funzadume
JF-Expert Member
- Jan 28, 2010
- 13,624
- 21,362
Hapo nilipo nalia sina pa kukimbilia
Mke kanikimbia na watoto kachukua
Sina pa kusemea dunia imeniinamia
Ndugu tusiwatenge wagonjwa wa UKIMWI
Nilipokuwa mzima, watu hawakunisema
si Rehema si Fatuma, ambao wanisakama
wanasema si mzima, utadhani wamenipima
Ndugu tusiwatenge wagonjwa wa UKIMWI
vipele vinanitoka, kujikuna nimechoka
najiona takataka, mwili unaninuka
kutembea ninataka, ila nguvu zimekata
Ndugu tusiwatenge wagonjwa wa UKIMWI
Hospitali nikienda, manesi wananiponda
basi nikitaka panda, nazuiliwa na konda
wajiona kama ganda, lililo njiapanda
Ndugu tusiwatenge wagonjwa wa UKIMWI
naomba wasamalia, mje kunisaidia
kifo chaninyemelea, kaburi lanililia
nuru yanipotea, fahamu zanikimbia
Ndugu tusiwatenge wagonjwa wa UKIMWI
nikienda maskani, wananiteta wahuni
wote hawanitamani, nimepoteza thamani
sitakiwi duniani, kwangu ni kaburini
Ndugu tusiwatenge wagonjwa wa UKIMWI
by Funzadume (mwana wa Washawasha)
Mke kanikimbia na watoto kachukua
Sina pa kusemea dunia imeniinamia
Ndugu tusiwatenge wagonjwa wa UKIMWI
Nilipokuwa mzima, watu hawakunisema
si Rehema si Fatuma, ambao wanisakama
wanasema si mzima, utadhani wamenipima
Ndugu tusiwatenge wagonjwa wa UKIMWI
vipele vinanitoka, kujikuna nimechoka
najiona takataka, mwili unaninuka
kutembea ninataka, ila nguvu zimekata
Ndugu tusiwatenge wagonjwa wa UKIMWI
Hospitali nikienda, manesi wananiponda
basi nikitaka panda, nazuiliwa na konda
wajiona kama ganda, lililo njiapanda
Ndugu tusiwatenge wagonjwa wa UKIMWI
naomba wasamalia, mje kunisaidia
kifo chaninyemelea, kaburi lanililia
nuru yanipotea, fahamu zanikimbia
Ndugu tusiwatenge wagonjwa wa UKIMWI
nikienda maskani, wananiteta wahuni
wote hawanitamani, nimepoteza thamani
sitakiwi duniani, kwangu ni kaburini
Ndugu tusiwatenge wagonjwa wa UKIMWI
by Funzadume (mwana wa Washawasha)