Shambulio la Lissu: Wajue wasiojulikana watakaojulikana na 'Wasiojulikana' ambao kamwe, hawatajulikana

Naona mipasho na porojo za vibarazani uswahilini tu.Waliofanya tukio hilo wanajulikana na ndio hao walioondoa CCTV eneo la tukio na ndio hao waliohakikisha kuwa walinzi wrote wanaondolewa siku hiyo
Herry kisanduku na Le mutuz ukiwakuta huko mtaani wabane au wape michepuko wakilewa wanatoa siri zote na sasa wanashinda na kukesha kwa waganga wa kienyeji wakitamani ndege itakayombeba Lisu kuja Tanzania ipotelee kwenye Mawingu iende mbinguni kutua isije Tanzania, maana wanahofia kutajwa Live kisha nguvu ya umma kuwapa Taabu sana.
 
Hii ni sinema moja nzuri ya kumtafuta asiyejulikana aliyewatuma wasiojulikana kawaida ya sinema umdhaniae sie ndo hua ndie na umdhaniae ndie kumbe sie inategemea tusubiri mwisho wa hii sinema.
 
Paskali, mwanzoni nilidhani na wewe huwajui "Wasiojulikana" na Wasiojulikana. Lakini nimeacha imani hiyo. Unawajua wote wa aina mbili na ndo maana unakimbilia kukosoa thread yangu badala ya kujikita na maswali niliyouliza.
Mkuu Baija, nchi inaongozwa kama familia, hata wewe ukiwa nyumbani, kama mtoto wa kiume unaejitambua, siku mama yenu amesafiri kwenda kijijini kwao kusalimia, huku nyuma baba akaingiza mgeni, na ukamuona. Kumbe yule mgeni aliacha chumbani kwa baba nguo yeke fulani, bila baba kujua, ama kwa kusahau kwa bahati mbaya ama kwa makusudi ili mwenye nyumba ajue hayuko peke yake.

Mama aliporudi, kukaibuka ugomvi mkubwa kati ya baba na mama kuhusu hiyo nguo imetoka wapi na imeachwa na nani?.

Baba kamwambia mama hamjui mwenye nguo hiyo wala hajui imeingiaje,labda watoto au msichana wa kazi alijichanganya.

Kwa vile wewe uliona picha nzima, jee utamweleza mama ukweli wa ulichoona?.

Hiyo ndio essence ya wasiojulikana hawa
Shambulio la Lissu: Wajue Wasiojulikana Watakaojulikana na 'Wasiojulikana' Ambao Kamwe, Hawatajulikana!. - JamiiForums

Kama baba amesema hajui nguo imefikaje, who are you kusema imefikaje?.

Kama yule aliyemshikia Nape bastola naye hajulikani mpaka leo anatafutwa na polisi, what are the chances kuwabaini julikana wa Lissu?.

Wana familia bora, wanamwamini baba mwenye nyumba, hata kama wewe ulimuona mgeni wa baba, lakini hukumshuhudia wakati akiivua hiyo nguo na kuiacha uvunguni mwa kitanda chumbani kwa baba, hivyo kama baba kasema hajui, then it migh be true, baba hajui, na hiyo nguo iliachwa siku nyingi nyuma na mgeni mwingine ambaye hata wewe hukumuona.
P
Hivyo nilitoa angalizo hili
Tuacheni Ramli Chonganishi: Tusihukumu, Tusije Tukahukumiwa!. "Karma Ndio Pekee Hutoa Hukumu ya Haki Hapa Duniani!. - JamiiForums

Kwenye hili la kuwabaini wasiojulikana wa Tundu Lissu, serikali yetu imeshindwa, nilisema humu, kwa vile tupo watu wenye uwezo kuisaidia serikali yetu iweze kuwabaini, nikauliza jee tujitolee tuu kuwabaini na kuwataja, kuisaidia serikali yetu au tuisubiri, serikali iseme imeshindwa ndipo isaidiwe?.

