SHAIRI LA MUYAKA Bin GHASSANY WA MOMBASA, KENYA.

SHAIRI LA MUYAKA Bin GHASSANY WA MOMBASA, KENYA.

Benson kaile

Member
Joined
Dec 15, 2013
Posts
7
Reaction score
1
Akutendeae Mema, Kushukuru ni lazima
Jaza ya mema ni mema, Maovu kutoyatia
Mbona umeghafilika? Kwa jambo lisilo shaka?
Shetani umemshika, Na kumuacha Nabia?
Unajifanya Mtesi, Kwa Mola wako Mkwasi
Unavitupa viasi, Sina la kukwambia
Silaha zote ni Zake, Wala na riziki Zake
Unakunywa maji Yake, Mbona umekosa haya?
Vita vyako fahamu, Havimdhuru Karimu
Ila wewe Bahaimu, Jijue Utaumia
Itunze yako fikara, Uwafikiri mabora
Wenye ngome na minara, Na panga za kuchinjia
Yatafakari mauti, Yeyote hayamuachi
Wala hayana wakati, Ghafla hukujilia
Yu wapi Firauni, Yu wapi Karuni
Na Shadadi maluuni, Wote wameangamia
Zao zilipokwisha, Ziraili kawafisha
Wameyawacha makasha, Na mambo haya na haya
Waimefika akhera, Madhalili mafukara
Uwapi wao bora, Wote umewakimbia
Kaburi zimewakaza, Hapana la kupumbaza
Kote kumefunga kiza, Adhabu kuwashukia
Adhabu hiyo ni kuu, Tena motoni kuwa juu
Majuto ni mjukuu, Tahadhari na dunia
Wapita na Siratini, Kuwangukia motoni
Kuteketea maini, Maisha kuteketea
Na yote ninayoyasema, Yatakufika lazima
Safari mbele na nyuma, Wengine hutangulia
 
Back
Top Bottom