ramadhani kimweri
Senior Member
- Apr 22, 2016
- 181
- 179
Siwezi kula makombo, ijapo niyakunona
Umesha jipaka shombo, siwezi kuramba tena
Yaliopita kitambo, yaliniumiza sana
Kurudi kwako siwezi, kurudi kudanganyana..
Kula nilichotapika, kwangu hilo ni haramu
Napaswa kukiepuka, hatakama ni kitamu
Yakwako nimetosheka, hayanipi hata hamu
Penzi lako la kishenzi, penzi la kudanganyana..
Bora niishi mpweke, sirudishi penzi lako
Lanifanya niteseke, siwezi kurudi kwako
Kheri nife wanizike, kuwa na wewe ni mwiko
Nataka sana mapenzi, lakini kwako hapana..
Donda ulonitonesha, nadhani halitopona
Ulonitenda yatosha, wala hamu sina tena
Yakwetu yameshakwisha, yaleo sio ya jana
Kuwa na wewe siwezi, yatosha niloyaona..
Sasa hivi sikupendi, nilikupenda zamani
Nakutoa kwenye kundi, la watu wenye thamani
Nawaza kile kipindi, kwangu ulikosa nini
Ukanitoa machozi, nikawa sina maana..
Kwaheri tena kwaheri, mie ninaenda zangu
Na kurejea sikiri, hiyo si tabia yangu
Kwako sirudi fedhuli, natunza heshima yangu
Kurudi kwako siwezi, kurudi kudanganyana..
[emoji2398]Ibn kimweri.
Ramadhanikimweri07@gmail.com
Mashairi mengine soma Shairi: Hakuna siri tena
Umesha jipaka shombo, siwezi kuramba tena
Yaliopita kitambo, yaliniumiza sana
Kurudi kwako siwezi, kurudi kudanganyana..
Kula nilichotapika, kwangu hilo ni haramu
Napaswa kukiepuka, hatakama ni kitamu
Yakwako nimetosheka, hayanipi hata hamu
Penzi lako la kishenzi, penzi la kudanganyana..
Bora niishi mpweke, sirudishi penzi lako
Lanifanya niteseke, siwezi kurudi kwako
Kheri nife wanizike, kuwa na wewe ni mwiko
Nataka sana mapenzi, lakini kwako hapana..
Donda ulonitonesha, nadhani halitopona
Ulonitenda yatosha, wala hamu sina tena
Yakwetu yameshakwisha, yaleo sio ya jana
Kuwa na wewe siwezi, yatosha niloyaona..
Sasa hivi sikupendi, nilikupenda zamani
Nakutoa kwenye kundi, la watu wenye thamani
Nawaza kile kipindi, kwangu ulikosa nini
Ukanitoa machozi, nikawa sina maana..
Kwaheri tena kwaheri, mie ninaenda zangu
Na kurejea sikiri, hiyo si tabia yangu
Kwako sirudi fedhuli, natunza heshima yangu
Kurudi kwako siwezi, kurudi kudanganyana..
[emoji2398]Ibn kimweri.
Ramadhanikimweri07@gmail.com
Mashairi mengine soma Shairi: Hakuna siri tena