Shaka: Baadhi ya matamko ya Viongozi wa Upinzani hayana Afya kwa Taifa

Shaka: Baadhi ya matamko ya Viongozi wa Upinzani hayana Afya kwa Taifa

SautiYaMnyonge

JF-Expert Member
Joined
May 13, 2018
Posts
439
Reaction score
742
Na Mwandishi Wetu,

Kutoka Tanga.

-Wataka Rais Samia Asishinikizwe kukutana nao

Mwandishi wetu Tanga.

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesisitiza kitaendelea kutoa mwelekeo wa siasa na uongozi wa nchi kwa vile ndicho kinachounda na kuongoza serikali, hivyo viongozi wa Chama na serikali katika ngazi za Kijiji hadi taifa kwa kiasi kikubwa wote wako katika fatiki za kufuatilia utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya mwaka 2020-2025 ili kutimiza wajibu wake kwa wananchi kwa kuwaondoshea kero na changamoto mbalimbali ili kuharakisha maendeleo.

Kimesema wakati wote Chama cha Mapinduzi kimekuwa chenye dhamira chanya ya kutoshiriki siasa za mti kwa macho, piga nikupige, kuhasimiana kisiasa na kuwagawa wananchi kwa sababu zozote zile, hivyo mwelekeo wake ni kuhimiza siasa safi zinazojali ustawi wa haki, usawa, amani, usalama, umoja na mshikamano na kusimamia maslahi ya wananchi walio wengi.

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa Itikadi na uenezi Shaka Hamdu Shaka ameyasema hayo wakati akizungumza na na wanachi wa Pangani Magharibi mkoani hapa ambapo alisema bado baadhi ya matamko ya viongozi wa upizani hayana afya katika ujenzi wa umoja wa kitaifa hasa kipindi hichi ambacho Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan amejipambanua katika kuwatumikia watanzania bila kuwabagua kwa misingi ya itikadi zao za kisiasa, ukanda, ukabila au udini.

“Matamshi yaliyotamkwa na baadhi ya viongozi wa kisiasa hivi karibuni yamevuka mipaka huku yakiwathibitishia watanzania kuwa baadhi ya vyama hivyo hakuna wanasiasa wenye maarifa na upeo, wenye kutambua dhana ya mgawanyo wa madaraka, wala kuelewa mipaka ya utawala pia yaonesha hawafahamu hadhi, nguvu wala dhamana ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzanai Samia Suluhu Hassan” Alisema Shaka

Shaka amefafanua kuwa hakuna chama chochote cha siasa chenye wajibu wala haki ya kumuamrisha Rais wa nchi na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama au kutoa shinikizo la aina yoyote Zaidi ya kuheshimiwa maamuzi yake anapoataka nani amuone lini ama kwa muda gani na si kwa madai ya kuandika barua na kuchelewa wahusika kupata majibu.

“Hakuna sababu ya kutishana wala kutoa masharti na shinikizo kwa jambo lolote lile kwani ni Rais Samia kwa kuthamini kwake ushirikishwaji wa kila mmoja wetu katika ujenzi wa nchi yetu akaona atafakari ni wakati gani akutane na viongozi wote wa vyama vya siasa sasa wasitake kujifanya ni wao ndio walitaka hilo. Aidha wapo viongozi wa vyama vya upinzani ambao wamekuwa mahiri wa kuchonga, kuzua na kuzusha mambo yanayopotosha, yanayochochea chuki na hata kuathiri umoja na mshikamano wetu lengo lao likiwa ni kutaka kututoa Chama na serikali kwenye mwelekeo wa ujenzi wa nchi yetu na tuanze malumbano nao jambo ambalo kamwe hawatafanikiwa zaidi tutawapa elimu ya siasa safi, uongozi na uzalendo kutokana na viongozi hao kuonekana wamekosa malezi mazuri ya kiuongozi au wamekosa kazi za kufanya.” Alisema Shaka

Shaka yuko katika ziara ya kikazi mkoani Tanga ambapo ataendelea na ziara yake katika wilaya za Muheza na Tanga Mjini. Ziara hiyo inaongozwa na katibu mkuu wa CCM Ndugu Daniel Chongolo ambaye yupo wilaya za Kilindi, Handeni na Korogwe. Wameongozana pia na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Kanali Mstaafu Ndugu Ngemela Lubinga ambaye atapita wilaya za Mkinga, Lushoto na Bumbuli.

IMG_20210613_002954_982.jpg
 
“We do not harbor any illusions about a broad basis of support between our two parties supporters, which I think animated some of the approach back then.

We view the forthcoming meeting with Mbowe and other opposition Party leaders as an important tool to manage what has always been a persistently difficult relationship.”

