Ibrambeya
Member
- Jul 25, 2014
- 36
- 2
Ziwe mbili au tatu, Hilo Bado mgogoto,
Nina mengi nawazua, wa kunifumbua hola,
Na hata akitokea, Heko yake nitampa,
Ziwe mbili au tatu; Serikali Tanzania?
Tume yake Warioba, Maoni ilikusanya,
Sampuli ikapata, Wenye hoja dadavua,
Kablasha kurundika, zikaitwa ni Rasimu
Ziwe mbili au tatu; Kwangu Bado ni utata.
Ubishi ukarandama, vikaibuka vihoja,
Ukawa na Tanzania; Mia mbili nae moja,
Midahalo imetanda, kuzimwaga zao fikra,
Ziwe mbili au tatu ; Ndio Msingi Katiba.
Ccm Upinzani, Ninataka Leo jibu,
Haja zenu nasikia, vikao nimeshiriki,
Mlitaja na gharama, na wengine kutengua,
Ziwe mbili au tatu; Pabaya Mtatufikisha.
Wananchi lalamika, usawa ati haupo,
Mara koti Muungano, Kuna mmoja kalivaa,
Ardhi nazo ajira, twadaiwa viparata,
Ziwe mbili au tatu; Changamoto tutanzue.
Wanazuoni kutanda, Midahalo kukamata,
Suluhu kuangazia, njia ipi tuipite,
Raisi akaibuka, hotuba zake katoa,
Ziwe mbili au tatu; Tuzitumie busara.
Kuna moja naliona, nathubutu kulisema,
Tanzania walalama, wasubiri tafuniwa,
Mchakato wa Katiba, tushiriki sisi sote,
Ziwe mbili au tatu; Ndio Roho ya Katiba.
Tusijesemea Ninge, maji yakisha mwagika,
Tunamuda kutanzua, sauti zetu zipaza,
Haijali unakotokea, Ipaze yako sauti,
Ziwe mbili au tatu; Pambana popote pale.
Mwenye jibu nipatie, mimi ubongo utandu,
Nimechoka tapatapa, kwa nyingi kauli mbiu,
Washairi mnijibu, Kijukuu chake Robert,
Ziwe mbili au tatu; Kalamu nimeishiwa!.
Nina mengi nawazua, wa kunifumbua hola,
Na hata akitokea, Heko yake nitampa,
Ziwe mbili au tatu; Serikali Tanzania?
Tume yake Warioba, Maoni ilikusanya,
Sampuli ikapata, Wenye hoja dadavua,
Kablasha kurundika, zikaitwa ni Rasimu
Ziwe mbili au tatu; Kwangu Bado ni utata.
Ubishi ukarandama, vikaibuka vihoja,
Ukawa na Tanzania; Mia mbili nae moja,
Midahalo imetanda, kuzimwaga zao fikra,
Ziwe mbili au tatu ; Ndio Msingi Katiba.
Ccm Upinzani, Ninataka Leo jibu,
Haja zenu nasikia, vikao nimeshiriki,
Mlitaja na gharama, na wengine kutengua,
Ziwe mbili au tatu; Pabaya Mtatufikisha.
Wananchi lalamika, usawa ati haupo,
Mara koti Muungano, Kuna mmoja kalivaa,
Ardhi nazo ajira, twadaiwa viparata,
Ziwe mbili au tatu; Changamoto tutanzue.
Wanazuoni kutanda, Midahalo kukamata,
Suluhu kuangazia, njia ipi tuipite,
Raisi akaibuka, hotuba zake katoa,
Ziwe mbili au tatu; Tuzitumie busara.
Kuna moja naliona, nathubutu kulisema,
Tanzania walalama, wasubiri tafuniwa,
Mchakato wa Katiba, tushiriki sisi sote,
Ziwe mbili au tatu; Ndio Roho ya Katiba.
Tusijesemea Ninge, maji yakisha mwagika,
Tunamuda kutanzua, sauti zetu zipaza,
Haijali unakotokea, Ipaze yako sauti,
Ziwe mbili au tatu; Pambana popote pale.
Mwenye jibu nipatie, mimi ubongo utandu,
Nimechoka tapatapa, kwa nyingi kauli mbiu,
Washairi mnijibu, Kijukuu chake Robert,
Ziwe mbili au tatu; Kalamu nimeishiwa!.