Shahada ya uzamili udom haitambuliki?

ng'wabuki

Member
Joined
Oct 27, 2011
Posts
80
Reaction score
4
Kwa muda sasa wahadhiri waliohitimu masomo yao ya shahada ya pili na kupandishwa madaraja yao kitaaluma na chuo. Cha kusikitisha ni kuwa wahadhiri hao wana mwaka mzima sasa hawajalipwa mshahara wa ngazi yao mpya na yamekuwepo majibu yasiyoeleweka juu ya malipo hayo japo chuo chao kinadai kilishatuma madai yao ya mshahara huo mpya hazina, wizara ya elimu na ofisi ya rais utumishi.

Swali hapa je ndo kusema taifa kupitia wizara ya elimu limewapotezea muda wao wahadhiri hao kusoma shahada ya pili chuoni hapo nakuona hawastahili kulipwa madai au mshahara wao huo mpya? Ama hazina, utumishi na elimu mnataka walimu hawa wafanye nini waweze kulipwa stahiki zao wakati wao wanatumikia taifa bila kukopesha huduma yao kwa wanafunzi?

Inasikitisha sana kuona wahadhiri hawa hawajaliwi wakati wasomali na waimbizi wengine wanahudumiwa vizuri pasipo mchango wowote wa maana ukilinganisha na wataalamu hawa.

Mawaziri mkulo, Ghasia na Kawambwa mnataka mpewe nini na wahadhiri hawa muweze kulipa stahiki zao?
 
Kichwa cha habari kinaonyesha mtazamo hasi tu kwenye masters za udom kitu ambacho si cha kweli wala sio sababu ya wahadhiri kutolipwa nyongeza zao,tatizo ni urasimu tu katika mambo ya ya fedha ila mwisho wa siku watalipwa pamoja na malimbikizo yao
 

Badilisha HEADING
 
Basi tutemane naye, japo tatizo la kupanshisha daraja na kulipwa kiwango cha mshahara stahiki ni tatizo kila sector ya serikali (polisi, walimu, manesi n.k)
ana nia ya kupotosha watu
 
content na kichwa cha habari haviendani
 
Umangimeza wizarani umesabisha kipato chenu kisitune.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…