Donatila
JF-Expert Member
- Oct 23, 2014
- 7,772
- 22,598
SHAHIDI upande wa serikali kesi ya Wema Sepetu kutuhumiwa kutumia madawa ya kulevya amesema msokoto wa bangi ulikutwa ukiwa kabatini jikoni kwake.
Hayo yamesemwa na ofisa wa ofisi ya Mkuu wa Upelelezi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Inspekta Willy akimweleza Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba, wakati akiongozwa na Wakili wa Serikali, Constantine Kakula.
Inspekta Willy anakumbuka Februari 4, mwaka huu aliitwa na mkuu wake wa kazi na kupewa jukumu la kufanya upekuzi nyumbani kwa Wema Sepetu ambapo aliongozana na maofisa wenzake hadi nyumbani anakoishi huko Ununio jijini Dar es Salaam.
Alisema baada ya kufika nyumbani kwa Wema walimkuta mfanyakazi wake wa ndani wa kike ambaye walimuomba waonane na mjumbe wa shina wa maeneo hayo ambapo baada ya kufanikwa kumwona walimweleza shida yao na kuanza kazi ya uchunguzi ili kutafuta dawa za kulevya.
Aliongeza kwamba baada ya hapo walifanya uchunguzi ndani ya chumba cha wafanyakazi wa ndani wa kike, walikuta msokoto wa bangi uliotumika ndani ya kibiriti na baadaye walijaza hati ya ukamataji, kisha kuondoka na Wema hadi kituo cha polisi.
Aidha shahidi huyo aliiomba mahakama ipokee kielelezo hicho mbele ya Mahakama ambapo wakili wa utetezi, Peter Kibatala, alipinga kupokelewa kwa hati hiyo, akidai ina mapungufu ya kisheria. Kutokana na mvutano huo, Hakimu Simba ameahirisha kesi hiyo hadi kesho kwa ajili ya kutoà uamuzi wa kupokea kielelezo hicho ama la.
=======
Wema Sepetu kukamatwa na kuhukumiwa kwa kukutwa na madawa ya kulevya
- Wema Sepetu, Mr. Blue, TID, Recho wahusishwa na Dawa za Kulevya. Watakiwa kuripoti kituo cha Polisi
- Kamanda Siro: Wema Sepetu, TID na Nyandu Tozi bado wanashikiliwa na jeshi la polisi
- Sakata la Madawa ya Kulevya: Wema Sepetu afikishwa Mahakamani, apata dhamana
- Wema Sepetu kapatikana na bangi
- Tundu Lissu kumtetea Wema Sepetu
- Maajabu: Serikali haiwajui Vigogo wa Dawa za Kulevya hadi inataka Wema awatajie?
- Makonda kumfuata Wema mahabusu nyakati za usiku, hii imekaaje?
- Sauti ya Wema Sepetu iliyosambaa akiwatoa hofu Mashabiki
- Kesi ya Wema Sepetu hadi mwakani
- Wema Sepetu amefiwa, kesi yake yapigwa kalenda
- Dawa za Kulevya: Wema adai Makonda anatembea na Agnes Masogange ndio maana hakamatwi
- Wema Sepetu Apandishwa Tena Kizimbani Kisutu leo
- Vita ya Dawa za Kulevya: Steve Nyerere alivyopiga kambi Bungeni Kumuokoa Wema Sepetu
- Kesi ya Wema Sepetu yaahirishwa, uchunguzi haujakamilika
- Kutoka mahakamani: Wema Sepetu hakufanyiwa upekuzi kwenye maungo ya mwili wake, asema Hakimu
- Mkemia Mkuu: Mkojo wa Wema Sepetu ulikuwa na bangi
- Kibatala aandika barua ya kujitoa kesi ya Wema Sepetu, Alberto Msando aandika barua ya kuwa wakili mpya
- KISUTU: Wema Sepetu afika na Wakili wake Msando kwenye kesi. Diamond na Hamisa nao wafika Mahakama ya watoto
- Shahidi kesi ya Wema asema bangi ilikutwa jikoni
- Kisutu: Korti yakataa vielelezo vya ushahidi kesi ya Wema Sepetu. Masogange akutwa na kesi ya kujibu
Kuhukumiwa na kuachiwa huru baada ya kulipa faini