SHAIRI: Jibu la Bi Khadija Kopa 'Jimbo liko wazi tangu Mume wangu afariki, Mjumbe akija lazima awe na Umri Mkubwa'

SHAIRI: Jibu la Bi Khadija Kopa 'Jimbo liko wazi tangu Mume wangu afariki, Mjumbe akija lazima awe na Umri Mkubwa'

Joined
Sep 12, 2018
Posts
34
Reaction score
27
1. Habari afikishiwe, miye Mzenji mwenziwe.
Haliendi kwenginiwe, hilo ni langu mwenyewe.
Upesi nikubaliwe, umri tabu isiwe.
"Huyu namtaka mimi, nimrudishe nyumbani"

2. Nina wengi marafiki, wajuzi wa Aisiti (ICT) .
Yeye kwa kummiliki, tutabadilisha cheti.
Sitini ngo itiki, nisimpe gatigati.
"Huyu namtaka mimi, nimrudishe nyumbani"

3. Urithi wa nyumba yangu, tamuandikia yeye.
Na kila kilicho changu, kitakuwa chake yeye.
Akitaka roho yangu, niradhi apewe yeye.
"Huyu namtaka mimi, nimrudishe nyumbani"

4. Yote hayo aambiwe, siwezi bila ya yeye.
Nimekumbwa na kiwewe, yote sababu ni yeye.
Ni busara niambiwe, ni chizi miye kwa yeye[emoji1787]
"Huyu namtaka mimi, nimrudishe nyumbani"

5. Ombi likikubalika, tagawa kwa nyote pesa.
Mji hautakalika, Foro hadi Mambosasa.
Biriani kadhalika, Malti za bakharesa.
"Huyu namtaka mimi, nimrudishe nyumbani"

Shairi limetungwa na kuandikwa na HMH, Unguja - Zanzibar.
 
1. Habari afikishiwe, miye Mzenji mwenziwe.
Haliendi kwenginiwe, hilo ni langu mwenyewe.
Upesi nikubaliwe, umri tabu isiwe.
"Huyu namtaka mimi, nimrudishe nyumbani"

2. Nina wengi marafiki, wajuzi wa Aisiti (ICT) .
Yeye kwa kummiliki, tutabadilisha cheti.
Sitini ngo itiki, nisimpe gatigati.
"Huyu namtaka mimi, nimrudishe nyumbani"

3. Urithi wa nyumba yangu, tamuandikia yeye.
Na kila kilicho changu, kitakuwa chake yeye.
Akitaka roho yangu, niradhi apewe yeye.
"Huyu namtaka mimi, nimrudishe nyumbani"

4. Yote hayo aambiwe, siwezi bila ya yeye.
Nimekumbwa na kiwewe, yote sababu ni yeye.
Ni busara niambiwe, ni chizi miye kwa yeye[emoji1787]
"Huyu namtaka mimi, nimrudishe nyumbani"

5. Ombi likikubalika, tagawa kwa nyote pesa.
Mji hautakalika, Foro hadi Mambosasa.
Biriani kadhalika, Malti za bakharesa.
"Huyu namtaka mimi, nimrudishe nyumbani"

Shairi limetungwa na kuandikwa na HMH, Unguja - Zanzibar.
Haya wazee wa pwani kajichomekeni muimbiwe mashairi
 
Na kwayo ukitaraji, inatesa nakwambia.
Utalizwa mfanyaji, hamu itakukimbia.
Acha ulazimishaji, hasa kwa jambo la ndoa.
Ni heri kuomba dua, kupata hilo hitaji.

Maguvu sio mtaji, kisa wataka kuoa.
Hadija ni msemaji, tena atakuumbua.
Yule mama mkanyaji, tena bingwa kabobea.
Aheri uombe dua, Kupata hilo hitaji.

Ungetaka mfanyaji, kimya ungemuendea.
Ukampa makulaji, na vingi kumvutia.
Na usiwe mjuaji, ukae kwa kutulia.
Aheri uombe dua, Kupata hilo hitaji.

