SHAIRI: Janga la kubeti

SHAIRI: Janga la kubeti

MakaDik

JF-Expert Member
Joined
May 31, 2019
Posts
239
Reaction score
136
SHAIRI
JANGA LA KUBETI

1. Kipo kilio cha wazi, kingine kimefichika
Mfano kuchunwa buzi, huwezi wazi kuweka
Kwetu kama fumanizi, kilio kimetufika
Kubeti nalo ni janga, limeteka watu wengi

2. Kubeti nalo ni janga, limeteka watu wengi
Watu waishiwa mwanga, kama walao milungi
Mwovu katupiga Chenga, tena kwa yetu shilingi
Kubeti nalo ni janga, limeteka watu wengi

3. Janga sio kwa mmoja, limegusa kila kundi
Unapotaka kuchuja, wengi wetu ni mafundi
Hazina nyingi zavuja, kwa kupoteza Paundi
Kubeti nalo ni janga limeteka watu wengi

4.Wafanyao biashara, Watumishi serikali
Visiwani hata bara, wengi tumelala chali
Ingawaje inakera, bado twaiona dili
Kubeti nalo ni Janga limeteka watu wengi

5. Taasisi watu wake, nazo zimeingiliwa
Watu wafanya makeke, kubeti wamechaguwa
Mtu binafusi yake, nae anasumbuliwa
Kubeti nalo ni Janga limeteka watu wengi

6. Wengi tumewapoteza, sababu kubwa kubeti
Puresha walizikuza, mwisho zikawataiti
Vijana wanaongoza, kwenye simu wanabeti
Kubeti nalo ni janga limeteka watu wengi

7. Ndoa nazo ziko hoi, kubeti chanzo kamili
Vyuoni wasijidai, kubeti kumeshamili
Imeondoka nishai, hofu pia na kujali
Kubeti nalo ni janga limeteka watu wengi

8. Ni Kati ya watu mia, moja aweza kupata
Wengine wataumia, kwa kuugonga ukuta
Wazazi twatazamia, mzizi huu kukata
Kubeti nalo ni janga limeteka watu wengi

9. Taasisi za kidini, serikali saidia
Bebeni hii huzuni, kizazi kukiokoa
Njia nzuri kuzibuni, majibu kutupatia
Kubeti nalo ni janga limeteka watu wengi

10. Beti kumi zinatosha, kufungua maelufu
Na kama nimepotosha, mnichape maradufu
Hujaelewa kausha, usikomenti uchafu
Mungu wetu tuokoe, epusha kilio hiki
 
Sijasoma lote ila ni kweli kabisa...
Hili ni janga la Taifa
 
Yaani umekosa majanga mengine kama ccm,ukimwi,joto,mbu,uchawa ila ukaamua uje na betting kweli!!!!!
 
Yaani umekosa majanga mengine kama ccm,ukimwi,joto,mbu,uchawa ila ukaamua uje na betting kweli!!!!!
😳😳Ambalo hujaliona kama janga mimi nimelichagua kujulisha kuwa nalo ni janga🤣
 
Back
Top Bottom