya Yanga wilayani Sikonge na Tabora Kwa ujumla.
Enzi za uhai wake Bi Rebeca alifahamika kama shabiki wa Yanga mwenye mbwembwe nyingi sana hasa pale anapokutana na watani wa jadi. Na ndipo watu walipompa jina la "Mama Wa Yanga"
Natoa pole kwa familia pamoja na ndugu na jamaa waliofikwa na Msiba Huo.
NB: Samahani sana, Sina habari Za Kina juu ya Ajali hiyo ya Basi ambayo ilitokea jana.