Shairi la mapenzi

Shairi la mapenzi

Joined
May 6, 2019
Posts
9
Reaction score
4
Nipo Mbali:
Nipo mbali unajua,
Simu ndo kiunganishi,
Kwa nilicho kigundua,
Kukuwaza hakuniishi.

Najua unalijua,
Mwanamke ni stara,
Usije jishebedua,
Samaki msafi ukimpara.

Sio tu umevua,
Ukamtia jikoni,
Tumbo litakusumbua,
Usipende uhisani.

Nipo mbali ila hai,
Nitarudi hivi punde,
Ilinde yako nishai,
Isitolewe kwa punje.
 
USIPOMSIFIA:
Usipomsifia wewe,
Wapo wa kukusaidia,
Tena si kwa mayowe,
Jinale watamwita Dia.

Usiposifia chochote,
Umeshawapa ushindi,
Hata umvishe Pete,
Wanajiita wahindi.

Usipomsifia mkeo,
Unapunguza mapenzi,
Kwanza wavuliwa vyeo,
Wanaveshwa washenzi.

Kwanini usimsifu?
Acha umajinuni,
Mfanye mchangamfu,
Asikuone muhuni.

Kumsifia si kazi,
Hakuitaji gharama,
Ngoja nikuweke wazi,
Sifu epuka lawama.👨🏽‍🦯👨🏽‍🦯👨🏽‍🦯👨🏽‍🦯👨🏽‍🦯
 
Back
Top Bottom