Shairi (la kubuni)

Shairi (la kubuni)

funzadume

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2010
Posts
13,624
Reaction score
21,362
Hapo nilipo nalia sina pa kukimbilia
Mke kanikimbia na watoto kachukua
Sina pa kusemea dunia imeniinamia
Ndugu tusiwatenge wagonjwa wa UKIMWI

Nilipokuwa mzima, watu hawakunisema
si Rehema si Fatuma, ambao wanisakama
wanasema si mzima, utadhani wamenipima
Ndugu tusiwatenge wagonjwa wa UKIMWI

vipele vinanitoka, kujikuna nimechoka
najiona takataka, mwili unaninuka
kutembea ninataka, ila nguvu zimekata
Ndugu tusiwatenge wagonjwa wa UKIMWI

Hospitali nikienda, manesi wananiponda
basi nikitaka panda, nazuiliwa na konda
wajiona kama ganda, lililo njiapanda
Ndugu tusiwatenge wagonjwa wa UKIMWI

naomba wasamalia, mje kunisaidia
kifo chaninyemelea, kaburi lanililia
nuru yanipotea, fahamu zanikimbia
Ndugu tusiwatenge wagonjwa wa UKIMWI

nikienda maskani, wananiteta wahuni
wote hawanitamani, nimepoteza thamani
sitakiwi duniani, kwangu ni kaburini
Ndugu tusiwatenge wagonjwa wa UKIMWI

by Funzadume (mwana wa Washawasha)
 
Pole sana funzadume, kwa hayo yaliyokupata,
Huo ndio uanaume, kuvumilia matata,
Umekanyaga umeme, mchana wa saa sita,
Japokuwa umenaswa, JF hatutakutenga.
 
Pole sana funzadume, kwa hayo yaliyokupata,
Huo ndio uanaume, kuvumilia matata,
Umekanyaga umeme, mchana wa saa sita,
Japokuwa umenaswa, JF hatutakutenga.

kila nikikohoa watu wanaziba pua
nikitaka kunyoa, vinyozi wanikimbia
sina pa kukimbilia, naijutia dunia
Ndugu tusiwatenge wagonjwa wa UKIMWI

nilipopata sijajua, maana ni nyingi njia
sindano za kuchangia , au nyembe kunyolea
ngono sikuzembea, mpira nilivalia
Ndugu tusiwatenge wagonjwa wa UKIMWI

jaribu nawe kupima, huenda si mzima
Kaburunye nimekusoma, asante kwa huruma
achana na kina Halima, watakuambukiza ngoma
Ndugu tusiwatenge wagonjwa wa UKIMWI
 
kila nikikohoa watu wanaziba pua
nikitaka kunyoa, vinyozi wanikimbia
sina pa kukimbilia, naijutia dunia
Ndugu tusiwatenge wagonjwa wa UKIMWI

nilipopata sijajua, maana ni nyingi njia
sindano za kuchangia , au nyembe kunyolea
ngono sikuzembea, mpira nilivalia
Ndugu tusiwatenge wagonjwa wa UKIMWI

jaribu nawe kupima, huenda si mzima
Kaburunye nimekusoma, asante kwa huruma
achana na kina Halima, watakuambukiza ngoma
Ndugu tusiwatenge wagonjwa wa UKIMWI


Hahahahaaa, umenikumbusha enzi zileeee:

Karudi baba mmoja, toka safari ya mbali,
kavimba yote mapaja, na kutetemeka mwili
watoto wake wakaja, ili kumtaka hali
wakataka na kauli, iwafae maishani

akatamka mgonjwa, ninaumwa kwelikweli
hata kama nikichanjwa, haitoki homa kali
roho naona yachinjwa, kifo kinanikabili
kama mnataka mali semeni niseme nini
 
Kilio unacholia,funza tumekisikia
Sina cha kukuambia,wewe sasa tangulia
Dua tutakuombea,peponi kwendatulia

Watoto tutawalea,na mama yao pia
skuli wataingia,shaka hiyo ondoa
Ada tutawalipia,pasi na kwabagua