WanaJF, Je tuisaidie Serikali yetu inaposhindwa au tusubiri ishindwe, tuibeze na kuizomea kuwa haiwezi? - JamiiForums

P .
 

na wawekezaji wa madini
 
Ukweli wa hili wanalo jeshi la polisi na wala hawawezi kulikwepa. Mosi ni kwa nini walinzi waliondolewa kwenye eneo lao la lindo na nani aliwaondoa na siku hiyo walinzi walikuwa kina nani, pili CCTV camera ziliondolewa na nani na kwa nini ziondolewe? Vitu viwili hivi kama yupo anayeweza kuhojiwa akajibu basi tubaweza kupata muelekeo. Naona nguvu ya serikali inajikita tu kuwa Lisu anaichafua serikali kwa kutaja slichofanyiwa. Wao hawataki kuuliza viswali viwili na hata kuwabana wshusika juu ya " why the guards were not at their post area of guard and why CCTV cameras were removed, and who did it" Serikali makini isingeshughulika na waombezi wa Lisu kwa kupiga ban fulana na ibada za wazi. Na bado wanaomhutaji Lisu home ni wale ambao walitumika kuharass waombezi wake, bado kuna sintofahamu kubwa juu ya sakata hili. Unadhani ipo siku mmojawao ataropoka tu kuwa " aaaah tulimkosa" na hapo ndipo tutajua hadithi yote ilivyokaa
 
Mkuu Evarist, kwa vile unakiri kufanya vitu visivyo sawia, ukaungama, kwa ushauri tuu, kwa mujibu wa kanuni ya karma, kuungama pekee hakutoshi, inakubidi kufanya mema mengi ili kupindua ule uovu!.

Jee inawezekana hata tukio la Lissu likawa ni vijana wenu?.
P.
 
Leo siku ya tarehe 7/Sept. 2019 ni siku ya kumbukumbu ya miaka miwili toka Mh.Tundu Lisu aliposhambuliwa kwa risasi na watu wasiojulikana. Mpaka leo bado wasiojulikana hawa bado hawatajulikana na uchunguzi mkubwa, makini na mkali wa Jeshi letu adilifu la polisi, unaendelea kuwabaini wasiojulikana hawa, hivi sasa kuna mashuhuda wawili muhimu sana, wanasubiriwa wao tuu kuhojiwa ndipo taarifa rasmi ya polisi kuhusu maendeleo ya uchunguzi huu ndipo ilatolewa.

Tuvute subra.
Get well soon Mhe. Tundu Lissu and welcome back home.
P
 
  1. Ina maana hujui nani kaamuru kuawa Ben Saanane?
  2. Hujui nani kaamuru Tundu Lissu ashambuliwe?
  3. Hujui nani alikuwa nyuma ya utekaji wa Mo Dewji ?
Nakuheshimu kitu kimoja, unatumia verified ID, lakini ukweli unaujua. Tuishie hapa
Kwanza nakushukuru kwa kuniheshimu kutumia verified name. Licha ya kutumia verified name pia mimi ni mwana habari, jukumu kuu la waandishi wa habari ni tell nothing but the truth. Hivyo mimi ni mkweli daima na yote niandikayo humu ni kweli tupu.

Kuamini ni jambo moja na kuwa na hakika ni jambo jingine. Nakuomba mambo ya imani, tuyaache kwenye dini, hapa tuzungumzie vitu vyenye uhakika na sio masuala ya imani.
  1. Ina maana hujui nani kaamuru kuawa Ben Saanane?. Kwanza sina uhakika kama Ben Saanane ameuwawa, wewe ndio unanieleza sasa. Nijuavyo mimi ni Ben Saanane ametoweka katika mazingira ya kutatanisha, mpaka sasa hakuna ajuaye kilichomkuta. Kumbe mwenzetu unajua kuwa kauwawa na una mjua hadi aliyeamuru Ben Saanane kuuwawa!. Una uhakika wa hili?.
  2. Hujui nani kaamuru Tundu Lissu ashambuliwe?. Pia simjui aliyeamuru Tundu Lissu ashambuliwe, kwenye hili la Tundu Lissu, mimi naungana na mamlaka rasmi kuwa Tundu Lissu ameshambuliwa na watu wasiojulikana, na nimeisha andika mabandiko mengi kuhusu shambulio la Tundu Lissu. Vipi wewe mwenzetu unamjua aliyeamrisha Tundu Lissu ashambuliwe, una uhakika?.
  3. Hujui nani alikuwa nyuma ya utekaji wa Mo Dewji ?. Hata aliye nyuma ya shambulio hili mimi simjui, wewe mwenzetu unamjua?. Una uhakika?.
P
 
Haya sasa kazi ya kuwatambua wasiojulikana kupitia kwa karma inaanza taratibu, Marekani imeanza kuwasaidia!, tunaianza safari mdogo mdogo mwisho wa siku, wasiojulikana watajulikana tuu!.
P
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…