Shairi mahiri: Tumbo unanidhalilisha!

Shairi mahiri: Tumbo unanidhalilisha!

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,137
Reaction score
17,908
Mwanangu leo amenitumia shairi. Ameliita 'shairi mahiri'. Linasomeka:

Tumbo nimezaliwa nawe,
Tumbo usinifanye nipagawe,
Tumbo usiniache mwenyewe,
Tumbo unanidhalilisha.

Tumbo mimi nimesoma,
Tumbo nimesaka maisha mema,
Tumbo nimefika utu uzima salama,
Tumbo unanidhalilisha.

Tumbo uanafanya nitamani,
Kupata kila kitu maishani,
Hata vile ambavyo haviwezekani,
Tumbo unanidhalilisha.

Tumbo unanifanya kuhama,
Kutoka chama hadi chama,
Unanisogeza karibu na karma,
Tumbo unanidhalilisha.

Tumbo unanipelekesha,
Usiku kucha nakesha,
Kupanga cha kuchekesha,
Tumbo unanidhalilisha.

Tumbo unanipotezea marafiki,
Sasa naonwa mnafiki,
Naimbwa hata kwenye muziki,
Tumbo unanidhalilisha.

Tumbo unafanya natengwa,
Na majungu kujengwa,
Nanyimwa hata machungwa,
Tumbo unalidhalilisha.

Sieleweki,
Siaminiki,
Sishauriki,
Tumbo unanidhalilisha.

Mambo ya expansion joints hayo!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
Naona Manenge anakula kwa macho..........achana kabisa na kitu kinaitwa Tumbo!!


21909468_1541814489195701_4981986072780079104_n.jpg
 
Ndio maana tumbo limekaa mbele lipewe kipaumbele.
 
Mwanangu leo amenitumia shairi. Ameliita 'shairi mahiri'. Linasomeka:

Tumbo nimezaliwa nawe,
Tumbo usinifanye nipagawe,
Tumbo usiniache mwenyewe,\
Tumbo unanidhalilisha.

Tumbo mimi nimesoma,
Tumbo nimesaka maisha mema,
Tumbo nimefika utu uzima salama,
Tumbo unanidhalilisha.

Tumbo uanafanya nitamani,
Kupata kila kitu maishani,
Hata vile ambavyo haviwezekani,
Tumbo unanidhalilisha.

Tumbo unanifanya kuhama,
Kutoka chama hadi chama,
Unanisogeza karibu na karma,
Tumbo unanidhalilisha.

Tumbo unanipelekesha,
Usiku kucha nakesha,
Kupanga cha kuchekesha,
Tumbo unanidhalilisha.

Tumbo unanipotezea marafiki,
Sasa naonwa mnafiki,
Naimbwa hata kwenye muziki,
Tumbo unanidhalilisha.

Tumbo unafanya natengwa,
Na majungu kujengwa,
Nanyimwa hata machungwa,
Tumbo unalidhalilisha.

Sieleweki,
Siaminiki,
Sishauriki,
Tumbo unanidhalilisha.

Mambo ya expansion joints hayo!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

Dah mzee wangu , ahsante kwa shairi murua, Shida ni tumbo hata si ubinadamu father.
 
Back
Top Bottom