Masharubu ninalia,funzadume waondoka
Wapitutakimbilia,machozi yanatutoka
Jamvini Utapotea,yako yatasahaulika
 
Hahahahaaa, umenikumbusha enzi zileeee:

Karudi baba mmoja, toka safari ya mbali,
kavimba yote mapaja, na kutetemeka mwili
watoto wake wakaja, ili kumtaka hali
wakataka na kauli, iwafae maishani

akatamka mgonjwa, ninaumwa kwelikweli
hata kama nikichanjwa, haitoki homa kali
roho naona yachinjwa, kifo kinanikabili
kama mnataka mali semeni niseme nini
shuka mistari tuendelee na shairi letu
 
Kilio unacholia,funza tumekisikia
Sina cha kukuambia,wewe sasa tangulia
Dua tutakuombea,peponi kwendatulia

Watoto tutawalea,na mama yao pia
skuli wataingia,shaka hiyo ondoa
Ada tutawalipia,pasi na kwabagua

Masharubu ninalia,funzadume waondoka
Wapitutakimbilia,machozi yanatutoka
Jamvini Utapotea,yako yatasahaulika
nashukuru masharubu, umegonga sukurubu
kwa Muumba natubu, nawafuata mababu
jinsi navyopata tabu, kutokufa sina sababu
Ndugu tusiwatenge wagonjwa wa UKIMWI
 
Hongera Funzaadume naona sasa mtaanza kwenda sambamba na mwanakijiji na MJ1
 
shuka mistari tuendelee na shairi letu

Funzadume sikiliza, nikupe zangu nasaha
Ngono uliendekeza, ukadhania ni raha
kwa kweli umeteleza, imegeuka karaha
Pole sana mwanakwetu, kwa hayo yaliyokupata

Nakushauri mwenzangu, sasa hebu ugeuke
Atakusamehe Mungu, Kama ukitubu kwake
Ataondoa uchungu, hatakupiga mateke
Mungu husamehe dhambi, ukitubu kwa ukweli

Watafute walokole, wakufanyie maombi
Mwasema wana kelele, lakini hawana dhambi
Yamekutoka mapele, utapona kwa maombi
Mungu aponya ukimwi, hata wafu afufua

wamkumbuka jeska, yule dada wa haruna,
alikuwa mwathirika, kwa maombi amepona
jambo hili ni hakika, hata wewe utapona
hebu ufanye haraka, usiwe na moyo mgumu

hapa tamati nafika, nina majonzi moyoni
uchungu umenishika, hili ni balaa gani
funzadume wangu kaka, umenitia huzuni
Mungu akusaidie, upone ugonjwa wako
 
Funzadume sikiliza, nikupe zangu nasaha
Ngono uliendekeza, ukadhania ni raha
kwa kweli umeteleza, imegeuka karaha
Pole sana mwanakwetu, kwa hayo yaliyokupata

Nakushauri mwenzangu, sasa hebu ugeuke
Atakusamehe Mungu, Kama ukitubu kwake
Ataondoa uchungu, hatakupiga mateke
Mungu husamehe dhambi, ukitubu kwa ukweli

Watafute walokole, wakufanyie maombi
Mwasema wana kelele, lakini hawana dhambi
Yamekutoka mapele, utapona kwa maombi
Mungu aponya ukimwi, hata wafu afufua

wamkumbuka jeska, yule dada wa haruna,
alikuwa mwathirika, kwa maombi amepona
jambo hili ni hakika, hata wewe utapona
hebu ufanye haraka, usiwe na moyo mgumu

hapa tamati nafika, nina majonzi moyoni
uchungu umenishika, hili ni balaa gani
funzadume wangu kaka, umenitia huzuni
Mungu akusaidie, upone ugonjwa wako

shauri nimelipata, tatizo vipi tafika
kufika kwa katekista, nauli zahitajika
hela zimeshakata nakabiliwa ukata
Ndugu tusiwatenge wagonjwa wa UKIMWI
 
shauri nimelipata, tatizo vipi tafika
kufika kwa katekista, nauli zahitajika
hela zimeshakata nakabiliwa ukata
Ndugu tusiwatenge wagonjwa wa UKIMWI


