ramadhani kimweri
Senior Member
- Apr 22, 2016
- 181
- 179
NIMEZICHOKA DHARAU
Ni kheri niende zangu, sababu umenichoka
Wateseka moyo wangu, nimezichoka dhihaka
Wazarau pendo langu, ya nini kutaabika
Japo bado nakupenda, nimezichoka dharau.
Nimechoka kuziona, kebehi, dharau zako
Waona sina maana, thamani yangu haiko
matusi kunitukana, naonekana kicheko
japo bado nakupenda, zimenichosha dharau.
Bora nipate mwingine, nijifosi kumpenda
Atanipenda pengine, na pia akanilinda
na maumivu yapone, niepuke zako shida
Nisahau kukupenda, nifurahi angalau
[emoji2398]Ibn kimweri
ramadhanikimweri07@gmail.com
Kusoma mashairi mengine bofya Shairi: Hakuna siri tena
Ni kheri niende zangu, sababu umenichoka
Wateseka moyo wangu, nimezichoka dhihaka
Wazarau pendo langu, ya nini kutaabika
Japo bado nakupenda, nimezichoka dharau.
Nimechoka kuziona, kebehi, dharau zako
Waona sina maana, thamani yangu haiko
matusi kunitukana, naonekana kicheko
japo bado nakupenda, zimenichosha dharau.
Bora nipate mwingine, nijifosi kumpenda
Atanipenda pengine, na pia akanilinda
na maumivu yapone, niepuke zako shida
Nisahau kukupenda, nifurahi angalau
[emoji2398]Ibn kimweri
ramadhanikimweri07@gmail.com
Kusoma mashairi mengine bofya Shairi: Hakuna siri tena