Nakuasa muoaji, jaribu kuangalia.
Pengo lataka magwiji, wewe bado nakwambia.
Kwasasa marefu maji, huwezi kuogelea.
Hata uwe na kibwaji, kwa pale hutatoboa.
 
1. Habari afikishiwe, miye Mzenji mwenziwe.
Haliendi kwenginiwe, hilo ni langu mwenyewe.
Upesi nikubaliwe, umri tabu isiwe.
"Huyu namtaka mimi, nimrudishe nyumbani"

2. Nina wengi marafiki, wajuzi wa Aisiti (ICT) .
Yeye kwa kummiliki, tutabadilisha cheti.
Sitini ngo itiki, nisimpe gatigati.
"Huyu namtaka mimi, nimrudishe nyumbani"

3. Urithi wa nyumba yangu, tamuandikia yeye.
Na kila kilicho changu, kitakuwa chake yeye.
Akitaka roho yangu, niradhi apewe yeye.
"Huyu namtaka mimi, nimrudishe nyumbani"

4. Yote hayo aambiwe, siwezi bila ya yeye.
Nimekumbwa na kiwewe, yote sababu ni yeye.
Ni busara niambiwe, ni chizi miye kwa yeye[emoji1787]
"Huyu namtaka mimi, nimrudishe nyumbani"

5. Ombi likikubalika, tagawa kwa nyote pesa.
Mji hautakalika, Foro hadi Mambosasa.
Biriani kadhalika, Malti za bakharesa.
"Huyu namtaka mimi, nimrudishe nyumbani"

Shairi limetungwa na kuandikwa na HMH, Unguja - Zanzibar.
Utamfaa kwenye kutunga nyimbo zake!
 
1. Habari afikishiwe, miye Mzenji mwenziwe.
Haliendi kwenginiwe, hilo ni langu mwenyewe.
Upesi nikubaliwe, umri tabu isiwe.
"Huyu namtaka mimi, nimrudishe nyumbani"

2. Nina wengi marafiki, wajuzi wa Aisiti (ICT) .
Yeye kwa kummiliki, tutabadilisha cheti.
Sitini ngo itiki, nisimpe gatigati.
"Huyu namtaka mimi, nimrudishe nyumbani"

3. Urithi wa nyumba yangu, tamuandikia yeye.
Na kila kilicho changu, kitakuwa chake yeye.
Akitaka roho yangu, niradhi apewe yeye.
"Huyu namtaka mimi, nimrudishe nyumbani"

4. Yote hayo aambiwe, siwezi bila ya yeye.
Nimekumbwa na kiwewe, yote sababu ni yeye.
Ni busara niambiwe, ni chizi miye kwa yeye[emoji1787]
"Huyu namtaka mimi, nimrudishe nyumbani"

5. Ombi likikubalika, tagawa kwa nyote pesa.
Mji hautakalika, Foro hadi Mambosasa.
Biriani kadhalika, Malti za bakharesa.
"Huyu namtaka mimi, nimrudishe nyumbani"

Shairi limetungwa na kuandikwa na HMH, Unguja - Zanzibar.

"Penye nia"
Penye nia kuna njia, welishasema zamani
Msemo nakumbukia, na yake pia thamani
Usjeikata tamaa, utajafika nyumbani
Penye nia pana njia, walishasema wahenga.

Fikisha wako ujumbe, ajuwe yalo moyoni
Pitia hata kwa jumbe, wake hapo mtaani
wajuwe nawe ni jembe, hunao pia utani
Penye nia pana njia, walishasema wahenga!

Tamaa usiikate, ujiulize kwa nini?
Utamvisha na pete, hapo kwake kidoleni
mapenzi ni kama kete, akili yako kichwani
Penye nia pana njia, walshasema wahenga!

Waliyosema wahenga, ingawaje ni zamani
Ni ukweli si ujinga, na wala siyo utani
Jitoe pia muhanga, kujiingiza penzini
Penye nia pana njia, walishasema zamani

Wakatabahu waraka, hapa kwangu kituoni
Tena fanya kwa haraka, uyatowe ya moyoni
kama kweli wamtaka, akutiye akilini
Penye nia kuna njia, walishasema zamani!!

Wakatabahu,


Choveki
 
Back
Top Bottom