Eneo la tanganyika, pekazi pale ya kawe
watu waliookoka, watakutoa kiwewe
usije kudanganyika, ukaelekea msewe
kama nauli ni shida, piga simu wakufate.

namba za simu nataja, ziandike kwa makini
sifuri saba sita moja, ile voda ya zamani,
ukipiga watakuja, wewe uwe na imani
dawa ya ukimwi moja, nayo ni jina la Yesu
 
Eneo la tanganyika, pekazi pale ya kawe
watu waliookoka, watakutoa kiwewe
usije kudanganyika, ukaelekea msewe
kama nauli ni shida, piga simu wakufate.

namba za simu nataja, ziandike kwa makini
sifuri saba sita moja, ile voda ya zamani,
ukipiga watakuja, wewe uwe na imani
dawa ya ukimwi moja, nayo ni jina la Yesu
imani inaponya, lakini kwangu hapana
gonjwa lanisakanya, siwezi hata kuona
nimekuwa kama nyanya, ningali bado kijana
Ndugu tusiwatenge wagonjwa wa UKIMWI
 
imani inaponya, lakini kwangu hapana
gonjwa lanisakanya, siwezi hata kuona
nimekuwa kama nyanya, ningali bado kijana
Ndugu tusiwatenge wagonjwa wa UKIMWI


Mungu wetu anaponya, funzadume sikiliza,
hata uwe kama nyanya, hili halitatiza,
amemponya matonya, juma na hata Aziza,
wewe nenda pale kawe, au wapigie waje
 
Mungu wetu anaponya, funzadume sikiliza,
hata uwe kama nyanya, hili halitatiza,
amemponya matonya, juma na hata Aziza,
wewe nenda pale kawe, au wapigie waje
simu nilishauza, nipate kujiuguza
kutembea kwanikwaza, nguvu nimepoteza
tumaini nimepoteza, nakufa mie funza
Ndugu tusiwatenge, wagonjwa wa UKIMWI
 
simu nilishauza, nipate kujiuguza
kutembea kwanikwaza, nguvu nimepoteza
tumaini nimepoteza, nakufa mie funza
Ndugu tusiwatenge, wagonjwa wa UKIMWI


Waelekeze nyumbani, kama simu umeuza
wamo humu jamvini, waje shetani kumchakaza

sema unaishi wapi, niliwalete maskani
wakaa mtaa upi, nieleze kwa umakini
watakuja na mshipi, wakutoe mautini
Jina la Yesu kiboko, funzadume uamini
 
Funzadume nimekuja, sio kukutia tabu
majibu ninayo ngoja, sio kukupa sulubu,
uliopata ugonjwa, haki unanipa tabu,
Gonjwa hilo la ukimwi, wapi ulilipatia?

Vyanzo vyake vingi kweli, kutwa hatwishwi ambiwa
wewe msema ukweli, chanzo wakijuulia
uliupata kwa mwali, au nao wezaliwa?
Gonjwa hilo la ukimwi, wapi ulilipatia?
 
Funzadume nimekuja, sio kukutia tabu
majibu ninayo ngoja, sio kukupa sulubu,
uliopata ugonjwa, haki unanipa tabu,
Gonjwa hilo la ukimwi, wapi ulilipatia?

Vyanzo vyake vingi kweli, kutwa hatwishwi ambiwa
wewe msema ukweli, chanzo wakijuulia
uliupata kwa mwali, au nao wezaliwa?
Gonjwa hilo la ukimwi, wapi ulilipatia?
siwezi kukupa jibu, wapi nilipopatia
labda kwenye ulabu, akili zilipotea
ushauri wa tabibu, kinga nilitumia
Ndugu tusiwatenge wagonjwa wa UKIMWI
 
Back
Top Bottom