Kikwete - when he was meeting the US ambassador in his office.
 
Huyu Dogo ajikite kwa kujenga chama chake CCM, swala la Mh.Rais SSH kukutana na wapinzani sio lake tena maana Mh.rais alishaamua atakutana nao, ili kujenga upya mstakabali ya Taifa letu.

Dogo aachane na siasa za kushamba kama walivyoziita mzee Kinana na wenzdke. Jikite kwenye siasa za kistaarabu hatutaku siasa za KUNUNUA wapinzani na kuwatisha kwa kuwabambikia makesi ya kishamba.
 
CCM nzima haina faida kwa wananchi wa Taifa hili na mustakbali wake,itangazwe tu CCM ni janga la Taifa. Ni suala la mida tu Vyama vikuu vya upinzani vitakuja na kauli mbiu ya CCM Ni Janga la Taifa.(CJT)
 
Huyu Dogo ajikite kwa kujenga chama chake CCM , swala la Mh.Rais SSH kukutana na wapinzani sio lake tena maana Mh.rais alishaamua atakutana nao, ili kujenga upya mstakabali ya Taifa letu.Dogo Haachane na siasa za kushamba kama walivyoziita mzee Kinana na wenzdke. Jikite kwenye siasa za kistaarabu hatutaku siasa za KUNUNUA wapinzani na kuwatisha kwa kuwabambikia makesi ya kishamba
Ni kheri wapinzani wakaangalia kauli zao kuhusiana na suala hili.

Mheshimiwa rais ni mtu mstaarabu na mwenye malengo ya dhati kabisa ya kutaka Tanzania iendelee. Na ndio maana ameamua kushirikisha kila mtu katika kuijenga nchi.

Rais kusema atakutana na chadema haijaandikwa kwenye msahafu kwamba haiwezi futika au badilishwa. Anaweza asikutane wala nini na makutano yakawa kwenye kampeni mwaka 2025 na Chadema hawatakuwa na cha kumfanya.
 
CCM nzima haina faida kwa wananchi wa Taifa hili na mustakbali wake,itangazwe tu CCM ni janga la Taifa. Ni suala la mida tu Vyama vikuu vya upinzani vitakuja na kauli mbiu ya CCM Ni Janga la Taifa.(CJT)
Tatizo hatuna upinzani imara, watu tuliowaamini wametuangusha (Mdee, Matiko, Slaa, Lipumba, Lowasa, Sumaye, Katambi, Mwita, Gekul...mifano ni mingi), kwa hilo sioni wa kuongoza nchi hii kwa sasa CCM wakiondoka.

Hawa akina Mbowe, Mnyika kelele nyingi jukwaani, lakini ni ngumu sana kuaminika kwa watu wengi kwa tabia walizoonesha since 2014 hadi leo hii.
 
Ni kheri wapinzani wakaangalia kauli zao kuhusiana na suala hili.

Mheshimiwa rais ni mtu mstaarabu na mwenye malengo ya dhati kabisa ya kutaka Tanzania iendelee. Na ndio maana ameamua kushirikisha kila mtu katika kuijenga nchi.

Rais kusema atakutana na chadema haijaandikwa kwenye msahafu kwamba haiwezi futika au badilishwa. Anaweza asikutane wala nini na makutano yakawa kwenye kampeni mwaka 2025 na Chadema hawatakuwa na cha kumfanya.
Kuna kitu huyu Shaka anakikosa au haelewi.

Ni upungufu mkubwa kuamini kuwa Rais hawezi kushinikizwa. Wananchi au makundi fulani yana uwezo wa kumshinikiza Rais, japo si lazima Rais afanye kama wanaoshinikiza wanavyotaka. Zaidi inategemea nguvu ya hilo kundi.

Wananchi au kundi fulani wana uwezo na haki ya kushinikiza kukutana au kulazimisha Rais awasikilize. Hicho ni kitu cha kawaida kwenye demokrasia. Ndiyo maana unakuta watu wanaandamana wanafanya migomo, yote hayo yanakuwa ni mashinikizo.

Kama vyama vya upinzani viliomba kukutana na Rais, vina uwezo wa kujipangia muda wa kusubiria. Muda huo ukipita, vina haki ya kwenda kwenye plan B, kama wanayo. Kwa sababu huwezi kusubiria milele.
 
Tafadhali mwenye namba ya shaka ya Simu ya mkononi please naionba
 
SHAKA
Kama Rais alishawajibu hiyo sio kazi yako yakutafsiri,mwachie msemaji was serikali.
Aliandikiwa kama Rais.
Umeanza mapema kuonesha uwezo wako mdogo kiutendaji.Acha CDM wajikoroge
 
Back
Top Bottom