Idd Ninga
JF-Expert Member
- Nov 18, 2012
- 5,497
- 4,775
Mchakato wa katiba bado unaendele na huu ni ujumbe wangu kwa leo.
1.CCM na UKAWA,mbona mwazidi vutana ?.
Bado mambo hayajawa,mnaanza kamatana.
Mtaweza kutugawa,na nchi mtaichana.
Tusitumie vibaya, mchakato wa katiba.
2.Tujenge katiba njema,ya nchi siyo siasa.
Tuijenge nchi njema,na tuipige msasa.
Mtapo fanya wema,mtadumu kama kasa.
3.Wananchi tunataka,katiba yenye maana.
Wala siyo takataka,na vurugu ziso maana.
Ubabe mkiutaka,mtaipata laana.
Tusitumie vibaya,mchakato wa katiba.
4.Katiba tukiijenga,sote tutaja fadika.
Katiba tusipojenga,sote hatutaja cheka.
Na kama tukijitenga,mataifa yatacheka.
Tusitumie vibaya,mchakato wa katiba.
5.Ubabe kufanyiana,siyo jambo la maana
vitisho kutoleana,ni mwanzo wa kuachana.
Kwa hoja tukishindana,tutakuja kupatana.
Tusitumie vibaya, mchakato wa katiba.
Tumuombe mungu kama watanzania,tupate katiba bila ya mabaya yoyote.
1.CCM na UKAWA,mbona mwazidi vutana ?.
Bado mambo hayajawa,mnaanza kamatana.
Mtaweza kutugawa,na nchi mtaichana.
Tusitumie vibaya, mchakato wa katiba.
2.Tujenge katiba njema,ya nchi siyo siasa.
Tuijenge nchi njema,na tuipige msasa.
Mtapo fanya wema,mtadumu kama kasa.
3.Wananchi tunataka,katiba yenye maana.
Wala siyo takataka,na vurugu ziso maana.
Ubabe mkiutaka,mtaipata laana.
Tusitumie vibaya,mchakato wa katiba.
4.Katiba tukiijenga,sote tutaja fadika.
Katiba tusipojenga,sote hatutaja cheka.
Na kama tukijitenga,mataifa yatacheka.
Tusitumie vibaya,mchakato wa katiba.
5.Ubabe kufanyiana,siyo jambo la maana
vitisho kutoleana,ni mwanzo wa kuachana.
Kwa hoja tukishindana,tutakuja kupatana.
Tusitumie vibaya, mchakato wa katiba.
Tumuombe mungu kama watanzania,tupate katiba bila ya mabaya yoyote.