GuDume
JF-Expert Member
- Jan 18, 2015
- 6,651
- 14,337
MIDEGE ISIYOLIWA HIYO NI MIDEGE GANI?
Midege isiyofugika, hiyo ni midege gani?
Moyo wahangaika,nitapa jibu gani
Mawazo kunifunika, yataniIsha lini
Midege isiyolika, hiyo ni kidege gani ?
Nimeona ndege wengi, tena wa kila rangi
Wana maumbo mengi, na sauti nyingi nyingi
Wenye kuruka kwa wingi, na mikiani vishungi
Midege isiyolika , hiyo ni midege gani ?
Nimefika kumburu, nikawaona kunguru
Nkaona wao wapo huru, walizunguka duru
Wanacheza zegeduru, hawana udhuru
Midege isiyolika, hiyo ni midege gani ?
Nmewaona kasuku , hawa hawaliki
Lakini si kama kuku, bei yao haishikiki
Wanaleta mtafaruku, kwa sauti lukuki
Midege isiyofugika, hiyo ni midege gani ?
Nawajua bata, nikiwaona wanapita
Hao utawapata, si kila mtaa ukipita
Nyie mnaokula bata, utamu gani mwapata!
Midege isiyolika, hiyo ni midege gani ?
Kuna hawa chiriku, wao si kama kasuku
Muulize mama chiku, usimwulize chausiku
Atakwambia njoo huku,nikondoe shauku
Midege isiyolika ,hiyo ni midege gani ?
Nmewakumbuka kanga, niliwaona kwa luhanga
Hawa ni kama wakunga, watamba chini na anga
Wao wamejipanga, kuyakabili majanga
Midege isiyofugika , hiyo ni midege gani ?
Midege isiyofugika, hiyo ni midege gani?
Moyo wahangaika,nitapa jibu gani
Mawazo kunifunika, yataniIsha lini
Midege isiyolika, hiyo ni kidege gani ?
Nimeona ndege wengi, tena wa kila rangi
Wana maumbo mengi, na sauti nyingi nyingi
Wenye kuruka kwa wingi, na mikiani vishungi
Midege isiyolika , hiyo ni midege gani ?
Nimefika kumburu, nikawaona kunguru
Nkaona wao wapo huru, walizunguka duru
Wanacheza zegeduru, hawana udhuru
Midege isiyolika, hiyo ni midege gani ?
Nmewaona kasuku , hawa hawaliki
Lakini si kama kuku, bei yao haishikiki
Wanaleta mtafaruku, kwa sauti lukuki
Midege isiyofugika, hiyo ni midege gani ?
Nawajua bata, nikiwaona wanapita
Hao utawapata, si kila mtaa ukipita
Nyie mnaokula bata, utamu gani mwapata!
Midege isiyolika, hiyo ni midege gani ?
Kuna hawa chiriku, wao si kama kasuku
Muulize mama chiku, usimwulize chausiku
Atakwambia njoo huku,nikondoe shauku
Midege isiyolika ,hiyo ni midege gani ?
Nmewakumbuka kanga, niliwaona kwa luhanga
Hawa ni kama wakunga, watamba chini na anga
Wao wamejipanga, kuyakabili majanga
Midege isiyofugika , hiyo ni midege gani ?